Taratibu na sifa za Msindika nafaka

Taratibu na sifa za Msindika nafaka

Malila

JF-Expert Member
Joined
Dec 22, 2007
Posts
5,329
Reaction score
5,024
Hi all,

Nataka kuanza kusindika nafaka, hasa Mahindi, pia ninunue na kuhifadhi nafaka mbali mbali.Mpunga sitashughulika nao.
Nimetafiti na kupeleleza nikaambiwa hata ghara la kuhifadhia lazima lisajiriwe. TFDA nao wanaingia ndani, sijui TBS kama ni lazima kuwaona.

Sitajenga plant Dar,sababu jamaa wa REA wameleta habari njema ktk vijiji fulani huko Iringa ndani ndani. Ninachoomba kwa wadau wa jukwaa hili ni michango ya kuweza kulifanya zoezi hili liwe rahisi, si kwangu tu na wengine wanaotarajia kufanya biashara hii ya kusindika nafaka.

Maeneo ya kuchangia;

Ujenzi wa ghara, sifa na usajiri wake kwa mamlaka husika,
Usajiri wa jina la sembe itakayozalishwa,
Kibali toka TFDA/TBS,
Mashine za mradi ( kuna hizi za Ihemi Iringa- Sembe tofauti, inabidi tuzijue),
Madawa ya kuhifadhia nafaka na upatikanaji wake.

Karibuni.
 
Big up my brother ni wazo zuri sana. Ngoja wataalamu waje. Kuanzia kuna doc moja ya wizara ya kilimo inaelezea hii kitu. Halafu kuna kijarida mkulima mbunifu walielezea madawa yake. Ukiingia BID network kuna sample plans za hapa na kwingine Africa utapata idea. All the best
 
Big up my brother ni wazo zuri sana. Ngoja wataalamu waje. Kuanzia kuna doc moja ya wizara ya kilimo inaelezea hii kitu. Halafu kuna kijarida mkulima mbunifu walielezea madawa yake. Ukiingia BID network kuna sample plans za hapa na kwingine Africa utapata idea. All the best

Hizi doc muhimu ulizotaja naweza kuzipata nikienda Wizarani pale?
 
Nitakuwekea hapa au kwa email kesho

Asante dada,

Weka hapa na pia nitumie kwa e mail yangu. Ukiweka hapa utakuwa umeongeza ubora wa jukwaa letu. Mimi nazihitaji sana lakini kuna watu hawajauliza pia wanahitaji kama si leo ni kesho.
 
Hi all,

Nataka kuanza kusindika nafaka, hasa Mahindi, pia ninunue na kuhifadhi nafaka mbali mbali.Mpunga sitashughulika nao.
Nimetafiti na kupeleleza nikaambiwa hata ghara la kuhifadhia lazima lisajiriwe. TFDA nao wanaingia ndani, sijui TBS kama ni lazima kuwaona.

Sitajenga plant Dar,sababu jamaa wa REA wameleta habari njema ktk vijiji fulani huko Iringa ndani ndani. Ninachoomba kwa wadau wa jukwaa hili ni michango ya kuweza kulifanya zoezi hili liwe rahisi, si kwangu tu na wengine wanaotarajia kufanya biashara hii ya kusindika nafaka.

Maeneo ya kuchangia;

Ujenzi wa ghara, sifa na usajiri wake kwa mamlaka husika,
Usajiri wa jina la sembe itakayozalishwa,
Kibali toka TFDA/TBS,
Mashine za mradi ( kuna hizi za Ihemi Iringa- Sembe tofauti, inabidi tuzijue),
Madawa ya kuhifadhia nafaka na upatikanaji wake.

Karibuni.
Mkuu hapo kwenye mpunga kwanini umeachana nao au ni sababu binafsi tu, kama zipo zingine kutokana na uzoefu wako mwaga hapa zitusaidie na wengine tafadhari
 
Mkuu hapo kwenye mpunga kwanini umeachana nao au ni sababu binafsi tu, kama zipo zingine kutokana na uzoefu wako mwaga hapa zitusaidie na wengine tafadhari

Biashara ya mpunga ina sumbua sana,hasa kwa sisi tunaoanza.
 
Mkuu Malila!!

