Tanzanian MPs Msigwa na Lema KTN Kenya kuhusu Lissu n.k

vitu visible ndio vp hivyo?? hivi jimboni kwa msigwa umefika ukahoji. wananchi wake au umekaa kwenye ofisi ya ghorofani yenye AC ndio unamjua msigwa sana kuliko wananchi waliompa madiwani 80% pamoja na kura za heshima je kma angekuwa hajafanya maendeleo angeshinda??

anyway unasema kuongea hujui kelele zao ndio zimesababisha bandarini watumbuliwe zimesababisha makontena yazuiwe, na mengineyo hivi bila upinzani kupiga kelele muswada wa gesi leo hii ungebadilishwa??

mkuu sometimes have respect kwa opposition wangeweza kula na kulala tu kma wwe ila watu wakijitoa kupigania wanachoamini kitaleta maendeleo ya taifa watie moyo sio kuwakejeli maana kumbuka wameaminiwa na wananchi wao ssa wwe unamjua msigwa kuliko wana mwembetogwa??
 
At least far better than Tanzania rail ametishia mpka jeshi hadi kazuia watu wasiende kazini ila bado hajaitwa mchochezi wala kulala jela hivi Tanzania inawezekana hiyo??
Kama kutukana tukana hovyo kwa akili yako ndo maana ya kweli ya demokrasia basi nadhani hakuna haja ya kuendelea kudiscuss, nyinyi ndo walewale wanasiasa njaa kwenye ukweli hamtaki, kwenye uongo mnataka. Mnawachezea sana wapiga kura wenu kwa kutokuwa na uelewa. Mnadhani siasa zenu cheap zitajenga nchi. Mtangoja sana kuweza kuongoza nchi kwakweli
 
Hakuna cha serious reform, this same agreements that were agreed in the past, these white investors were not honouring them. They were stealing, lying wrong amounts of quantities in the makinikias, lying that they were incurring loss whilst the stock exchange in London and Canada showing viceversa.
Unakuja hapa unanituhumu ninawadanganya wakati wewe hujui kitu na unaficha uovu wa chama chako. Serious reforms za kazi gani wakati hawatii makubaliano ya past reforms.

Chama chenu ni cha watu wasio na msimamo, watu waongo, Zito mlimfukuza kwa sababu gani, Slaa aliwakimbia sababu gani, Lowasa aligombea kwa Bendera ya chama chenu, demokrasia ilifuatwa?

Lowasa mlimtuhumu aje miaka kadhaa iliyopita alafu juzi mkaja tufanya wananchi wajinga kwa kumsifia tena. Nyie sympathizers mnanishangaza vichwa vyenu sijui mnafikiria aje. Eti ndio mkabidhiwe nchi, si bora huyo dikteta.
 
Nani politician hapa mini natoa main yangu haimaanishi nina ubia na chadema or what.... pia demokrasia sio kutukana kma katukana niambue tusi likwapi? demokrasia ni kruhusu free flow of ideas ndani ya mipaka ya sheria ndio maana marekani kuna hadi wanamziki wamemtukana trump ila wameachwa sababu ndio mawazo yao ila kma unasema tunatukana je huyo dikteta anayeita watu vilaza sijui wapumbavu mbona hakamatwi??? kuna mtu aliita watanzania malofa na wapumbavu mbona hamuwakamati????

unasema upinzani watasubiri sana ssa kma unajua hilo mnaogopa nnii mikutano ya kisiasa mnaogopa nni kuleta tume huru??

unadai tunawadanganya watanzania hivi walioahidi maisha bora kwa kila mtanzania si ni hao ccm enhee mpaka leo mbona tunaishi chini ya dollar 1??? hao maccm ndio wakweli wakaahidi
 
Wanasiasa wangapi wa Kenya wamepigwa shaba na kuuwawa wewe sympathizer, umewahi waona TBC au media yeyote Tz wakilia lia kama hao vishoia hapo.
Embu kaa pembeni kamanda, unaniaibisha.
 
tafsiri yako ya [][]
 

Hapo ndio nachoka mimi, pamoja na Chadema kuwa na mwanasheria mnayeseama kabobea lakini Chadema hiyo hiyo ilishindwa kutatua tatizo la Lema. kuna mahakama ngapi ambazo Lema anheweza kupeleka shauri la rufaa yake na akasikiliza, kuanzia mahakama kuu ya Tanzania, mahakama ya rufaa ya Tanzania, mahakam ya kikanda EACJ iliyoko Arusha, mahakama ya Umoja wa Afrika ambayo pia inakitenge hapo hapo Arusha. Unataka kusema mahakama zote hizo ziko mifukoni mwa serikali ya CCM?

