Tanzania Yasaidia Kuleta Muafaka Kenya


JK was there kwa capacity ya Mwenyekiti wa Au na alikuwa mtu wa kushuhudia na si zaidi .Siamini kama Kenya wanaweza kumsikiliza JK ama Ben Mkapa maana wanajua yale ya Kenya yametokea Kiteto na Zanzibar kote damu ilimwagika
 
..wanaostahili pongezi ni viongozi wa kenya na wasuluhishi[annan,machel,mkapa] walioketi wiki kadhaa kutafuta muafaka.

..watanzania tunapenda sana miujiza. kuamini kwamba maridhiano haya yametokea kwasababu ya presence ya Kikwete ni kuamini kwamba Kikwete ana nguvu za miujiza.
 

Mkuu Joka kuu,

hata aliyeanzisha hii thread anajua kabisa kuwa since last friday haya makubaliano yalikuwa tayari yamefikiwa na ilikuwa imebaki kusaini tu.

Hapa ni watu wanatafuta good news baada ya kukosa real good news kwa upande wao. Ni vizuri Kikwete ameenda Kenya na sasa inabidi aende SOmalia na Sudan ili nyota yake "izidi kungara" kabla ya kuja nyumbani na kushughulikia mauaji ya wapemba mwaka 2001 na mwafaka wa huko pia!
 
Thanks Lunyungu,

Si kwamba hatutaki kumpongeza JK akifanya vizuri, bali kwa hili nadhani kama kumpongeza ni bwana K.Annan, JK Naona alienda kushudia utiwaji saini tu! Shughuli kubwa ilisha fanywa na wengine!
 

JK umasikini aliukuta, halafu oopssss inahusiana nini na hapa? na kuoa tena? sasa mambo makubwa, dada vipi? umechanganyikiwa?
 
TUombe Mungu watekeleze waliyoamua.

By the way, ni kitu gani hasa wamekubaliana?

ODM walikuwa wanataka PM anayeteua baraza la mawaziri ndo ilivyokubalika?

Na kama ni hivyo ina maanisha nini? PM ni juu ya rais?

Wamepata Hio uPM unaosema Hume.

Raila ni Executive Prime Minister and Leader of Government Business in Parliament. Anateua yeye na kusimamia mawaziri. Yaani he is the Head of Government.

Kibaki is the President and Commander-in-Chief of the Armed Forces. Anamteua PM ambaye kwa sasa lazima awe Raila kulingana na maafikiano. In future huyu PM atakuwa kiongozi mwenye chama chake kina viti vingi zaidi bungeni. Kibaki kama Rais au hata Rais wa awamu nyingine hawezi mvuta PM huyu kazi. Yeye atasema tuu kwamba anataka kumfukuza kazi ila Bunge lazima iidhinishe kutimuliwa kazini kwa PM by majority vote yaani 114 Votes.


Kifupi:
1. Raila Odinga - Prime Minister, Head of Government and Leader of Government Business in Parliament. Atasaidiwa na Makamu wawili toka ODM, chama chake. Raila ndio anawapatia kazi maMinista na kuongoza baraza la mawaziri hawa. Hawezi kuwafuta kazi bila kushauriana na Kibaki. Lazima nusu wawe toka chama chake cha ODM na nusu toka kwa chama cha Kibaki na rafikize (PNU/KANU/ODM-Kenya).

2. Mwai Kibaki - President, Head of State and Leader of The Armed Forces. Atasaidiwa na Makamu wa Rais (Ambaye yeye ndiye anamuandika kazi na kwa sasa ni mpinzani aliyeibuka namba tatu Desemba yaani Kalonzo Musyoka wa ODM-Kenya).

3. ODM ina wingi wa wabunge bungeni.
4. ODM ina wingi wa makansela wa mabunge madogo ya miji na jiji (Municipal and County Councils). Mameya wa miji yote mikubwa ya Kenya- Nairobi, Mombasa, Nakuru, Kisumu, Eldoret, Garissa na Kakamega ni wa chama cha ODM.
 
This is the first major achievement for JK as a AU Chair.
He deserves a pat on the back.
 
This is the first major achievement for JK as a AU Chair.
He deserves a pat on the back.

Nakupinga Dotori. JK amekuwa busy na ufisadi Tanzania na baadaye Bush .Kaenda Kenya for only 2 days wakati mzozo umedumu zaidi ya mwezi na Koffi Annan has been there .Yeye kaenda kushuhudia makubaliano na si kwamba ndiye kapatanisha maana uwezo huo JK hana . Akitaa tumpe pongezi achukue maneno ya Ali Karume na afanye kweli Zanzibar tutampa Hongera .Pale Kenya alienda kama mwenyekiti wa AU .
 
Thanks Lunyungu,

Si kwamba hatutaki kumpongeza JK akifanya vizuri, bali kwa hili nadhani kama kumpongeza ni bwana K.Annan, JK Naona alienda kushudia utiwaji saini tu! Shughuli kubwa ilisha fanywa na wengine!

Wote wanafaa kupongezwa, lakini ngoja nikukumbushe Mzee Roja Mila, alikuwa reserve mechi zake zilizompa sifa kuliko zote, watu wanacheza weeee akiingia yeye tu dakika za mwisho ananyuka bao sifa zote ni zake, lakini "ananyuka bao" ndio muhimu. Na hivyo ndio alivyofanya JK, watu wamecheza weeeeeee, kuingia yeye kanyuka bao.