Kuhusu hizi mashine za jamaa wa "Ihemi Iringa" nimemuuliza Meneja wa SIDO moshi, kuwa kwa nini au inakuwaje SIDO wasiweze kutengeneza mashine kama hizo? Jibu alilonipatia ni kuwa kwa sasa hivi hawajaweza kuzitengeneza, ila naye alisha zisikia hizo za hao jamaa wa Iringa na aksema kuwa" Hizo mashine Complete Set, nikiwa na maana na Packaging machine) zinaagizwa nje ya nchi, probably INDIA, ila unaweza kuwasiliana naye pia, ni jamaa mwenzetu, yupo poa. Kwani mashine zao za kusaga na kukoboa zinasifika sana.

Tupo wote mkuu, ngoja tuwasubiri na wengine waje mn amawazo yao, nami pia nipo INTERESTED na hii idea.
 
mambo ya mashine na aina zake ziliishaongelewa sana hapa hasa za SIDO Moshi, BICCO na Ubungo. Hizi doc ni za kuhifadhi nafaka na madawa, kuna madawa asili ingawa kwa kusindika kibiashara sijui kama yatafaa mfano Utupa (Tephrosia vogelii) ni mmea wa jamii ya mikunde ambao huishi kwa muda unaozidi miaka mitatu. Mmea huu hutoa maua mengi, kuzaa mbegu nyingi na una majani mengi. Mmea huu hukua haraka pia ni rahisi kuzalisha. Huweza kukua hadi kufikia urefu wa futi 10. Inashauriwa kuukata baada ya miaka mitatu ili kurefusha maisha yake na kuwezesha kutoa majani mengi. Mmea huu hustawi vizuri sehemu mbalimbali na zipo aina kuu tatu. Aina hizo zinatofautishwa kwa maua yake kama ifuatavyo: inayotoa maua ya njano, pinki na meupe. Utupa unaoteshwa kwa mbegu na unakuwa tayari kutumika baada ya miezi 4-6 tangu mbegu zipandwe. Sehemu yenye sumu katika utupa ni majani na mizizi. Inadhuru visumbufu wa mimea vinapokula na kugusa, hii inavisababishia kukosa hamu ya kula. Utupa unaweza kutumika kama kiuatilifu cha wadudu kama vile kupe, utitiri, kimamba, cabbage headworm, viwavi, sota funza wa vitumba, bungua wa mahindi, vithiripi, fuko, viroboto, chawa na magonjwa ya ngozi. Pia utupa unafaa kutandaza shambani na kurutubisha ardhi.[h=3]Kutayarisha dawa ya unga wa utupa[/h] Twanga majani hadi yawe laini na uanike. Saga majani yaliyotwangwa na kuanikwa kuwa unga. Wakati wa kuotesha mazao, changanya unga wa dawa na mbegu ya zao unalotaka kupanda. Tumia shambani kwa kunyunyizia dawa kwa kushika kwenye vidole vitatu kwa shina moja la kabichi.[h=3]Matumizi ya ghalani[/h] Majani ya utupa yanatumika pia kuhifadhia mazao ghalani. Yanatumika kufukuza fukuzi na mende wa maharage. Chuma majani ya utupa, anika kwenye kivuli, twanga majani kupata unga. Pima na changanya gm 100 katika kg 100 za nafaka/mikunde. Dawa hii inatumika pia kuhifadhi mahindi.[h=3]Tahadhari kwa watumiaji[/h] Kuvaa kinga ya mwili mzima wakati wa unyunyuziaji Tumia dawa baada ya uchunguzi wa visumbufu Usile mazao kabla ya siku 10- 14 kwisha baada ya kunyunyuzia dawa Iwekwe mbali na watoto, maji na mifugo Utupa ni sumu kali kwa samaki, inaweza kuua wadudu marafiki na wanyama. Kwa nafaka za chakula hakikisha unga wa dawa unakaushwa vya kutosha kwani unaweza kusababisha harufu kali kwenye nafaka.
 