Mimi sipingi wao kuwa Nairobi, lakini napinga upinzani wanatumia janga la Lissu kama fursa. Mara michango kitu, mara video za shutuma, mara Tanzania sio salama, mara udikteta. Hivi kweli chadema imeshindwakupata $50.000 huku inalamba ruzuku $1.2million? Mtu ana bima ya bure inayolipiwa na bunge, ingeweza kumpatia matibabu ya aina yoyote lakini wenzetu kidogo imekuwa fursa. Hata hiyo mnayoisema serikali ya Tanzania ni mbaya, mbona serikali ndio ililkuwa ya kwanza kutoa offer ya kumuhudumia Lissu lakini wakubwa Chadema wakapiga chini? Mtu hada damu hazijakauka hawooo ....wamemkibiza Nairobi kama sio fursa ni nini. Matibabu anayoyapata Lissu Nairobi naweza kukuhakikishia angeweza kuyapata hapahapa Dar. Mpaka leo hii, hakuna ushirikano toka kwa watu walio kuwa karibu na Lissu siku ya tukio kutu ambacho kinakwamisha juhudi za kujuwa ukweli uko wapi.
 

Hivi ni kweli mtu unaweza kulinganisha na ubeberu, ubaguzi na ukatili uliokuwa unafanya na serikali ya kikaburu na utawala wowote uliowai kutokea Tanzania? Yani, utawala wa kikaburu uliokuwa unapingwa na 90% ya mataifa ya duniani ndio utasema kina Lema na wenzake wanapambana nano? Kama kweli Tanzania ina ongozwa na udiketa, mbona hakuna hata serikali moja au taifa lolote lililo toa tamko au kutoa reference yoyote kama hivi sasa Tanzania ni nchi ya kidiketa. Wapinzani mnatuumiza vichwa jamani Khaa, kila mahali ni fursa, hata majanga yaliyo mkuta Lissu na hiyo mnaigeuza kuwa fursa.

Hata huyo John Kerry unaemsema aliuponda utawala wa Bush akiwa nje ya nchi, haujasema jinsi vyombo vya habari vya Marekani walimchukuliaje aliporejea nyumbani. Kitendo cha yeye kumpinga Rais aliye madarakani kama amechukuwa uamuzi wa ovyo kuanzisha vita ya Iraq, kiliwakwaza waumini wa dini ya kikristo wa Marekani ya kati pamoja na Wayaudi wa Marekani ambao mara nyingi ndio wenye uwezo mkubwa wa kukupaisha au kukuangusha kisiasa kitu ambacho kilitokea kwa Kerry.
 

CHADEMA huwa nawaangalia kwa kitu kidogo tu, wanaposema wanataka kuleta mabadiliko ni vyema wakaonyesha mfano bora, kipindi cha miaka zaidi ya kumi kikiwa na wabunge wengi wa kutosha na kuwa na ruzuku kubwa hata kuonyesha mfano wa kuwa na Ofisi yenye hadhi makao makuu hakuna, hata ofisi katika mikoa hakuna, kazi kukimbiza na kugawana ruzuku na kuwapa watu masikini bendera, kila ukipita ni bendera. Nasikitika watu bado wanawaza bendera kama kitu cha maana sana - Wanasema visibility sawa lakini iendane na wakati (Tuna bendera ya Taifa inatosha) Hata Marekani huwa wanatumia bendera ya Taifa lao katika Campaigns. Bendera ya nchi haibadiliki hata chama kingine kikishinda. Kwao inamaanisha utaifa ndio jambo la msingi kwanza.
Demokrasia ya kukubali kubadilisha viongozi ndani ya chama hakuna, cha kushangaza zaidi ni pale mlipomchukua Mh sana Lowassa from no where bila kufuhata taratibu za kichama na kumsimamisha kuwa mgombea wa Urais, ndipo nilipofahamu kuwa kuna vyama vya siasa na kuna vyama vya wafanya biashara. Sijawahi kuona theory na practices mbovu katika historia ya uongozi kama hiyo. Bila hata ya kupita kwenye mchujo ndio namna viongozi wanavyopatikana kwenye vyama kweli ? Tena ni mtu mliyekuwa mnamtuhumu kila kukicha. Na hii yote inafanyika ili kuweza kuchukua uongozi wa nchi.... Uongozi huwa unatafutwa kwa kufuhata utaratibu sasa kama nyinyi ndo mnakuwa wavunjaji wa utaratibu in the first place, Mlikuwa mnataka kuipeleka nchi hii wapi?
 
