Tanzania yashiriki katika Mkutano wa Dunia wa Jumuiya ya Habari (WSIS), nchini Uswisi

Tanzania yashiriki katika Mkutano wa Dunia wa Jumuiya ya Habari (WSIS), nchini Uswisi

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
photo_2024-05-27_16-14-51.jpg

photo_2024-05-27_16-14-50.jpg
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Moses Nnauye (MB), akiongozana na Naibu Katibu Mkuu, Nicholaus Mkapa ameongoza kikao kazi cha ujumbe wa Tanzania katika ofisi ya balozi na mwakilishi wa wakudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa kabla ya Mkutano wa Dunia wa Jumuiya ya Habari (WSIS) kwa mwaka 2024 (WSIS 2024).

Mkutano huu unalengo la kujadili masuala mbalimbali ya TEHAMA na uwezo wake katika kukuza maendeleo, kuimarisha upatikanaji wa habari na maarifa, kuchochea ustadi na kuhamasisha matumizi ya TEHAMA kwa maendeleo ya kijamii na kiuchumi..Mkutano huu unafanyika jijini Geneva, Uswisi kuanzia tarehe 27 hadi 31 Mei 2024.

Ushiriki wa Tanzania kwenye mkutano huu ni moja ya jitihada katika kuimarisha mashirikiano yake Duniani katika kukabili changamoto mbalimbali katika TEHAMA na kuongeza tija katika utekelezaji wa miradi ya TEHAMA.
photo_2024-05-27_16-14-49.jpg
 
Back
Top Bottom