joto la jiwe
JF-Expert Member
- Sep 4, 2017
- 26,117
- 46,617
TANZANIA imetajwa kuwa mzalishaji mkubwa wa mazao ya nafaka katika ukanda wa Afrika Mashariki, huku pia ikitajwa kuwa na fursa kubwa ya kutawala soko la Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika(SADC) kwa kutumia fursa za kilimo cha umwagiliaji.
Mfano umetolewa kwenye zao la mpunga, ambalo kwa sasa uzalishaji wake nchini umefikia tani milioni 2.1, wakati nchi za Kenya, Uganda uzalishaji wa zao hilo ni kati ya tani 100,000 na 200,000 tu.
Akizungumzia fursa hiyo kwa Tanzania wakati wa Maonesho ya Kilimo, Ufugaji na Uvuvi yaliyofanyika kitaifa mkoani Simiyu mapema mwezi huu, Mkuu wa Kitengo cha Ukaguzi na Udhibiti Ubora wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC), Daniel Manase, alisema maboresho kwenye sekta ya kilimo cha umwagiliaji ndiyo yaliyoleta manufaa hayo.
Alisema baada ya kuundwa NIRC na kuanza kutekeleleza majukumu yake rasmi mwaka 2015, eneo linalomwagiliwa nchini limeongezeka kutoka hekta 461,333 mwaka 2015, hadi kufika hekta 694,715 mwaka huu.
Aidha, alisema skimu za umwagiliaji 2,555 zimesambaa nchi nzimam hivyo kutoa fursa kwa Tanzania kufanya vizuri zaidi kwenye kilimo hicho, huku fursa ya kuteka soko la EAC, SADC na Afrika kwa ujumla ikiwa kubwa endapo mkazo zaidi utawekwa kwenye kilimo hicho.
Akizungumzia kilimo cha umwagiliaji kwa nchi za Afrika Mashariki, Manase alisema Tanzania ikilinganishwa na mataifa mengine, ina fursa kubwa ya kuwa mzalishaji mkubwa wa mazao ya nafaka katika Afrika kupitia kilimo cha umwagiliaji.
Alisema kwa mwaka, Tanzania hupata mvua ya wastani wa milimita 950, huku eneo linalolimwa mpunga kwa sasa likiwa hekta milioni 1.23 na eneo lililoendelezwa kwa umwagiliaji likiwa hekta 694,715.
Alisema uzalishaji wa mpunga nchini kwa sasa ni tani milioni 2.01 kwa mwaka, huku tija ikiwa ni tani 1.5 hadi 8.1 kwa hekta.
Alisema Tanzania ina eneo la hekta milioni 29.4zinazofaa kwa kilimo cha umwagiliaji na kati ya hizo, milioni 2.3zina uwezekano mkubwa wa kumwagiliwa, milioni 4.8zina uwezekano wa kati na milioni 22.3zina uwezekano mdogo wa kumwagiliwa.
Manase alisema hivi sasa Tanzania inajitosheleza kwa chakula na ina akiba tani milioni 2.79, ambazo zimetokana na mikakati ya nchi kwenye kilimo kwa kutumia pembejeo bora, kuimarisha mifumo ya kilimo na kutoa fursa ya mikopo ya kilimo bila riba.
Kwa upande wa Kenya, hupata mvua ya wastani wa milimita 500 hadi 2,000 kwa mwaka, huku eneo linalomwagiliwa likiwa hekta 125,000 na jumla ya eneo linalofaa kwa umwagiliaji ni hekta 1.3 na uzalishaji wa mpungua kwa sasa ni wastani wa tani 150,000, huku tija ya uzalishaji wa mpunga kwa sasa ni tani 1.1 hadi 5.2 kwa hekta.
Nchini Uganda, uzalishaji wa mpunga umetajwa kuwa wastani wa tani 215,000, wakati mahitaji ya nafaka hiyo ni tani zaidi ya 230,000, hivyo kuwa na mahitaji ya kuagiza mchele kutoka nje ya nchi hiyo.
Hata hivyo, eneo linalofaa kwa umwagiliaji kwa ujumla nchini Uganda ni hekta milioni 3.03, lakini lililoendelezwa kwa kilimo hicho ni dogo ikilinganishwa na ukubwa uliopo.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka Shirika la Chakula Duniani (FAO), kilimo cha umwagiliaji kimechangia kuongeza tija ya uzalishaji na uzalishaji wa mazao mbali mbali katika miongo ya karibuni barani Afrika na na kutaka mkazo uwekwe na nchi hizo kukiendeleza kwa sababu ndio eneo bora zaidi lenye tija ya kweli.
Mafanikio mengini ya kilimo cha umwagiliaji ni kupitia mazao ya mbogamboga, ambapo Meneja Mazingira ya Biashara wa Taasisi Binafsi inayoundwa na wadau wa mnyororo wa thamani wa kilimo cha mbogamboga, matunda na viungo (Taha), Kelvin Remen, amesema kina tija iwapo wakulima wataweka mkazo.
