Tasnia ya filamu Tanzania ni sekta ya 'kuganga njaa'

Tasnia ya filamu Tanzania ni sekta ya 'kuganga njaa'

Kitu kilichoniacha hoi Tanzania ni kuwa actor anamwambia director nini cha kufanya sio the other way around, last year nilimuona Michael Bay alivyokuwa anawatukana akina Tyrese, LeBeouf, Duhammel mpaka nikachoka mwenyewe.

Storyline inatakiwa ireflect maisha halisi ya watanzania lakini wahandishi wa script zetu wao sijui wanataka kutuambia nini maana chache nilizoziona zilikuwa unrealistic.

Set Design iki ni kitu kingine ambacho wengi wetu tunakidharau ila set design.

Budget: Tutabishana till kingdom come ila ukweli utabaki kuwa budget ni important part ya movie yoyote, kama budget yako ndogo basi utapata kile unacholipia. Siwezi kucomment kwenye ili kwa sababu sijui financing ya movie za Tanzania inapatikana vipi.

Will be back,

3D ukipata muda pitia site ya Digital Domain ama Zoic Studios.

**By the way kwa watanzania walio na interests na visual effects Zoic Studios wanatoa unpaid internship kila baada ya miezi minne.
 
@Asha D;

Ni kweli kuwa mtu anayehitaji kufanya Visual Effects ni lazima asome sana. Ukweli ni kuwa Visual Fx ni combination ya science na art/artistry. Nikijisema mimi, honestly nasoma sana, tena sana, nabrowse sana, tena sana, nafuatilia habari nyingi politics, science, art, history etc. Fahamu jambo moja, nasoma sana. Kuna moment naogopa ntakuwa chizi. Nasoma sana kwa sababu kwa mazingira yetu tunalazimika kufahamu mambo mengi kwa kuwa hatuna wataalamu wa kutosha.
AVATAR na JAMES CAMERON
Niseme nini? Cameron is said to be partly artist partly inventor. Katika Avatar ali-device miniature camera ambazo zilikuwa zinarekodi facial expressions (emotions) ili animators waweze kurudia the same/similar emotions kwenye models zao. Teknolojia ya Motion Capture imesaidia kufanya seamless/smooth animations za characters katika filamu ya AVATAR. Filamu hii imefanyiwa effects na Studio mbalimbali duniani zikiongozwa na Weta Digital ya New Zealand. Niseme tu kuwa storage capacity wakati wa development ya Avatar ilikuwa takribani 1 petabyte (1 million gigabytes), imagine! James Cameron ni mtuu mwingine kabisa. Hata hivyo Steven Spielberg alitikisa dunia na filamu ya Jurassic Park kwa upande wa effects za filamu.
Teknolojia ya 3D stereoscopy ni kitu kingine wenzetu wanachotuacha. Visual experience yake ni beyond imagination kwa wale ambao hawajawahi kuiona. Mtaani watu wanweza kukimbia kama filamu ni ya kutisha. Mlimani City wamekuwa wakionesha 3D stereoscopy ya filamu ya Thor. Hata Fast Five na Pirates of the Caribbean: On Stranger Tides zimekuwa zikioneshwa this week (Japo hizi hazikuwa 3D stereoscopic).


I believe on the above it is common knowledge between us two kua we are
in agreement.. Na hizo movies in highlighted they are killing me kua bado sijapata
wala kuangalia plus Hangover 2... enways nakazana kua patient...


POROJO:
Wakati niko O'level mwalimu mmoja wa Kiswahili alikuja na mgeni darasani. Akatuuliza tunasoma kitabu gani cha Kiswahili katika literature, tukataja "Ngoswe, Penzi kitovu cha uzembe." Akatuambia, "Mwandishi wake ndiye huyu mbele yenu"! Alikuwa ni Edwin Semzaba!!! Nafahamu aliwahi kuandika hadithi gazetini "Tausi wa Alfajiri" sikumbuki gazeti maana nadhani ni zaidi ya miaka 10 iliyopita.




Badala ya kukuambia hongera you know Dr Semzamba... (a very good charming person who loves life...)
my mind was all tuned in trying to calculate the age (sorry... curiosity i guess...lol) not that you have to tell

HAKIMILIKI
Ni kweli kuwa niliowataja wengi wameffariki. Hata hivyo kuna publishers ambao ndiyo husimamia hakimiliki ya kazi zao. Shaaban Robert alifariki zamani lakini vitabu vyake kama kusadikika nadhani vinatumika mashuleni hadi leo (kama sijakosea) hii inamaanisha vinachapishwa. Nilinunua Adili na Nduguze toka kwa publishers ambao ndiyo wana copyright. Hatujakubaliana kuwa tutengeneze sinema ila nilimweleza afisa mmojawapo juu ya dhamira yangu, alionekana kushangaa as if ni jambo la kutoka ahera. Aliniambia nikiwa tayari niende ofisini kwao kwa mazungumzo. NIlikinunua ili nirudie kusoma stori yake na kuangalia challenges zitakazokuwepo. Stori ni nzuri. Visual Effects zikifanyika vizuri huenda ikawa exceptional film. Ina composition nzuri kwa maana ya stori pamoja na chance ya kufanyika visual effects. Shaaban Robert nadhani alikuwa-inspired na hadithi za Kiarabu ama Kiajemi.

Tunachokosea sisi ni kutengeneza sinema na kujaza effects bila sababu ya msingi as long as tunaweza kufanya. Ngoja tuone tutafika wapi. Kuhusu post uliyoweka ya Filamu ya Manzese, Dr Mhella naona mwanzoni alipata pressure kwa kuhisi watu wana nia ya kumkatisha tamaa, kumbe sivyo. Kuna vijana wazanzibari (Kwa uongozi wa Mazd, member wa JF) wameandaa filamu "The Crazy." ambayo wanasema wameweka visual effects, For trailer cheki link The Crazy_TRAILER_2011 (1).mpg - 4shared.com - online file sharing and storage - download. Bado wanarudia makosa yanayoweza kuepukwa kama Kiingereza na uhalisia hata wa mazungumzo tu. Kazi bado ipo. Nitawatumia waandaaji review yangu nikiishaiona filamu yote.




