Replica
JF-Expert Member
- Aug 28, 2017
- 1,681
- 8,887
TANZIA: Msanii maarufu wa maigizo Afrika Mashariki, Maureen Wana, ambaye pia alikuwa akijulikana kama Sabrina au Ketty katika tamthilia ya Kashfa iliyokuwa na Azam TV kupitia channel ya Azam TWO, amefariki dunia alfajiri ya leo.
Maureen amefariki katika hospitali ya Kilifi iliyoko mjini Mombasa kutokana na matatizo ya uzazi wakati akijifungua.
Msanii huyo atakumbukwa kutokana na umahiri wake katika uigizaji, uwezo wa kucheza nafasi mbili kwa wakati mmoja katika tamthilia moja.
Katika tamthilia ya Kashfa, Maureen alicheza ipasavyo nafasi ya Sabrina kama binti mshamba kutoka kijijini lakini pia aliweza kucheza vizuri kama Ketty, binti wa mjini na mrembo katika tamthilia hiyo hiyo.
Maureen ameacha mtoto mmoja wa kiume.
Azam TV tunaungana na familia ya Maureen, na wapenzi wote wa sanaa ya maigizo Afrika Mashariki kuomboleza msiba huu mkubwa.
Maureen amefariki katika hospitali ya Kilifi iliyoko mjini Mombasa kutokana na matatizo ya uzazi wakati akijifungua.
Msanii huyo atakumbukwa kutokana na umahiri wake katika uigizaji, uwezo wa kucheza nafasi mbili kwa wakati mmoja katika tamthilia moja.
Katika tamthilia ya Kashfa, Maureen alicheza ipasavyo nafasi ya Sabrina kama binti mshamba kutoka kijijini lakini pia aliweza kucheza vizuri kama Ketty, binti wa mjini na mrembo katika tamthilia hiyo hiyo.
Maureen ameacha mtoto mmoja wa kiume.
Azam TV tunaungana na familia ya Maureen, na wapenzi wote wa sanaa ya maigizo Afrika Mashariki kuomboleza msiba huu mkubwa.