Tasnia ya Filamu Tanzania inakosa "Master mind" wa kuitazama Bongo muvi kibiashara

Tasnia ya Filamu Tanzania inakosa "Master mind" wa kuitazama Bongo muvi kibiashara

May Day

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2018
Posts
6,311
Reaction score
9,027
Kuna wakati utawasikia baadhi ya Wasanii wa Bongo fleva wakifikia hatua ya kuwashutumu wale waliojitokeza na kukaa katikati yao na soko.

Wanachosahau Wasanii wengi ni kuwa kuwa na kipaji ni jambo moja na biashara ni jambo lingine.

Ili kipaji kiwe biashara lazima kuwe na Mfanya biashara. Uwezo au kipaji chako cha kufinyanga Vyungu Kijijini hakukufanyi tu wewe kuwa Milionea, unaweza ukajitutumua kwa kubeba bidhaa zako na kuzipeleka sokoni lakini mara nyingi utaishia kupata hela ya kujikimu tu huku ukipoteza muda mwingi nje ya eneo lako la kazi.

kila shughuli inahitaji "master mind" mmoja au kadhaa mkakaa chini na kugawana kazi, na hivyo kazi yako ikabaki ni kufinyanga tu Vyungu na kupokea pesa.

Kadri yeye anavyonufaika sokoni ndivyo na Mfinyanzi utaneemeka, na huenda sasa akakuwezesha ukanunua vitendea kazi vya kisasa, ukaajiri nguvu kazi zaidi ili kuongeza uzalishaji n.k.

Kati ya changamoto kubwa zinazoikumba tasnia ya Filamu hapa nchini ni kumkosa au kuwakosa hawa Master mind wa kuigeuza tasnia kuwa biashara inayouzika.

Na kwa isivyo bahati hata Mamlaka zikizungumzia tasnia hii zinawaona Wasanii peke yake, na hili ni tatizo kubwa maana tasnia hii imezungukwa na kada mbalimbali na kiukweli Msanii yeye huajiriwa tu kwa "project" iliyopo mezani.

Mpaka pale tasnia itakapompata Mtu au Watu wenye muda na nia njema na jicho la kibiashara kwa tasnia, basi tusitegemee makubwa haswa kwa upande wa tasnia kuwa kibiashara.
 
Kanisa Katoriki yazindua filamu Mpya inayoitwa UTU

Humo ndani utamkuta Mkojani, Mzee Muogo Mchungu, Mzee Korongo (marehemu) na wengineo..

Pata nakala yako..
 
Bongo movie inahitaji watu dizain ya Sallam Sk, Ruge Mutahaba, Seven Mosha, Babu Tale na Ncha Kali.

Bongo movie kuna pesa nyingi kuliko soka na bongofleva combined.
 
Bongo movie inahitaji watu dizain ya Sallam Sk, Ruge Mutahaba, Seven Mosha, Babu Tale na Ncha Kali.

Bongo movie kuna pesa nyingi kuliko soka na bongofleva combined.
Kuna hela lakini lazima Vichwa vikae chini waweke mikakati, la sivyo tasni itaendelea kudema dema tu.

Mpaka leo Wasanii Wakubwa ni wale wale wa enzi za Kaole...hakika asnia imekwama.
 
Mtu anaweka pesa kwenye pesa. Hata kama ingekua ni wewe Kwa hawa wasanii wa bongo muvi , ungeweka pesa yako?.
 
SIYO WABUNIFU NA HAWANA JICHO LA TATU.......
Ila hii ni kazi ya Producers, Wafanya biashara.

Ni bahati mbaya tu hapa Bongo Wasanii wana viherehere vya kukaba kila kitu, wanasahau kuwa wao wanapaswa kubaki tu kwama Wasanii.

Wanahitajika Watayarishaji na Wazalishaji Wabunifu na wenye jicho la kibiashara kuipeleka tasnia kutoka hapo ilipo.
 
Ila hii ni kazi ya Producers, Wafanya biashara.

Ni bahati mbaya tu hapa Bongo Wasanii wana viherehere vya kukaba kila kitu, wanasahau kuwa wao wanapaswa kubaki tu kwama Wasanii.

Wanahitajika Watayarishaji na Wazalishaji Wabunifu na wenye jicho la kibiashara kuipeleka tasnia kutoka hapo ilipo.
Ni wasanii wachache wanapokuwa mbele ya kamera huonesha uhalisia wa mazungumzo,body language na viitikio vya hisia halisi
 
Kuna hela lakini lazima Vichwa vikae chini waweke mikakati, la sivyo tasni itaendelea kudema dema tu.

Mpaka leo Wasanii Wakubwa ni wale wale wa enzi za Kaole...hakika asnia imekwama.
Exactly, kikubwa ni mipango na investment.

Vibandaumiza ni platform tayari ipo ya kufikisha movie kwa walaji, waumize vichwa.
 
Nani aangalie utopolo WA hao Malaya uvccm wanajiita waigizaji
Kinachoangaliwa ni Sanaa, kama unavyoangalia sanaa nyingine.

Biashara ikiwepo pumba na mchele zitatengana automatically.
 
Hivi wanavyokusanyana kwenye kampeni za siasa wanapata faida Gani? Mana waoni kama chama Cha siasa
 
Tatizo vipaji butu. Miaka ya nyuma niliwahi kuona tangazo la huyu wa kuitwa Ray, kaandika, kama unajiona mrembo na unataka kuigiza fika kwenye ofisi zetu zilizopo Sinza.
Kwa mtazamo wangu tatizo linaanzia hapo. Wanaonekana hawapo serious. Badala ya kutafuta watu wenye uwezo wa kuigiza, wanatafuta mademu.
 
Tatizo vipaji butu. Miaka ya nyuma niliwahi kuona tangazo la huyu wa kuitwa Ray, kaandika, kama unajiona mrembo na unataka kuigiza fika kwenye ofisi zetu zilizopo Sinza.
Kwa mtazamo wangu tatizo linaanzia hapo. Wanaonekana hawapo serious. Badala ya kutafuta watu wenye uwezo wa kuigiza, wanatafuta mademu.

Ingekuwa kuigiza ni urembo tupu basi tusingewaona Lupita ny’ongo, viola davis etc
Industry inahitaji visionaries ngoja tunajiaandaa tutafika tu
 
Back
Top Bottom