Tanzania yawa kinara uzalishaji nafaka EAC
========
MY TAKE: Hivi kweli kuna mkenya ambaye bado anadhani Kenya inaweza kushindana na Tanzania?
Mfano umetolewa kwenye zao la mpunga, ambalo kwa sasa uzalishaji wake nchini umefikia tani milioni 2.1, wakati nchi za Kenya, Uganda uzalishaji wa zao hilo ni kati ya tani 100,000 na 200,000 tu.
Akizungumzia fursa hiyo kwa Tanzania wakati wa Maonesho ya Kilimo, Ufugaji na Uvuvi yaliyofanyika kitaifa mkoani Simiyu mapema mwezi huu, Mkuu wa Kitengo cha Ukaguzi na Udhibiti Ubora wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC), Daniel Manase, alisema maboresho kwenye sekta ya kilimo cha umwagiliaji ndiyo yaliyoleta manufaa hayo.
Alisema baada ya kuundwa NIRC na kuanza kutekeleleza majukumu yake rasmi mwaka 2015, eneo linalomwagiliwa nchini limeongezeka kutoka hekta 461,333 mwaka 2015, hadi kufika hekta 694,715 mwaka huu.
Aidha, alisema skimu za umwagiliaji 2,555 zimesambaa nchi nzimam hivyo kutoa fursa kwa Tanzania kufanya vizuri zaidi kwenye kilimo hicho, huku fursa ya kuteka soko la EAC, SADC na Afrika kwa ujumla ikiwa kubwa endapo mkazo zaidi utawekwa kwenye kilimo hicho.
Akizungumzia kilimo cha umwagiliaji kwa nchi za Afrika Mashariki, Manase alisema Tanzania ikilinganishwa na mataifa mengine, ina fursa kubwa ya kuwa mzalishaji mkubwa wa mazao ya nafaka katika Afrika kupitia kilimo cha umwagiliaji.
Alisema kwa mwaka, Tanzania hupata mvua ya wastani wa milimita 950, huku eneo linalolimwa mpunga kwa sasa likiwa hekta milioni 1.23 na eneo lililoendelezwa kwa umwagiliaji likiwa hekta 694,715.
Alisema uzalishaji wa mpunga nchini kwa sasa ni tani milioni 2.01 kwa mwaka, huku tija ikiwa ni tani 1.5 hadi 8.1 kwa hekta.
Alisema Tanzania ina eneo la hekta milioni 29.4zinazofaa kwa kilimo cha umwagiliaji na kati ya hizo, milioni 2.3zina uwezekano mkubwa wa kumwagiliwa, milioni 4.8zina uwezekano wa kati na milioni 22.3zina uwezekano mdogo wa kumwagiliwa.
Manase alisema hivi sasa Tanzania inajitosheleza kwa chakula na ina akiba tani milioni 2.79, ambazo zimetokana na mikakati ya nchi kwenye kilimo kwa kutumia pembejeo bora, kuimarisha mifumo ya kilimo na kutoa fursa ya mikopo ya kilimo bila riba.
Kwa upande wa Kenya, hupata mvua ya wastani wa milimita 500 hadi 2,000 kwa mwaka, huku eneo linalomwagiliwa likiwa hekta 125,000 na jumla ya eneo linalofaa kwa umwagiliaji ni hekta 1.3 na uzalishaji wa mpungua kwa sasa ni wastani wa tani 150,000, huku tija ya uzalishaji wa mpunga kwa sasa ni tani 1.1 hadi 5.2 kwa hekta.
Nchini Uganda, uzalishaji wa mpunga umetajwa kuwa wastani wa tani 215,000, wakati mahitaji ya nafaka hiyo ni tani zaidi ya 230,000, hivyo kuwa na mahitaji ya kuagiza mchele kutoka nje ya nchi hiyo.
Hata hivyo, eneo linalofaa kwa umwagiliaji kwa ujumla nchini Uganda ni hekta milioni 3.03, lakini lililoendelezwa kwa kilimo hicho ni dogo ikilinganishwa na ukubwa uliopo.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka Shirika la Chakula Duniani (FAO), kilimo cha umwagiliaji kimechangia kuongeza tija ya uzalishaji na uzalishaji wa mazao mbali mbali katika miongo ya karibuni barani Afrika na na kutaka mkazo uwekwe na nchi hizo kukiendeleza kwa sababu ndio eneo bora zaidi lenye tija ya kweli.
Mafanikio mengini ya kilimo cha umwagiliaji ni kupitia mazao ya mbogamboga, ambapo Meneja Mazingira ya Biashara wa Taasisi Binafsi inayoundwa na wadau wa mnyororo wa thamani wa kilimo cha mbogamboga, matunda na viungo (Taha), Kelvin Remen, amesema kina tija iwapo wakulima wataweka mkazo.
Tanzania yawa kinara uzalishaji nafaka EAC
========
MY TAKE: Hivi kweli kuna mkenya ambaye bado anadhani Kenya inaweza kushindana na Tanzania?