Taratibu za kufuata ili kupata TIN Number

ndio maana wabongo watu wa kati na wapiga dili hawaishi,lile tangazo la msukuma halikukutosha ?
ushauri mkubwa ni ufike jieleze uambiwe ufuate maelezo lakini ni bure.
kwa hili lililotangazwa kwenye media unasita je yasiyotangazwa si ndio mnalizwa na watoto wa mjini.
 
NDUGU YANGU USIDHANI ANAYEULIZA NI MJINGA SI LAZMA UJIBU UNAJUAJE KAMA MM NALIJUA TANGAZO LA HUYOO MSUKUMA ? NIMEULIZA ILI NIJUE NIPO KAZN MDA WOTE SASA KWENDA MAHALI HALAFU URUDISHWE AMA URUDI NYUMBANI KWASABABU UMEPUNGUKIWA NA KITU... NA MUDA WA KURANDARANDA KWENYE MAOFISI YA WATU SINA KWANZA KUNAKUPOTEZEANA MDA SANA NA NIMEKATA TAMAA KABISA WALIVYOSEMA HAZIFUNGULIWI JUMAMOSI NIMEUMIA SANA SANA NASIKITIKA
 
Wabongo bwana..kuingia play store na kudownload instagram au jf kila mtu anajua ila kupata TIN ya TRA hajui ataipata wapi wakati ashasema TIN ya TRA.
 
Unahitaji TIN kwa ajili ya nini? Mfano, biashara, leseni ya udereva, kutolea/kumiliki gari au pikipiki, au kulipia kodi ya majengo(property tax)? Nijibu hapo ili nikupe utaratibu.
mm na shida kwa ajili ya leseni ya udereva nisaidie
 
Mkuu unaposema huna muda kabisa unakosea. Wewe muda wa kufanya mambo yako unaupata jumamosi, je huyu mfanyakazi wa TRA ukitaka akuhudumie wewe mpaka jumamosi unadhani private zake yeye anazifanya lini? Mbona huyu mfanyakazi kuna huduma anazozihitaji ofisi nyingine na anajitahidi kuzipata pasipo kuathiri muda wa mwajiri wake? Panga muda wako vizuri, utapata japo nusu saa ya kufika TRA na kuhudumiwa and then urudi kufanya kazi zako. Dakika zinazotumika ku argue jf zinatosha kabisa kufika TRA ukachukua TIN yako.
 
April 08, 2016
DOMESTIC REVENUE DEPARTMENT‎


Re‎: ‎Application for TIN Registration‎
Dear Applicant‎;‎

The following are requirement for TIN Registration‎:‎
A‎) ‎Sole Proprietor or Individuals‎;‎
At least one of the following‎:‎
(‎i‎). ‎Birth registration certificate‎
(‎ii‎). ‎Voter registration identity‎
(‎iii‎). ‎Passport‎
(‎iv‎). ‎Affidavit from legal authority‎
(‎v‎). ‎Residential identification lellter from the Sub Ward ‎(‎Mtaa‎)‎
(‎vi‎). ‎School or university report‎
In addition two recent passport size photographs‎.‎
B‎) ‎Non Individuals‎;‎
(‎i‎). ‎For companies‎, ‎Memorandum and Articles of Association and certificate of ‎
Incorporation‎
(‎ii‎). ‎For foreign companies‎, ‎Memorandum and Articles of Association and certificate of ‎
Compliance‎
(‎iii‎). ‎For Cooperative Societies‎, ‎certificate of registration‎
(‎iv‎). ‎For Clubs and Associations‎, ‎certificate of registration‎
(‎vi‎). ‎For Partnerships‎, ‎Certificate of Registration and extract from registrar‎
(‎vii‎). ‎For Trust‎, ‎certificate of registration‎/‎incorporation as a trust‎, ‎Trust deed‎
(‎viii‎). ‎For Public Corporations‎, ‎an Establishment Act‎.‎
Together We Build Our Nation‎
Commissioner for Domestic Revenue‎

NIPO KAZINI MKUU WANGU
 
Nani amekwambia mimi ni mhaya?ntawaita mods wakupe ban for "name calling".

Na nani amekuambia mimi nina ka elimu?na kujua TIN nayo unahitaji kaelimu ambako mleta mada yeye hana?
 
mm na shida kwa ajili ya leseni ya udereva nisaidie
Nenda TRA na copy ya kitambulisho chako. Utapewa fomu ujaze kisha upigwa picha na kuchukuliwa akama za vidole na sahihi ya kielekroniki. Baada ya hapo utapewa TIN yako.
 

