Tanzia: Mwanzilishi na Bosi wa Tip Top Connection, Abdul Bonge afariki dunia

Nimepata taarifa kuwa kiongozi wa kundi la muziki la tip top amefariki mwenye taarifa rasmi ya kufariki kwa abdu bonge atujuze tafadhali
 
kwa mjibu wa east africa tv, msanii madee amethibitisha ktokea kwa kifo hcho usiku huu, nyumbani kwake abdu bonge ,R.I.P
 
RiP kama kweli maana humu ndani siku hizi kuna viwanda vya kutunga uongo
 
RIP Bonge, Manzese itakukumbuka milele...Kwa wasiomfaham vizuri bonge licha ya kubadili maisha ya vibaka kama Tundaman, Madee nk kuwa wasanii wakubwa wenye mafanikio.

Ata kitaa kabadili maisha ya vijana wengi walioshindikana mpaka na polisi kuwa watu wazuri.Kwa kuwapatia shughuli za kufanya na kuacha mambo ya kukaba na uporaji na kuifanya Manzese kuwa sehemu salama kabisaa,sasa hivi Manzese unaweza kupita ata na gold shingoni si polisi pekee wamefanya hii kazi.
 
Ameplay part yake kwa kweli bonge amewainua wasanii wengi sana japo kulikua na kasoro za unyonyaji but all may God rest his soul in eternal peace.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…