Attachments

mambo ya mashine na aina zake ziliishaongelewa sana hapa hasa za SIDO Moshi, BICCO na Ubungo. Hizi doc ni za kuhifadhi nafaka na madawa, kuna madawa asili ingawa kwa kusindika kibiashara sijui kama yatafaa mfano Utupa (Tephrosia vogelii) ni mmea wa jamii ya mikunde ambao huishi kwa muda unaozidi miaka mitatu. Mmea huu hutoa maua mengi, kuzaa mbegu nyingi na una majani mengi. Mmea huu hukua haraka pia ni rahisi kuzalisha. Huweza kukua hadi kufikia urefu wa futi 10. Inashauriwa kuukata baada ya miaka mitatu ili kurefusha maisha yake na kuwezesha kutoa majani mengi. Mmea huu hustawi vizuri sehemu mbalimbali na zipo aina kuu tatu. Aina hizo zinatofautishwa kwa maua yake kama ifuatavyo: inayotoa maua ya njano, pinki na meupe. Utupa unaoteshwa kwa mbegu na unakuwa tayari kutumika baada ya miezi 4-6 tangu mbegu zipandwe. Sehemu yenye sumu katika utupa ni majani na mizizi. Inadhuru visumbufu wa mimea vinapokula na kugusa, hii inavisababishia kukosa hamu ya kula. Utupa unaweza kutumika kama kiuatilifu cha wadudu kama vile kupe, utitiri, kimamba, cabbage headworm, viwavi, sota funza wa vitumba, bungua wa mahindi, vithiripi, fuko, viroboto, chawa na magonjwa ya ngozi. Pia utupa unafaa kutandaza shambani na kurutubisha ardhi.Kutayarisha dawa ya unga wa utupa

Twanga majani hadi yawe laini na uanike. Saga majani yaliyotwangwa na kuanikwa kuwa unga. Wakati wa kuotesha mazao, changanya unga wa dawa na mbegu ya zao unalotaka kupanda. Tumia shambani kwa kunyunyizia dawa kwa kushika kwenye vidole vitatu kwa shina moja la kabichi.Matumizi ya ghalani

Majani ya utupa yanatumika pia kuhifadhia mazao ghalani. Yanatumika kufukuza fukuzi na mende wa maharage. Chuma majani ya utupa, anika kwenye kivuli, twanga majani kupata unga. Pima na changanya gm 100 katika kg 100 za nafaka/mikunde. Dawa hii inatumika pia kuhifadhi mahindi.Tahadhari kwa watumiaji

Kuvaa kinga ya mwili mzima wakati wa unyunyuziaji Tumia dawa baada ya uchunguzi wa visumbufu Usile mazao kabla ya siku 10- 14 kwisha baada ya kunyunyuzia dawa Iwekwe mbali na watoto, maji na mifugo Utupa ni sumu kali kwa samaki, inaweza kuua wadudu marafiki na wanyama. Kwa nafaka za chakula hakikisha unga wa dawa unakaushwa vya kutosha kwani unaweza kusababisha harufu kali kwenye nafaka.

Dada ubarikiwe sana,
Nimeshanyonya na kuingiza ktk maktaba yangu. Siku moja njoo ukaone mwanzo wa mapumziko garden, site tayari. Niko nachakarika na master plan.
 
I see kumbe mapumziko garden tayari, hapo nakuaminia, nitakuja tu acha mambo ya Obama na Sabasaba yapite kuanzia mwezi ujao tutakutembelea.
Dada ubarikiwe sana,
Nimeshanyonya na kuingiza ktk maktaba yangu. Siku moja njoo ukaone mwanzo wa mapumziko garden, site tayari. Niko nachakarika na master plan.
 
I see kumbe mapumziko garden tayari, hapo nakuaminia, nitakuja tu acha mambo ya Obama na Sabasaba yapite kuanzia mwezi ujao tutakutembelea.

Nimepata site nzuri kando ya mto mdogo usio kauka barabarani kabisa na usafiri wa daladala upo, njoo uchangie mawazo.
 
Mkuu Malila hii Biashara ni nzuri sana kwa sababu Biana damu ni lazima ale, na ni kweli ina changamoto nyingi sana,

1. Kuhusu hawa TFDA na TBS hawa ni kweli ni lazima wakague kwa sababu, ndo kazi yao, na mpaka waje ku prove kuna mlolongo mwingi sana zikiwemo visit za ghafra kwenye site yako na kazalika.

2. Kuhusu Mashine, Mimi nazani hata China kuna Mashine nzuri Kabisa za Kusaga na Kupaki kabia, yaani ziko complete na mikanda yake mkila kitu, na ukienda kwenye Alibaba utakutana nazo za kutosha na kuna jamaa anga aliagiza moja China na ni nzuri sana au hata India nako ziko nzuri sana.