Team nzima iliyofanya kazi Kenya inastahili sifa zote, pamoja na Kibaki na Raila wanapongezwa sana kufikia makubaliano na JK anapata golden shoes ya kuwa mfungaji bora.
 
JK umasikini aliukuta, halafu oopssss inahusiana nini na hapa? na kuoa tena? sasa mambo makubwa, dada vipi? umechanganyikiwa?

ohh umasikini alikuta as if alitokea saturn, JK amekuwa kiongozi kwenye serikali miaka nenda rudi ikiwemo kuwa kwenye wizara nono na kuhusika na mikataba mingine ambayo leo inatusumbua hapa.

Yeah, kuna mtanzania mmoja mashuhuri aliwashauri watanzania kuwa kama wanampenda mtu kwa sura yake basi wakanywe naye chai. The same argument hapa kwa wewe ambaye unampenda JK binafsi (na wala sio utendaji wake ambao so far ni mbovu) basi inabidi ukumbushwe kuwa the guy is married.

Hapa JF hapendwi mtu bali utendaji wa kazi.
 
"Kibaki is the President and Commander-in-Chief of the Armed Forces. Anamteua PM ambaye kwa sasa lazima awe Raila kulingana na maafikiano. In future huyu PM atakuwa kiongozi mwenye chama chake kina viti vingi zaidi bungeni. Kibaki kama Rais au hata Rais wa awamu nyingine hawezi mvuta PM huyu kazi. Yeye atasema tuu kwamba anataka kumvuta ila Bunge lazima iidhinishe kuvutwa kwa PM by majority vote yaani 114 Votes. "




kumvuta kazi = kumfuta kazi/kumfukuza kazi.
 
This is the first major achievement for JK as a AU Chair.
He deserves a pat on the back.

Dotori,

Naomba ureview mchakato mzima wa hili jambo kabla ya ku comment hivyo!! JK amekuwa huko for only two days ....alienda kushudia utiwaji saini wa makubaliano? hii nayo ni achievement mkuu?
 

Huu ni mfano maiti siwezi kuufikiri hata mara moja .Yaani unaleta akili ya Mpira na real life ya watu wa Kenya ? Kumbuka Kenya ni moto mwingine hakuna goi goi wa kuwaza kama unavyo onyesha hapa .
 
Huu ni mfano maiti siwezi kuufikiri hata mara moja .Yaani unaleta akili ya Mpira na real life ya watu wa Kenya ? Kumbuka Kenya ni moto mwingine hakuna goi goi wa kuwaza kama unavyo onyesha hapa .

yeye hafikiri hili kabisa kwani analinganisha maisha ya watu na mifano ya kitoto kabisa! utetezi wa ufisadi unafilisi mawazo
 

Nikisema ni chuki binafsi unakasirika, hili sikujibu sio thread yake hapa, usichanganye mada, hapa JK anapewa sifa anazostahiki kwa kazi nzuri aliyoifanya as Mkuu wa AU.

Married tena sio mmoja ana watatu wenye sifa zote za haiba na si kama wewe (mara nanihii mara nanihii) na nasikia kaongeza wanne. labda wewe utajuwa zaidi hebu nitonye kidogo.
 
Nikisema ni chuki binafsi unakasirika, hili sikujibu sio thread yake hapa, usichanganye mada, hapa JK anapewa sifa anazostahiki kwa kazi nzuri aliyoifanya as Mkuu wa AU.

wewe ndio una hasira hapa baada ya juhudi za kutaka kufungia JF na kukamata wana JF kushindwa sasa umeamua kuja hapa na kuflood hii forum na pumba zako!

Married tena sio mmoja ana watatu wenye sifa zote za haiba na si kama wewe (mara nanihii mara nanihii) na nasikia kaongeza wanne. labda wewe utajuwa zaidi hebu nitonye kidogo.

Kama unajua hili natumai utaacha kujikombakomba kwake kwa sasa!
 
Nami naungana na wengine wote kumpongeza JK ni heshima kwa Tz na yaweza kuwa chanzo cha amani Kenya!

Annan anafanya mediation under AU ambaye Raisi wake ni JK

Hii ni nzuri kwani yaonnyesha Afrika we can solve our own problems sii lazima wazungu wahusike!

Hongera JK, Hongera TZ, Hongereni Kibaki na Raila, Hongera AEC, hongera AU

Pia tusimsahau mzee BWM na mama Grace Mandela!

Kama walivyosema wengine- sasa iwe nguvu kubwa Darfur na Somalia as Burundi, DRC na Uganda hali zimeanza sasa kutengemaa!
 
Heshima mbele.....

Naomba niungane na wale wanaotoa pongezi kwanza kwa waKenya wote, pili ni vyama vya siasa vyote, tatu ni kamati ya usuluhishi iliyoongozwa na Kofi A na mwisho but NOT LEAST to JK, RAIS WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika kwa kazi kubwa waliyoifanya kumaliza ghasia za kule kwa jirani zetu wa Kenya....

Kazi waliyopewa wasuluhishi wameitekeleza with flying colours na sasa tuwaombee Mungu ndugu zetu wa Kenya wadumishe amani na kuyatimiza yale waliyokubaliana........

Mungu Ibariki Afrika!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…