TANZIA: Mchezaji wa zamani wa Simba, Christopher Alex Massawe afariki dunia

TANZIA: Mchezaji wa zamani wa Simba, Christopher Alex Massawe afariki dunia

MUNGU ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi amina.
 
Nikikumbuka kipaji chake kile na hilo kochi alilokalia nakosa raha kabisa,

Vijana mnaochipukia tafadhari tumieni vipaji vyenu kutengeneza maisha acheni kulewa sifa,Simba na Yanga sio baba zenu.

M.A.P
 
RIP Masawe, kwa mwenye picha ya Masawe enzi za uhai wake aiweke ili kuweka kumbukumbu sawa

massawe+clip.jpg
 
RIP massawe,TB inamaliza watu kwa kweli,tubadilike tabia
 
Ameugua bila msaada. Baada ya kufariki ndio tutaanza kuwaona viongozi wetu wakiwa kimbelembele kwenye mazishi na kumwaga sifa nyingi za kinafiki. ndio Tz yetu!
 
Tumeumbwa kwa mavumbi na tutarudi kuwa mavumbi....bwana ametoa na bwana ametwaa jina lake lihimidiwe
 
Tyta;

Umetekeleza ombi kwa haraka, ukamilifu na uaminifu. Ubarikiwe
 
Last edited by a moderator:
Jana tu watu wamemtaja taja humu.....RIP
Dah,
Mungu anisamehe tu aisee, maana ni kama nlikua namchulia.
Huyu jamaa pamoja na mafanikio aliyoyapata kipindi anacheza, lakini ni mojawapo ya wachezaji wachache waliodumu kwenye game kwa muda mfupi sana.

Alicheza kwa kipindi kisichozidi miaka mitatu kisha akaachana na mpira huku akiwa katika kiwango cha juu. Wengi wetu tulidhani ni mtoto wa Mfanyabiashara Tajiri Bw. Alex Massawe hivyo tukafikiri kaamua kusimamia biashara za Baba yake.

Hivi karibuni aliekua mchezaji mwenzake timu ya Simba Boniface Pawassa (Baba Mwenye Nyumba) alidhamiria kuandaa mechi ya hisani kuchangisha hela za kumtibia Christopher lakini kutokana na urasimu mechi Mpaka leo haijafanyika.

Anyway, R. I. P Christopher Alex Massawe
 
dah a great player of his time,rip brother Massawe......you will be remembered.
 
Sasa msiba utaenda kwa baba yake Kwa alex massawe moshi?
 
Watu wamekula GOOD TIME enzi zao na warembo wa kila aina bt kipind cha matatizo wanakimbilia kwa WAZAZI WAO kuwaongezea mzigo
 
Back
Top Bottom