3. KUHUSU JINA LA BIASHARA
Hapo ndo unatakiwa kuwa makini sana, ni lazima uwe na Brand yako ambayo itawakilisha product yako, na ni lazima iwe tofauti na Brand zingine za wakina Azam na kazalika,
Na Katika hii biashara kwa sababu kuna wakongwe wako sokoni wakina Azam na wengine wengi sana ambao wana saga na kusindika so ni lazima wewe uje kivingine kabisa ili kuweza kukamata soko

NA VITU VYA KUJIULIZA NI

- Ni kwa nini watu/ wanunue Sembe yako na si ya Azam? Hapo mkuu Malila ni lazima uwe na Mjaibu ya kwa nini unazani wanaweza nunua unga wako?

-
Na mara nyingi hizi Unga zinafanana almost kila kitu so ni lazima wewe uone unaweza tofautisha vipi product yako nay a hao wengine

- Utawalenga wakina nani? Make ni lazima ujue kabisa unaenda Kuanza lakini utawalenda watu wa Kundi Fulani, unaweza ikawa na watu wa kati, Matahiri au masikini kabisa, so ni lazima ucheki na situation zenyewe za hapo,

-
Na ishu nyingine ya Muhimu sana ni kwenye Kupaki, Malila hapa ni lazima uwe Uje na Packeging yako ambayo ni ya kipekee kabisa,

- Na Ukiwasiliana na Jamaa wa China wanaweza kukutengenezea Mifuko unayo taka wewe mwenyewe,

-
Kwenye Kupaki some time ni lazima utumie Vifungashio ambavyo mara baada ya Mtu kutumia Huo Unga anaweza tumia huo mfuko kwa kazi zingine mfano


Kuendea sokoni

Kubebea mizigo
Kutumia hata kuzibia nyumba yake au hata chochote kile

- Cheki mfano zamani, Tulikuwa tunatu,ia mifuko ya Sement kujaradia madaftari, so ilikuwa inabidi tuitafute popte pale ilipo,


- Kuna Packeging zingine utakuta hiyo mifuko inatumika kubebea madaftari kabisa, au hata mtu kuweka Docomet zake, so ni lazima unapo kuwa unaandaa aina ya vifungashio jaribu kufanyia kazi hilo, make kwa maisha ya Bongo mtu anataka anunue kitu na baada ya kutumia kimsaidie kwa kazi zingine, Mfano ndooza mafuta zinatumika kubebea maji

- Kwa Sababu ya Ushindani wewe unaweza kuja na Jazo tofauti tofauti kabisa za kuweza ambazo wengine hawajawahi kupaki.

-Au unaweza paki kulingana na watu, Mfano watu walioko Gheto yaani Masela wakawa na packaging yao hata ya Nusu kilo na ikawa katika mfumo wa zilivyo Sabuni zile za Unga zile zilounganishwa kama Karanga au majani ya packit

- Na unaweza fikiria kupaki Hadi
Mugogo plus Mahindi, Muhogo plus Mtama
Dona pekee
Mtama pekee
Muhogo pekee
Hizi ni Unga ambao nazo zina watu wanaopenda sana, hasahasa walio kuwa wanaishi Bush na kwa sasa wako town na wanapenda sana kutumia msosi walio kuwa wanatumia wakiwa Bushi, na hata kiafya Unga kama wa Dona ni mzuri sana,

SO KIKUBWA NI WEWE UNAPO INGIA UHAKIKISHE UNAKUWA TOFAUTI KABISA KWA KILA KITU NA WENZAKO, USITAKE UFANANE NAO ITAKUWIA VIGUMU SANA KUPENYEZA KWENYE SOKO LA UNGA
 
Nimepata site nzuri kando ya mto mdogo usio kauka barabarani kabisa na usafiri wa daladala upo, njoo uchangie mawazo.
Asante utatupa location na maelezo wapi hasa ili tukufikie, pamoja sana mkuu.
 
Mkuu Malila hii Biashara ni nzuri sana kwa sababu Biana damu ni lazima ale, na ni kweli ina changamoto nyingi sana,

1. Kuhusu hawa TFDA na TBS hawa ni kweli ni lazima wakague kwa sababu, ndo kazi yao, na mpaka waje ku prove kuna mlolongo mwingi sana zikiwemo visit za ghafra kwenye site yako na kazalika.

2. Kuhusu Mashine, Mimi nazani hata China kuna Mashine nzuri Kabisa za Kusaga na Kupaki kabia, yaani ziko complete na mikanda yake mkila kitu, na ukienda kwenye Alibaba utakutana nazo za kutosha na kuna jamaa anga aliagiza moja China na ni nzuri sana au hata India nako ziko nzuri sana.

