TARURA huu ni uhuni na usaliti kwa kata ya Kitunda, Mzinga na maeneo jirani

TARURA huu ni uhuni na usaliti kwa kata ya Kitunda, Mzinga na maeneo jirani

Mchokozi wa mambo

JF-Expert Member
Joined
Mar 27, 2014
Posts
201
Reaction score
159
Kwakweli inasikitisha kweli kwa kinachofanywa na TARURA katika barabara za Kata ya Kitunda, Mwanagati na maeneo jirani na kata hizo naweza kusema ni uhuni na kutukosea wananchi.

Wameweka bango kubwa la ukarabati wa barabara na kushangaza wamepitisha greda na kumwaga kifusi cha vumbi. Hata kama hatujui huu ni uhuni wa wazi na kutumia fedha zetu za maendeleo vibaya.

Hivi kweli Mbunge wa Ukonga, Madiwani, manispaa pamoja wenyeviti wa serikali za mtaa hamuoni hili linalofanyika?

barabara ya Kitunda- Mwanagati ni vumbi tupu ukipanda pikipiki au usafiri wowote ulio wazi unafikia eneo unaloenda ukiwa kama unafanya kazi mashineni.

Tunaomba wizara na wanaohusika na fedha za ukarabati wa barabara hizi waje wajiridhishe. Hali ni mbaya sana wanafunzi wa shule ya Sekondari Kitunda, Shule ya Msingi Kitunda na Jitihada wanaumia kwa vumbi linalotimuka.

Kitunda kumekuwa kama kichaka cha kupiga hela watendaji na viongozi mbalimbali. Kulikuwa na usafiri wa Magari Mwanagati Mnazi Mmoja na Machinga Complex lakini hivi sasa imebaki historia tu magari yote yanageuzia Kitunda pamoja na yanatakiwa kugeuzia Mwanagati huku trafiki wakiwepo eneo hilo, wanakula rushwa hatuelewi. Sisi wananchi wa Mwanagati kiukweli tunaumia sana kuona magari yetu yapo lakini yanaishia Kitunda.

Pia magari madogo ya Kitunda Banana waliambiwa hii root ife yabaki magari makubwa tu yanayoenda Mjini sasa hatuelewi kwanini mpaka sasa yapo na yanasababisha foleni kubwa ya magari eneo la Njiapanda Msikiti.

Wanaohusika na haya yote fuatilieni mjionee haya.

Asante
 
Yote kwa yote barabara inakera sana kutoka makaburini mpaka Kitunda ni mashimo matupu wameshindwa hata kupitisha tuu kijiko
 
Mwaka majuzi serikali ilipima barabara na kuweka alama mpaka kwenye nyumba na walisema barabara inajengwa mpaka Msongola, watu wa Kivule tulifurahia, lakini mpaka leo hamna kilichofanyika zaidi ya kujenga toka msikitini mpaka Mwembeni.
 
Yote kwa yote barabara inakera sana kutoka makaburini mpaka Kitunda ni mashimo matupu wameshindwa hata kupitisha tuu kijiko
Utadhani sisi wananchi wa Kitunda sio watanzania na wakati kodi tunalipa pia tozo za miamala tunakatwa pia. Kwanini na sisi tusifaidike?
 
Utadhani sisi wananchi wa Kitunda sio watanzania na wakati kodi tunalipa pia tozo za miamala tunakatwa pia. Kwanini na sisi tusifaidike?
Yaani inaboa sana,Kuna miji mingi tuu ilioanzishwa juzi juzi tuu lakini ina lami hadi vichochoroni lakini Kitunda mh!! Tabu tupu
 
Mwaka majuzi serikali ilipima barabara na kuweka alama mpaka kwenye nyumba na walisema barabara inajengwa mpaka Msongola, watu wa Kivule tulifuraia, lakini mpaka leo hamna kilichofanyika zaidi ya kujenga toka msikitini mpaka Mwembeni.
Shida tuna wabunge, madiwani na wenyeviti waliojiweka madarakani wenyewe. Inaumiza sana wote hawa wanajitanua kwa kuboresha maisha yao na familia zao. Mateso makubwa kwakweli
 
Yaani inaboa sana,Kuna miji mingi tuu ilioanzishwa juzi juzi tuu lakini ina lami hadi vichochoroni lakini Kitunda mh!! Tabu tupu
Kabisa fikiria Ulongoni na Kipunguni KM kuna lami na hakuna root ya gari katika maeneo hayo. Kitunda kuna root za kwenda Kariakoo, Kivukoni, Posta, Mnazi mmoja lakini barabara inasikitisha sana.
 
CCM CCM CCM CCM CCM CCM OVYOOOOOO..............HALAFU KULE SI NDIO KUNA NA HOSPITALI YA WLAYA ILALA?
 
Yaani inaboa sana,Kuna miji mingi tuu ilioanzishwa juzi juzi tuu lakini ina lami hadi vichochoroni lakini Kitunda mh!! Tabu tupu
Inabidi mbadiri majina. Muwe mnatunga majina vizuri. Kitunda, mwanagati, matembele.....
 
Back
Top Bottom