Tanzanian MPs Msigwa na Lema KTN Kenya kuhusu Lissu n.k

Tanzanian MPs Msigwa na Lema KTN Kenya kuhusu Lissu n.k

msigwa " Uhuru is a kind of president who doesn't lose a sleep when someone criticise him or insult him" ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha
 
msigwa " he allows people to speak their minds" ha ha ha ha ha ha shule muhimu sana
 
msigwa " this thing should spread in the continent" ha ha ha ha ha ha ha
 
msigwa" we can not interfere to to the tume ya uchaguzi" ha ha ha ha ha ha ha kshindwa kutaja tume ya uchaguzi kwa kiingereza
 
msigwa " we have a lot learn from Kenya" dah sijui alikuwa anataka kusema nn ha ha ha ha ha
 
lema " but the the, actually the limit u have I can see is tribal situation" ha ha ha ha ha ha ha ha
 
..ktk shauri la Godbless Lema CDM walifuata taratibu zote hizo ulizozieleza,lakini mahakama zilikuwa hazitoi haki. By the time wamevuka vikwazo vyote na kufika mahakama ya rufani Godbless Lema alikuwa ameshakaa gerezani miezi 5. Jaji wa Mahakama ya Rufani aliyemtendea haki Mh.Lema aliwalaani mawakili wa serikali kwa kuichafua mahakama kwa mapingamizi waliyokuwa wakiweka ili Mh.Lema asipewe dhamana.

..Kinachokwamisha CDM kupata haki siyo kuwa na wanasheria wabovu, bali baadhi ya mahakimu kuwa compromised na kutumiwa na serikali kukandamiza wapinzani. At least mahakama kuu na mahakama ya rufaa wapo Majaji wenye ujasiri wa kutenda haki, lakini by the time CDM wamekata rufani na kufika ngazi hizo za juu tayari wanachama wao wameshaumizwa, wamesumbuliwa, wamepotezewa muda, na wamepoteza fedha na rasilimali zao.

..Mpaka hivi tunavyozungumza TL ana kesi zaidi ya tano. Kesi ambazo naweza kusema zinatokana na mashinikizo ya kisiasa. Kesi hizo atakwenda kukabiliana nazo MUNGU akimponya. Vilevile wanachama wa CDM zaidi ya 300 wana kesi ktk maeneo mbalimbali ya Tz. TL alikuwa tegemeo lao kwasababu yeye ndiye mwanasheria mkuu wa chama.

..Suala la kwenda Nairobi inabidi ulielewe kwa mapana yake. Nadhani unapaswa kuzingatia hali ya wasiwasi juu ya usalama wa TL waliyokuwa nayo FAMILIA pamoja na uongozi wa CDM ikiwa mgonjwa angekuwa-refered kwenda Muhimbili. Kama wahusika walimpiga risasi mchana kweupe katika compound ambayo Naibu Spika na mawaziri wanaishi nini kingewazuia kumvamia huko Muhimbili? Hivi unafikiri hakuna uwezekano wa wauaji kuvaa kama madaktari na kumvamia tena TL wakiwa na bunduki za silencers and finish him off?

..Kwa hiyo suala la TL kupelekwa Nairobi lilitokana na security concerns more than anything else. Na pia unaposema serikali imetoa offer ya kumhudumia inabidi ujiulize offer hiyo ni ktk mazingira yapi?

..Kwa maoni yangu serikali[waziri wa afya, na katibu mkuu] na Spika Ndugai walikosea kulazimisha TL afuate taratibu wanazofuata wabunge wanapokuwa na matatizo ya kiafya. TL hakuwa na tatizo la kiafya bali alikuwa na DHARURA YA KIAFYA. Wahusika hao walitakiwa wafanye maamuzi ya haraka ya kuokoa maisha ya TL huku wakizingatia kuihakikishia familia yake usalama wa mpendwa wao.

..Zaidi mpaka sasa hivi sielewi kwanini serikali imekaa kimya kuanzia kutoa salamu za pole, na hata kuhakikisha kwamba TL anahamishiwa hospitali nyingine yenye specialized treatment kwa majeruhi wa silaha za kivita kama TL. Mimi naamini serikali inao uwezo wa kifedha, kinachokosekana ni nia ya kumsaidia TL. Kwanini serikali imeamua kuwasusia mgonjwa familia na CDM?

..Kama serikali ingetekeleza wajibu wake wa kumlinda TL tusingefika hapa tulipo. TL asingeshambuliwa na silaha za kivita mchana kweupe. Lakini zaidi, kama serikali ingeamua kumsadia matibabu TL basi hawa wana-CDM unaosema wanatumia tukio hili kama fursa wasingekuwa wanalaumu, au wasingepata "fursa."