ACHENI KUDANGANYA WATU!!!!! Si dhani kama ni lugha sahihi kutumia na hasa hasa tunapojiita GTs. Lkn naamini ungeji-homework-isha kidogo tu ungegundua TIN ni BURE. Tunalipa withoholding tax(10%) on rent sbb tumelipa kodi, vp kama ofisi/fremu ni yako mwenyewe, utalipa w/tax 10% based on what amount? Gharama uliyojengea ofisi? Mimi nilitakiwa kulipa hiyo w/tax nikawaambia silipi kodi ya pango sbb ni family premise na nilitakiwa kuthibitisha kwa kupeleka docs. Ishu ni kwamba huwez kupewa TIN wkt umekwepesha kodi yetu, w/tax lazima ilipwe kwa kila kodi ya pango utakayolipa.
Ila unaweza kutumia ujanja wa kuipunguza kwa muda lkn end of the day utatakiwa kuilipa tu.
Kama pango ni 200,000/= kwa mwez so it is 2,400,000/=kwa mwaka. therefore w/tax(10%) utakayolipa ni 240,000/=
Tafuta mkataba mwengine(utajua mwenyewe utakapo upata) utakao onyesha kodi ya pango ni 200,000/= lkn umelipa miezi miwili au mitatu yaani 600,000/= kwahiyo w/tax(10% ya 600,000) ni 60,000/=kwahiyo utakua umeipunguza kwa muda kutoka 240,000/= mpaka 60,000/= kwakweli inakera kulipa kodi kabla ujaanza biashara na kidogo ina leta saikolojiko satisfaksheni kuona badala ya kulipa 240,000 umelipa 60,000 na kuokoa 180,000/=ni nyingi sana kibiashara.
Kimsingi w/tax inabidi ilipwe na mwenye nyumba sbb yeye ndio mnufaikaji wa kodi ya nyumba lkn fanya hivyo TZ uone kama utapata hiyo nyumba au fremu yenyewe. Mpangaji ndio mwenye wajibu wa kuikata na kuiwakilisha TRA kisha receipt lazima apelekewe mwenye nyumba kama proof of payment of w/tax.
 
Nimeenda tra nimemkuta bint mmoja kanambia nitoe elfu ishirin kupata tin no
 
Nimeenda tra nimemkuta bint mmoja kanambia nitoe elfu ishirin kupata tin no
Huyo aliyekwambia umpe elfu ishirini yeye kama yeye amekosea sana. Lakini kama amrkwambia ulipie kodi hajakosea. Acha kulalamika nenda kwa boss wake hapo ofisini umuulize utaratibu wa kupata hiyo TIN na umweleze jinsi ulivyoambiwa na watumishi walioko chini yake. Atakusaidia jinsi ya kufanya.
 
thanx! Sikutembea na hela mda huo so nikahaid ntaenda kesho kwaiyo nikimwona boss wake hata sent sitatoa?
 
Mbona unapenda short cut ndugu?nenda tra ukapate tin then nenda manispaa kapate leseni.very simple.
Gharama za kupata leseni zikoje nataka kufanya biashara ya miamala ya simu (tigo pesa, m, pesa airtel money)??
 
Ndugu zangu mimi tin number ninayo nataka kufanya biashara ya miamala ya simu kama tigo pesa na m pesa Naomba kwa aliewahi kukata leseni ya biashara ya miamala ya simu anijuze ngarana ya leseni kwa biashara husika
 
Tin za sasa zinatolewa pale mahali ilipo biashara..na zinaonyesha location ya karibu naTra office..ukipata sehemu isiyo yako itakulazimu kuhamisha ,
 
Habari za muda na wakati huu,

Kuna jambo limenitatiza, naomba msaada kwa anayefahamu. Nataka kuapply for tin number nature of business ni online business na sioni haja ya kujaza location information since sitarajii kulipia kodi ya upangaji wa eneo la biashara kwani biashara nayotaka kuifanya is on my hand. Please naombeni consultation.

Je ni sahihi kujaza location while sitokuwa na physical office location?
 
Hapo kwenye bold, ni moja ya taarifa muhimu zinazotakiwa na mamlaka husika, ili upatiwe hiyo TIN number yako.

Nini cha kufanya:
- Tumia taarifa zilizotumika kwenye kadi yako ya mpiga kura.
- S.L.P ni muhimu - Tumia S.L.P za ofisi ya kata unapoishi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…