Tanzania yakopa bilioni 310 EXIM kutanua mfumo wa NIDA

Tanzania yakopa bilioni 310 EXIM kutanua mfumo wa NIDA

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Mkopo Tanzania.jpg

Serikali ya Jamhuri ya Korea imeipatia Tanzania mkopo wa gharama nafuu wa Tsh. Bilioni 310 kwa ajili ya upanuzi wa mfumo wa utambuzi wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) pamoja na uendelezaji na utunzaji wa mfumo wa taarifa za ardhi.

Hafla ya utiaji saini wa mikataba hiyo baina ya Serikali ya Tanza na Korea Kusini itakayotolewa kupitia benki ya Exim ya Korea, imefanyika leo Alhamisi, Oktoba 27, 2022 katika ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wa Korea Kusini iliyopo Seoul.

Mkataba wa awamu ya pili ya mradi wa upanuzi wa mfumo wa utambuzi wa NIDA una thamani ya Tsh. Bilioni 161 na mkataba wa uendelezaji na utunzaji wa mfumo wa taarifa za ardhi ambao una thamani ya Tsh. Bilioni 149.

Akizungumza wakati wa halfa hiyo ambayo ambayo pia ilishuhudiwa na Waziri Mkuu wa Korea Han Duck-Soo, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema kuwa Tanzania na Korea zinajivunia mahusiano yaliyodumu kwa miaka 30 ambayo yamekuwa chachu katika kukuza uchumi wa nchi hizo mbili katika sekta mbalimbali.

Viongozi wengine waliohudhuria hafla hiyo ni pamoja na Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk, Balozi wa Tanzania Nchini Korea Kusini, Balozi Togolani Mavura, Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Fedha na Mipango Zanzibar, Aboud Hassan Mwinyi na watendaji wengine wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
Aisee kazi inaendelea.

NIDA walikosea taarifa hasa tarehe za kuzaliwa, mtu akienda kubadilisha anaambiwa alipie Tsh20,000/=.
Kosa lao ila mimi ndio mlipaji.
 
Mnakopa hela mnaenda kugawana ..Ni kidogo Sana zinaenda zilikokusudiwa
 
Mfumo wa NIDA ulianzishwa na Waziri wa mambo ya ndani wakati huo (Lawrence Masha) chini ya DG Mwaimu, toka wajenge mfumo na card za utambulisho kuanza kuzalishwa, mfumo huu una chini ya miaka 15; what is so urgent mpaka kukopa zaidi ya 300bn ili kuboresha mfumo?

Maana nikopo ya aina hii, in most cases, Bank inatia mkopo kwa condition anaetakuwa kutoa huduma anatokea Korea. Hivyo, ni kama unakopa, unasaini mkopo na mtoa huduma anasaini kuwa contracted, ni kama fedha inahama bank ya Korea kwenda bank nyingine ya Korea na Tanzania anabakia mdaiwa.

Unless kama tuna IT big corporation za Watazania kweli fedha tutaiona, japo tutalazimika kununua hardware equipment tutajikuta tunanunua LG, Samsung and the likes toka S Korea tena.

Labda tuulize kwa kuangalia namna ya kukuza uchumi wetu kwenye majors. Tanzania imezungukwa na nchi 8 na kuna potential kuzifika nchi zaidi kwenye soko la Africa. Kwanini mkopo toka Exim Bank ya Korea usiende kwenye kuimarisha uzalishaji wa mpunga ili chakula nchini kiwe cha kutosha na kuongeza exports.
Kwanini mkopo usiwe sehemu ya kubadili uchumi wa blue kwa kuzalisha samaki wa kutosha kukidhi lishe ya Watanzania (mauzo ya samaki ni biashara kubwa sana) na hivyo Tanzania kuwa amongst top earners via mauzo ya samaki?

Angalia mahitaji ya fish sausages na bado mzingo wahitajika sokoni
Amazon product ASIN B09HWT3BP1


Kila la heri viongozi wetu kwenye kuijenga nchi.

Hepi furahidei.

Freddie
 
Mfumo wa NIDA ulianzishwa na Waziri wa mambo ya ndani wakati huo (Lawrence Masha) chini ya DG Mwaimu, toka wajenge mfumo na card za utambulisho kuanza kuzalishwa, mfumo huu una chini ya miaka 15; what is so urgent mpaka kukopa zaidi ya 300bn ili kuboresha mfumo?

Maana nikopo ya aina hii, in most cases, Bank inatia mkopo kwa condition anaetakuwa kutoa huduma anatokea Korea. Hivyo, ni kama unakopa, unasaini mkopo na mtoa huduma anasaini kuwa contracted, ni kama fedha inahama bank ya Korea kwenda bank nyingine ya Korea na Tanzania anabakia mdaiwa.

Unless kama tuna IT big corporation za Watazania kweli fedha tutaiona, japo tutalazimika kununua hardware equipment tutajikuta tunanunua LG, Samsung and the likes toka S Korea tena.

Labda tuulize kwa kuangalia namna ya kukuza uchumi wetu kwenye majors. Tanzania imezungukwa na nchi 8 na kuna potential kuzifika nchi zaidi kwenye soko la Africa. Kwanini mkopo toka Exim Bank ya Korea usiende kwenye kuimarisha uzalishaji wa mpunga ili chakula nchini kiwe cha kutosha na kuongeza exports.
Kwanini mkopo usiwe sehemu ya kubadili uchumi wa blue kwa kuzalisha samaki wa kutosha kukidhi lishe ya Watanzania (mauzo ya samaki ni biashara kubwa sana) na hivyo Tanzania kuwa amongst top earners via mauzo ya samaki?