tafsiri yako ya [][]
mkuu unanskitisha sana sasa nani kakwambja msigwa au Lema hawajawahi fanya mikutano majimboni na kuhamasisha maendeleo ila sababu wapo kenya na kipindi ni cha siasa za ukanda huu basi wakaona ndio fursa ya kuwahoji

2. kuinua elimu sio kupanda majukwani kudai elimu bora ila nakujibu wwe unayetaka kupotosha wakenya kwamba cost ndio changamoto ya elimu tanzania wakati shida zipo nyingi tu ila kwakuwa unajitoa ufaham ili mradi tu umsifie huyo dikteta wenu

3. muuaji wa lisu atakapojulikana??? kwahyo nape bashe na zitto nao waliodai wanafuatiliwa na gari hilo hilo hamkuchukua hatua yoyote alafu mnajidai mtampata wakati ameshatekeleza mpango?? kma hamhusiki mbona mlikataa bunge kuunda chombo kuchunguza masuala ya utekaji ambao wabunge walidai wapo tayari kuleta ushahidi???

mkuu acheni kushabikia udhalimu li yanampata lisu alafu wwe unaona hamna shida kisa hayasaidii maisha yako unasahau hao wanahusika kwenye kutunga sheria ambazo zinaweza affect maisha yako mfano wapinzani walipinga muswada wa gesi ila maccm yakapitisha huoni lei hii umegundulika ulikua umeenda kumnufaisha mzungu tu sio mwananchi wa tanzania ssa bila upinzani kupiga kelele nani angeuzuia wakati ccm ndio wengi bungeni???

Mi naendelea kuamini kuwa dikteta atakuja kuwageuka nape alikuwa anamtetea kulilo wwe leo kakaa benchi hku ametishiwa kuuawa na karipoti polisi siku wakianza pigwa risasi mawaziri ndio mtatia akili vzurii
 
embu acha upotoshaji kerry hakufa kisiasa zaidi alisifiwa kwa ushujaa wake mwisho wa cku alizawadiwa cheo na serikali ya obama sasa wapi alikufa kisiasa

hata museveni alimpinga sana idd amin akiwa dar es salaam na leo hii ni Rais sembuse msigwa akiwa nairobi??

Mkuu udikteta sio mpka wazungu waseme mbona walisema kuhusu burundi nni kimebadilika??eti mbona hamna nchi iliosema?? hivi kuna mtu anamuita aung san su kyi muuaji kisa kashindwa kuzuia ethnic cleansing myanmar?? au kuna mzungu kamuita al assad dictator???

sio mpaka dunia ikuite dikteta ndio ukweli ujulikane hta rwanda wahutu na watutsi walichinjana kuanzia 1990 ila dunia mbona iliita genocide ilipofika 1994??? mkuu wakurd wanatewa ila kuna mtu yeyote duniani anatambua mateso yao yani mpaka dunia iseme wakurd wanateswa ndio inakua uhalisia ila wasiposema basi wakurd ni waongo???