NB:

..Kuna madai kwamba ndege iliyokuwa impeleke TL hospitali ya Muhimbili haikuwa ndege inayofaa na ingetumia muda mrefu kusafiri kuliko ndege iliyokodishwa na CDM kumpeleka TL Nairobi.


00381081:35a3ea3533c9e335b19d7cd499fedad1:arc614x376:w1200.png


Huyo hapo juu ni Mh.Peter Lijualikali mbunge wa CDM Kilombero. Hapo alikuwa anaburutwa kupelekwa gerezani kutumikia kifungo cha miezi 6. Chama kilimkatia rufaa na kuweza kushinda lakini alishatumikia miezi kadhaa gerezani na kazi ngumu. Wakili aliyesimamia rufani hiyo ni Tundu Antipas Mughwai Lissu.

cc MK254

Pamoja na maelezo haya uliyo yatoa, bado nashindwa kuelewa CDM wakisema mahakama za Tanzania ziko chini ya CCM huku wakipigana vizuri wanashinda kesi. CCM kama chama, kina mapungufu yake, inawezekana ni kweli kama CCM inatumia nguvu zake za kidola kubambika kesi zisizo na kichwa wala miguu ili kuzohofisha CDM au upinzani. Lakini nashindwa kuamini kama mahakama zote na majaji wote wako mfukoni mwa CCM, na ndio maana nikasema kama Lema au CDM wanaona hawajatendewa haki na mahakama ya aina yoyote kwanini hawaendi ngazi nyingine ikiwa mpaka mahakama ya Afrika Mashariki au mahakama ya haki za binadamu ya Afrika. Spika ameeleza utaratibu wa kupata matibabu ya wabunge, lakini CDM (maana ni umamuzi wa CDM na sio Lissu maana alikuwa hajitambui wakati huo) ndio walianza kuja na madai yasio eleweka bila kufanya uhakiki kama kazi hiyo ingeweza kufanyika hapa hapa Tanzania au la. Sipati picha siku CDM wakiwa madarakani wao watakuwa watakatifu na wasitumie njama za aina yoyote kuongeza nguvu ya ngome yao.

Usalama wa Lissu au raia yoyote wa Tanzania ni jambo muhumu, na Tanzania kama nchi ina wajibu wa kulinda raia wake na mali zao panapo wezekana. Lakini tukirudi kwa Lissu, hivi kwa mtu anayehofia usalama wake unafikiri Nairobi watu wabaya wakimtaka Lissu watashindwa kufika? Kama maisha yake hayako salama mbona watoto wake bado wapo huku wanaedelea na maisha yao? Infact familia za viongozi wote wa CDM wapo huku na wanaendelea na maisha yao ya kawaida bila bugudha. Mnapo anaza kuweka lable mbaya kwa vyombo ya serikali eg. mahakama ya CCM, polisi ya CCM, hospitali za CCM, TISS ya CCM, mnajijengea tabaka la kutoaminiaa na vyombo hivyo kiasi kwamba hata mtashindwa kufanyanao kazi. hivi ikitokea siku CDM ikashika dola, mtafukuza kazi wafanyakazi wote wa hizo idara muajiri wapya? maana hicho kitakuwa ni kichekesho cha mwaka.
 
Enyi wakenya, hawa wapinzani wa bongo ni hovyo sana na mashabiki yao yenye akaunti kumi kumi huku wanadhani wana effect on the ground.

Wanalilia demokrasia wakati chama Chao kinaongozwa na mwenyekiti dikteta wao since their genesis, Mr Mbowe.

Na kiingereza Chao broken, they are not even proud of their language, at least Magufuli yeye he doesnt pretend huwa anabonga swahili mwanzo mwisho.

Huyo mwanasheria wao alietwangwa risasi alikuwa anaitisha press anasema Magufuli anatumia wrong approach kudeal na hao miners and that their company would sue us, kumbe tayari serikali ilishaweka sleeper cells in those companies, they had extracted all essential information and leaked them to the government, sasa hakuna cha kesi waliyofungua hadi sasa hivi, wamebanwa kwenye mazungumzo wanaongeza tu idadi ya negotiators.

Sasa wanaleta maneno huko kwenu kuonesha ubaya wa Magufuli.
They will fail
Unashtaki?[emoji1] [emoji1] [emoji1]
 
Wanasiasa wangapi wa Kenya wamepigwa shaba na kuuwawa wewe sympathizer, umewahi waona TBC au media yeyote Tz wakilia lia kama hao vishoia hapo.
Embu kaa pembeni kamanda, unaniaibisha.
sababu hawajawahi kuleta mgonjwa sar cku akiletwa watatoka povu wakiwa huku huku dar ila kma mwanasiasa museveni mbona alikuja dar akatoka povu kuhusu I'd amin na mwisho wa cku akapewa support ya kumtoa yule dikteta

pia ababu namwamba alikuja kwenye kongamano la ACT tafuta video iko youtube alimkaanga sana uhuru na sera za kenya za kibepari ssa kipi kipya hapa???
 