3. KUHUSU JINA LA BIASHARA
Hapo ndo unatakiwa kuwa makini sana, ni lazima uwe na Brand yako ambayo itawakilisha product yako, na ni lazima iwe tofauti na Brand zingine za wakina Azam na kazalika,
Na Katika hii biashara kwa sababu kuna wakongwe wako sokoni wakina Azam na wengine wengi sana ambao wana saga na kusindika so ni lazima wewe uje kivingine kabisa ili kuweza kukamata soko

NA VITU VYA KUJIULIZA NI

- Ni kwa nini watu/ wanunue Sembe yako na si ya Azam? Hapo mkuu Malila ni lazima uwe na Mjaibu ya kwa nini unazani wanaweza nunua unga wako?

-
Na mara nyingi hizi Unga zinafanana almost kila kitu so ni lazima wewe uone unaweza tofautisha vipi product yako nay a hao wengine

- Utawalenga wakina nani? Make ni lazima ujue kabisa unaenda Kuanza lakini utawalenda watu wa Kundi Fulani, unaweza ikawa na watu wa kati, Matahiri au masikini kabisa, so ni lazima ucheki na situation zenyewe za hapo,

-
Na ishu nyingine ya Muhimu sana ni kwenye Kupaki, Malila hapa ni lazima uwe Uje na Packeging yako ambayo ni ya kipekee kabisa,

- Na Ukiwasiliana na Jamaa wa China wanaweza kukutengenezea Mifuko unayo taka wewe mwenyewe,

-
Kwenye Kupaki some time ni lazima utumie Vifungashio ambavyo mara baada ya Mtu kutumia Huo Unga anaweza tumia huo mfuko kwa kazi zingine mfano


Kuendea sokoni

Kubebea mizigo
Kutumia hata kuzibia nyumba yake au hata chochote kile

- Cheki mfano zamani, Tulikuwa tunatu,ia mifuko ya Sement kujaradia madaftari, so ilikuwa inabidi tuitafute popte pale ilipo,


- Kuna Packeging zingine utakuta hiyo mifuko inatumika kubebea madaftari kabisa, au hata mtu kuweka Docomet zake, so ni lazima unapo kuwa unaandaa aina ya vifungashio jaribu kufanyia kazi hilo, make kwa maisha ya Bongo mtu anataka anunue kitu na baada ya kutumia kimsaidie kwa kazi zingine, Mfano ndooza mafuta zinatumika kubebea maji

- Kwa Sababu ya Ushindani wewe unaweza kuja na Jazo tofauti tofauti kabisa za kuweza ambazo wengine hawajawahi kupaki.

-Au unaweza paki kulingana na watu, Mfano watu walioko Gheto yaani Masela wakawa na packaging yao hata ya Nusu kilo na ikawa katika mfumo wa zilivyo Sabuni zile za Unga zile zilounganishwa kama Karanga au majani ya packit

- Na unaweza fikiria kupaki Hadi
Mugogo plus Mahindi, Muhogo plus Mtama
Dona pekee
Mtama pekee
Muhogo pekee
Hizi ni Unga ambao nazo zina watu wanaopenda sana, hasahasa walio kuwa wanaishi Bush na kwa sasa wako town na wanapenda sana kutumia msosi walio kuwa wanatumia wakiwa Bushi, na hata kiafya Unga kama wa Dona ni mzuri sana,

SO KIKUBWA NI WEWE UNAPO INGIA UHAKIKISHE UNAKUWA TOFAUTI KABISA KWA KILA KITU NA WENZAKO, USITAKE UFANANE NAO ITAKUWIA VIGUMU SANA KUPENYEZA KWENYE SOKO LA UNGA

Mkuu Chasha tunashukuru kwa Mchango wako nina swali moja naomba kuja hizi hawa Alibaba wanaaminika? unaweza agiza kitu tokea kwao na kikafika salama bila utapeli?
 
Mkuu nisha agiza na vinafika salama, ni kweli kuna kipindi kulikuwa na wa Nigeria wanevamia ila Serikali ya china na wamiliki wa Alibaba waliweza kupambana nao vilivyo, Nisha agiza mara tatu na mzigo unafika kabisa.
Ni wewe tu unaamua kwa njia gani, Meli, au Ndege
 
Back
Top Bottom