Angalia mahitaji ya fish sausages na bado mzingo wahitajika sokoni
Amazon product ASIN B09HWT3BP1


Kila la heri viongozi wetu kwenye kuijenga nchi.

Hepi furahidei.

Freddie
Huo mkopo wamepewa,trust me, shida zitabaki pale pale hakuna jipya

Ova
 
Deni la taifa litakuwa limefikia sh ngapi[emoji848][emoji848]
 

Serikali ya Jamhuri ya Korea imeipatia Tanzania mkopo wa gharama nafuu wa Tsh. Bilioni 310 kwa ajili ya upanuzi wa mfumo wa utambuzi wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) pamoja na uendelezaji na utunzaji wa mfumo wa taarifa za ardhi.

Hafla ya utiaji saini wa mikataba hiyo baina ya Serikali ya Tanza na Korea Kusini itakayotolewa kupitia benki ya Exim ya Korea, imefanyika leo Alhamisi, Oktoba 27, 2022 katika ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu wa Korea Kusini iliyopo Seoul.

Mkataba wa awamu ya pili ya mradi wa upanuzi wa mfumo wa utambuzi wa NIDA una thamani ya Tsh. Bilioni 161 na mkataba wa uendelezaji na utunzaji wa mfumo wa taarifa za ardhi ambao una thamani ya Tsh. Bilioni 149.

Akizungumza wakati wa halfa hiyo ambayo ambayo pia ilishuhudiwa na Waziri Mkuu wa Korea Han Duck-Soo, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema kuwa Tanzania na Korea zinajivunia mahusiano yaliyodumu kwa miaka 30 ambayo yamekuwa chachu katika kukuza uchumi wa nchi hizo mbili katika sekta mbalimbali.

Viongozi wengine waliohudhuria hafla hiyo ni pamoja na Naibu Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk, Balozi wa Tanzania Nchini Korea Kusini, Balozi Togolani Mavura, Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Fedha na Mipango Zanzibar, Aboud Hassan Mwinyi na watendaji wengine wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Hiyo kazi ni ngumu hivyo mpaka tunaikopea mahela yote hayo
 
Naona kuna Waziri wa Zanzibar kwenye ziara ya muungano. No wonder Wazanzibar wameridhika sana awamu hii..... Imagine mpaka akina Jussa wamekana kimya.
Hao hautawasikia hadi rais atoke bara ndiyo utasikia makelele yao

Wataanza mara Zanzibar alikuwa na kiti UN, mara mafuta siyo ya muungano yaani vurugu tupu
 
Mfumo wa NIDA ulianzishwa na Waziri wa mambo ya ndani wakati huo (Lawrence Masha) chini ya DG Mwaimu, toka wajenge mfumo na card za utambulisho kuanza kuzalishwa, mfumo huu una chini ya miaka 15; what is so urgent mpaka kukopa zaidi ya 300bn ili kuboresha mfumo?

Maana nikopo ya aina hii, in most cases, Bank inatia mkopo kwa condition anaetakuwa kutoa huduma anatokea Korea. Hivyo, ni kama unakopa, unasaini mkopo na mtoa huduma anasaini kuwa contracted, ni kama fedha inahama bank ya Korea kwenda bank nyingine ya Korea na Tanzania anabakia mdaiwa.

Unless kama tuna IT big corporation za Watazania kweli fedha tutaiona, japo tutalazimika kununua hardware equipment tutajikuta tunanunua LG, Samsung and the likes toka S Korea tena.

Labda tuulize kwa kuangalia namna ya kukuza uchumi wetu kwenye majors. Tanzania imezungukwa na nchi 8 na kuna potential kuzifika nchi zaidi kwenye soko la Africa. Kwanini mkopo toka Exim Bank ya Korea usiende kwenye kuimarisha uzalishaji wa mpunga ili chakula nchini kiwe cha kutosha na kuongeza exports.
Kwanini mkopo usiwe sehemu ya kubadili uchumi wa blue kwa kuzalisha samaki wa kutosha kukidhi lishe ya Watanzania (mauzo ya samaki ni biashara kubwa sana) na hivyo Tanzania kuwa amongst top earners via mauzo ya samaki?

Angalia mahitaji ya fish sausages na bado mzingo wahitajika sokoni
Amazon product ASIN B09HWT3BP1


Kila la heri viongozi wetu kwenye kuijenga nchi.

Hepi furahidei.

Freddie
Kaka wanataja mikopo kwenye mambo ambayo sio rahisi mwananchi kuyaelewa wala kuhoji au kuona umuhimu wake wa moja kwa moja ili UPIGWAJI uwe rahisi

Nani atahoji au anajua expenditure kwenye hiyo miundo mbinu?

Hizo pesa zingeenda kwenye changamoto zinazowagusa wananchi moja kwa moja kama umwagiliaji au kilimo lau kungekua na tija
 
Kaka wanataja mikopo kwenye mambo ambayo sio rahisi mwananchi kuyaelewa wala kuhoji au kuona umuhimu wake wa moja kwa moja ili UPIGWAJI uwe rahisi

Nani atahoji au anajua expenditure kwenye hiyo miundo mbinu?

Hizo pesa zingeenda kwenye changamoto zinazowagusa wananchi moja kwa moja kama umwagiliaji au kilimo lau kungekua na tija
Kwa kweli kukopa pesa ndefu kama hiyo kwa ajili ya kuimarisha miundo mbinu ya NIDA ni uzuzu.

Wenye akili wanakopa pesa kwa ajili ya infrastructure au huduma muhimu za jamii kama afya au elimu.

Kwa kweli haya MaCCM huwa nashindwa kuyaelewa priorities zao. Yani wao wanaowaza matumbo yao tu.
 
Back
Top Bottom