Sio sawa kabisa kuukataa ukweli kisa majirani hawajasema ila udikteta unaanzaga ivo ivo magufuli alishatishia vyombo vya habari baadae kaanza kutishia kushughulikia mitandao later upinzani eti ataushughulikia nje ya bunge ssa huyo tumuiteje??? ana viashiria vya udikteta mkuu ukatae ukubali ila siku akianza kuwamaliza kina msukuma na bashe kwa SMG ndio mtatia adabu
 
hahahahaha hi nchi bhana salsa hutaki reforms mbona prof. usoro alisema the same kwamba tubadili sheria kwanza ili tuzibe mianya au wwe unajua kuliko usoro alieandaa ripoti???

reforms tukimaanisha huyo mnayesema ameiba anajengewa mazingira mfano unaambiwa hata mashine za kupimia ha tuna ila wanazo wawekezaji pekee?? sheria haiwalazimishi kuchenjua makinikia hapa sasa huoni mnajenga mazingira ya kuibiwa kisheria?? unaambiwa baada ya ukaguzi makontena hayafungwi tape kwanza mpka bureaucracy kibao zipitiwe huoni zinatoa mwanya wawekezaji kuchezea huo mchanga??? ssa sheria iliyonyook kuhusu ukaguzi upitiaji wa nyaraka ungetusaidia kuzuia wizi??? sababu yye akidau TRA TMAA huwa wanakagua makontena na kuyaidhinisha Sasa anawezaje kuiba wakati serkali huwa inakagua??

lisu aliraise maswali kadhaa kuhusu jinsi gani sheria ingeokoa wizi na nlifurahi kuona bunge inazipitia sheria upya ila wengine mkamuita msaliti alafu sijui kina mkapa chenge yona msabaha na karamagi tuwaiteje??
 
At first, I thought you would abandon your political ties and discuss the subject matter without taking sides!
Now I understand your political side. But to the centrally, I have no political affiliations!

How can I help then, I officially withdraw! All the best!
 
Wakenya sio wapumbavu kama wewe na misukule wenzio
 
Which language did they use to speak with KTN Broadcaster, i know Tanzanians most of them, they do scare to speak out English

even some Kenyans are falling on the same category, and the good example is yourself.you are not good at contracting english sentences in grammatical way.

"i know Tanzanians most of them, they do scare to speak out English".this sentence is totally wrong.

it would sound better if you would write/say:
"i know many Tanzanians scare to speak english".
 

Haha, zaidi ya kuwa senator wa jimbo analotoka Kerry (Massachusetts) ambapo wananchi wengi ni watu wa asili yake ya ki-Irish, ameshidwa kwenda na kukubalika nchi zima mpaka Obama akampa kifuta machozi kuwa waziri wa mambo ya nje.

Sasa kama sio lazima dunia kusema kama nchi fulani ni ya kidiktea, mbona kina Msigwa na wenzake wanaranda randa wakiamabia dunia wakate misaada yao kwa Tanzania kwasababu Tanzania ni nchi ya kidikteta (funny enough, hakuna hata nchi moja iliyoitikia huo mwito). Hata hiyo Burundi unayo isema hapa, ipo mpaka kwenye kumbukumbu za UN kama ni nchi iliyo na doa baya la kisiasa, Je umeshawahi kusikia Tanzania ikiwa na sifa kama hiyo? kwani unafikiri dunia hawana wawakilishi wao hapa Tanzania ambao wangekuwa wa kwanza kunyoosha kidole kwa Tanzania kama nchi inayo kwenda kusiko endeka?
 

Nikupe tu hongera kwa msimamo wako wa kutetea nafsi na maslahi ya watu, wanao kupa shibe ya matumaini ya kufikirika (rejea hoja zangu hapo awali nilivyokujibu).

Kwangu mimi, Tanzania kuna demokrasia ya kweli kabisa. Kinachoonekana kwa upinzani, na wewe kutetea, ni tafsiri ya utawala wa sheria kwako kuwa ni udikteta. Na tofauti kubwa kati yangu na wewe ni kwamba mimi nina mtazamo chanya wa maisha yangu. Siasa, kama dini, ni utajirisho wa kifikra kwa kundi moja dogo dhidi ya kundi kubwa katika jamii (fumbo mfumbie mjinga).
 
Let us agree to disagree or agree in principal, that time will tell!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…