At first, I thought you would abandon your political ties and discuss the subject matter without taking sides!
Now I understand your political side. But to the centrally, I have no political affiliations!

How can I help then, I officially withdraw! All the best!
U wanted me to be neutral while I'm ipposing ur motion??? where did i declare that am from chadema or CUF???? since when is opposing a motion of criticizing opposition one becomes supporter of the opposition??

mkuu there is no reason to look for justifications in order to run away from the truth Desmond Tutu once said that neutrality when the oppressed are suffering is siding with the oppressor

have a good day too
 
Nikupe tu hongera kwa msimamo wako wa kutetea nafsi na maslahi ya watu, wanao kupa shibe ya matumaini ya kufikirika (rejea hoja zangu hapo awali nilivyokujibu).

Kwangu mimi, Tanzania kuna demokrasia ya kweli kabisa. Kinachoonekana kwa upinzani, na wewe kutetea, ni tafsiri ya utawala wa sheria kwako kuwa ni udikteta. Na tofauti kubwa kati yangu na wewe ni kwamba mimi nina mtazamo chanya wa maisha yangu. Siasa, kama dini, ni utajirisho wa kifikra kwa kundi moja dogo dhidi ya kundi kubwa katika jamii (fumbo mfumbie mjinga).
hakuna udikteta ila sheria??? haya niambie sheria gani inakataza mikutano ya kisiasa eti mpka 2020 nipe hicho kifungu ntaacha kumuita dikteta rasmi leo
 
U wanted me to be neutral while I'm ipposing ur motion??? where did i declare that am from chadema or CUF???? since when is opposing a motion of criticizing opposition one becomes supporter of the opposition??

mkuu there is no reason to look for justifications in order to run away from the truth Desmond Tutu once said that neutrality when the oppressed are suffering is siding with the oppressor

have a good day too
Oh boy, reread my post and show me where i said you are are supporting chadema or cuf as you mentioned. at least do me tht favour!
 
Oh boy, reread my post and show me where i said you are are supporting chadema or cuf as you mentioned. at least do me tht favour!
If I may assume why are you imposing character assassination for example if I'm raisin a question why should u then mind about my political affiliations??? does it mean if im ccm or chadema then u can neva have answers for my kind??? imean thats impossible in every political motion one has to take sides irrespective ur supportin the political parties involved or not
 
hakuna udikteta ila sheria??? haya niambie sheria gani inakataza mikutano ya kisiasa eti mpka 2020 nipe hicho kifungu ntaacha kumuita dikteta rasmi leo
Ukikubaliana na mimi kwamba kila shughuli ya binadamu ina wakati wake, nitarejea kujibu maswali yako hasa hili la [/]haya niambie sheria gani inakataza mikutano ya kisiasa eti mpka 2020[/I]
 
Ukikubaliana na mimi kwamba kila shughuli ya binadamu ina wakati wake, nitarejea kujibu maswali yako hasa hili la [/]haya niambie sheria gani inakataza mikutano ya kisiasa eti mpka 2020[/I]
ina wakati eeh mbona mheshimiwa Rais anafanya mfano kigoma alimpigia kampeni ndalichako kwa ajili ya 2020 pia pole pole alikuepo kugawa kadi jukwaani kabisa ssa kwanni yye anafanya??

pia unasema kuna wakati wa kila kwahyo unataka kusema waliotunga sheria ya vyama vya siasa hawakujua hilo??ila awamu ya tano ndio imelifaham hilo je kwanni basi msiende bungeni muibadilishe sheria ili wapinzani wakose kujitetea maana zuio la mikutano litakuwepo kisheria
 
Nikupe tu hongera kwa msimamo wako wa kutetea nafsi na maslahi ya watu, wanao kupa shibe ya matumaini ya kufikirika (rejea hoja zangu hapo awali nilivyokujibu).

Kwangu mimi, Tanzania kuna demokrasia ya kweli kabisa. Kinachoonekana kwa upinzani, na wewe kutetea, ni tafsiri ya utawala wa sheria kwako kuwa ni udikteta. Na tofauti kubwa kati yangu na wewe ni kwamba mimi nina mtazamo chanya wa maisha yangu. Siasa, kama dini, ni utajirisho wa kifikra kwa kundi moja dogo dhidi ya kundi kubwa katika jamii (fumbo mfumbie mjinga).
Matumaini ya kufikirika kivp wakati wote tunaona bungeni wanavyojenga hoja za kutetea maslahi ya wananchi ila wwe niambie hao CCM wamefanikisha nini hata kimoja toka uhuru
 
Back
Top Bottom