Taratibu jamii ya Watanzania inaanza kuinyanyapaa elimu ya mtaala wa NECTA. Unaweza kuamini msomi kama Carol Ndosi anaweza kuandika kitu kama hiki

Kubeza elimu ni ushamba na mlengo wa kisiasa ,kama mtu alikuwa kipanga basi ni kipawa chake wala hakuna uhusiano na maisha magumu...Kubeza elimu ni sawa na kuharibu vizazi vinavyokuja.

Elimu itabaki kuwa vile vile ishu .....Hapa kwa undani zaidi inachangiwa na kupoteza ile hali ya watu kujisifu maana kila kona kuna wasomi kwa sio kama zamani.


Hao wenzetu wakikutana na wazungu siku kadhaa basi wanaona Tanzania ni takataka na kejeli zao za kishamba ila wameanzia huku.

Tuache hayo ,vipanga wengi kama wote wana maisha safi kabisa msidanganywe kabisa ..
 
Kufanikiwa kuwa na Maisha Makubwa Kuna hitaji vitu vingi Sana ikiwemo
Ubahili
Self control
Investiment
Socialization
God fearing and hard working

Sasa hayo mambo unaweza kuwa hujasoma ila ukapata bahati ya kuyafahamu Mapema Sana kipindi Cha ukuaji wako na ukatoboa vizuri as the same unaweza ukawa Umesoma ukashindwa kuyafahamu hayo mambo na ukashindwa kutoboa.

So wasomi wengi hapa bongo huwa wanaishia Kupata stress na kuishi kiujanja ujanja hiyo yote ni ukosefu wa Maarifa Sahihi ya Maisha then sioni umuhimu wa kumpima Mtu kuwa namba moja katika mitihani na kuwa namba moja katika Maisha all doesn't work
 
Sahihi 100%
 
Yupo sahihi kabisa, Elimu ibadilishwe , ukikaa na watu wazima waliosoma miaka ya 80 kurudi nyuma utaona Elimu yao ilikuwa angalau bora kuliko ya sasa
Tujiulize kidogo..
Elimu ilikuwa bora au kizazi hicho kilikuwa bora zaidi ya kilichopo sasa?
Kuna mambo ya kufikirisha kidogo;
Miaka hiyo walikuwa wanaanza shule wakiwa na umri gani?
Je walitambua kwanini wanaenda shule?
Mategemeo yalikuwaje kwa anayeenda shule, anasoma kwaajili yake, familia, ukoo, kijiji au taifa?
Mara kadhaa watu wamefanya mambo makubwa kwasababu ya uhitaji na mategemeo ya wengine, kama maisha yamekuwa rahisi kiasi cha kushusha uhitaji 'labda' imeathiri ufanisi wa wanaoitafuta elimu
 
Kwa sehemu kuna ukweli. Elimu dunia inatu limit kufikiria, kujaribu au kufanya kitu ambacho hatujasomea. Ukitaka kuzungumzia politics itasema hujasomea hilo, ukitaka kuzungumzia kuhusu ubora wa barabara, utaambiwa huna ujuvi. Pamoja na mengi mazuri ya elimu dunia, ila inatudumaza ule ufikiriaji au uhuru wa kufanya kitu kulingana na elimu ya asili ambayo kila mtu anazaliwa nayo. Pia elimu hii imetutengenezea mitazamo kwamba tulichosoma ndio sahihi pekee, nje ya hapo ni uongo.
 
Sasa wewe unadhani nini kifanyike ili kuheshimisha elimu yetu mkuu?
 
Achana na kuchambua mambo ya uchawi na dhana za kusadikika jikite katika vitu vinavyoonekana wazi kama hivi tusome content za kueleweka na zenye maana.
Siachi
 
Achana na kuchambua mambo ya uchawi na dhana za kusadikika jikite katika vitu vinavyoonekana wazi kama hivi tusome content za kueleweka na zenye maana.
 
Mimi ckujaliwa kusoma elimu ya darasani ila kuna kitu nilijifunza mwanzo kabisa wa maisha yangu. Na nakiishi mpaka kesho na kimenilipa kwa kweli.
Iko hiv. Ukishaamua kufanya kitu fanya kwa nguvu zako zote akili yako yote na kwa maarifa yako yote. Lazima ufaulu. Na unafanya kwaajili yako sio kwaajili ya kushinda hapana. Unafanya ili kutimiza ndoto zako. Usimuangalie mtu wala usinung'unike kwanini wameniachia mwenyewe. Maadamu uko hilo eneo onyesha umuhim wako then jamii itakutafuta kila mahali na life itakuwa very easy kwako.
 
Dah nimesoma na vichwa ila now ni walevi mavi kuna wana nimesoma nao chuo leo wanaona mm nina afadhali. Napata tabu sana nikikutana nao hawako huru kabisa ninachojifunza kwenye maisha alichopanga Mungu juu yako hakihusiani na mafanikio yako ya darasani. Elimu yetu inatudhalilisha wenyewe kwa kutoendana na mifumo yetu ya ajira na shughuli mbali mbali
 
Maisha ni koneksheni, jua pia kuna maprofesa wako chini ya menejimenti ya watu wenye elimu za kawaida.
Nenda shule kwa ajili ya kupata ujuzi na si cheti tu.
 
Kwa mtazamo wangu tatizo sio elimu tatizo ni kazi. Kazi zinatakiwa ziwe nyingi kuliko watu kama kipindi cha Nyerere. Mtu anamaliza form four anaenda kugonga field. Akimaliza form six anagonga field tena. Mpaka mtu anafika chuo ana uzoefu na anajua anataka kufanya nini. Kuna kitu wazungu hawaonyeshi kwenye movie zao. Huku kazi vijana wanaanza mapema 16 and 17 years. Sasa mazingira yetu aliyefaulu ndio anaambiwa akae nyumbani likizo apumzike ajiandae na shule. Aliyefeli mdo anaongozana na mzee kwenye biashara.
 
Professor gani huyo?. Maana full proffesors Tanzania hawazidi 66, na wengi wapo vyuoni.
Angaza vizuri utawaona.
Kuhusu kuwa wachache, ni kwa sababu ya ubinafsi wa kutokuweka bajeti ya kutosha katika kuwaendeleza wengine
 
Word!!!
 
Watu wanatakiwa kulijua hili
 
Connections na Baba ni nani, msidanganye watoto wa maskini.
Kaka huwezi amini kabisa wote watoto wa katani tu o level ila walikomaa sana A level mmoja jkt Mungu jaalia alikutana na uhitaji wa watu waliofaulu PCM pakambeba na hakujua hata wapi anaenda mwingine ufaulu wake tu wa petroli uko university umemfikisha hapo.
Sometimes uki bukuka pana faida yake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…