This above paragraph very useful infor... appreciated 3D...
Thank you for the link... i was trying kuifungua imenigomea but will try tena.
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
Tunahitaji fikra pevu kama hizi kutuletea thread zenye kutuelimisha.
Thanks M'bongo na wanaJF mliochangia kwenye thread hii.
Mimi bado mgeni nahitaji kujifunza mengi kutoka kwenu


Waweza kua mgeni katika jukwaa lakini sio katika mawazo,
fuatilia kwa ukaribu na utakuta waweza changia...
Karibu saana JF...
 
Badala ya kukuambia hongera you know Dr Semzamba... (a very good charming person who loves life...)
my mind was all tuned in trying to calculate the age (sorry... curiosity i guess...lol) not that you have to tell

Whose age? Semzaba's or mine?
Semzaba is 60, I am 32.
 
Waweza kua mgeni katika jukwaa lakini sio katika mawazo,
fuatilia kwa ukaribu na utakuta waweza changia...
Karibu saana JF...


Asante sana Asha D kwa kuniencourage. Nimejifunza jambo muhimu msana kupitia kwako
 
Asha D, sasa nimerudi rasmi kuchangia.

Kutokana na upeo wangu mdogo nadhani tuna matatizo kwenye tasnia yetu ambayo
yanaathiri sekta ya filamuna hadi sasa hakuna juhudi zozote zinazochukuliwa kuyatatua.
Matatizo hayo ni kutokuwepo malengo, mipango mibovu na uchoyo usiokuwa wa lazima
kwa filmmakers wenyewe.

Pia ukosefu wa elimu na kutokuwepo utafiti kwa waandishi wa miongozo pia vinasababisha
kuwa na uzalishaji mbovu wa sinema nchini kwetu. Huu ukosefu wa elimu umesababishwa
na mfumo mbovu wa nchi yetu kutokuwepo chombo maalum cha kuhakikisha mafunzo ya
msingi (nitty-gritty) ya namna ya kutengeneza kazi kwa watayalishaji wa filamu katika kiwango
kinachokubalika yanatolewa, na kwa sababu ya ubinafsi filamu zetu zimekuwa ni kitu kisichozingatia
au kuhitaji taaluma yoyote.

Pamoja na upeo wangu mdogo lakini sidhani kama uharamia katika filamu (film piracy) linaweza
kuwa tatizo kubwa sana hapa nchini bali uwepo wa mikakati mibovu katika masoko ndiyo tatizo kubwa
linaloikabili sekta yetu.

Kumekuwepo vurugumechi katika soko la filamu nchini inayochangiwa na watu walioko sokoni kujaribu
tu kupata faida iliyo kubwa zaidi bila kuangalia upande wa pili unafaidikaje. Kwa maana hiyo, wanachochewa
zaidi na uchoyo na ubinafsi, na siyo kuwajali wengine.
 
Kitu kilichoniacha hoi Tanzania ni kuwa actor anamwambia director nini cha kufanya sio the other way around, last year nilimuona Michael Bay alivyokuwa anawatukana akina Tyrese, LeBeouf, Duhammel mpaka nikachoka mwenyewe.

Storyline inatakiwa ireflect maisha halisi ya watanzania lakini wahandishi wa script zetu wao sijui wanataka kutuambia nini maana chache nilizoziona zilikuwa unrealistic.

Set Design iki ni kitu kingine ambacho wengi wetu tunakidharau ila set design.

Budget: Tutabishana till kingdom come ila ukweli utabaki kuwa budget ni important part ya movie yoyote, kama budget yako ndogo basi utapata kile unacholipia. Siwezi kucomment kwenye ili kwa sababu sijui financing ya movie za Tanzania inapatikana vipi.

Will be back,

3D ukipata muda pitia site ya Digital Domain ama Zoic Studios.

**By the way kwa watanzania walio na interests na visual effects Zoic Studios wanatoa unpaid internship kila baada ya miezi minne.



EQLYPS..

Habari yako bana! Sisi Tanzania bado saana am telling you… I really hope other people ambao wako katika hio Industry wangekua wanapata ujumbe/ushauri wanaopewa… Akina Kanumba (I mention him for I believe he is considered the best&#8230😉 bado hawaja realize ni jinsi gani wanaweza stabilize Film industry by a very stratified strategic Hit on focus… kua for them to succeed inatakiwa wa change in the sense wafanye a little research watafute watu wakali katika all film related sector… Since X-PASTER amaeni encourage I am kind of pushihg my self into trying to watch more Bongo Moveis thou it is proving really hard.
I was so disappointed that hata tu subtitles wanachakachua… Come on! Tanzania has a lot of people fluent and good in that sector but they are busy kupeana kazi tokana na nerworking (not bad kama the person is capable..) I Presume maana kwanini umpe kazi mtu kama hawezi na wapo wanaoweza… au ndo mambo ya budget???

Kuhusu Movie industry budjet in Bongo… hahaha… you don't have to be in it to get how the Budget works… Once when I was at Campus.. walikuja actors ku act pale… dah it's not about the budget… ukitaka kujua hilo angalia wadada wanavyo vaa sometimes… instead of kuvaa tokana na nafasi anavaa ngua ya kuuza sura na her sexual appeal… Naona I have to slow down hapa…..
And set designing… film industry in Bongo from by observation wanaamini kua set designing kuna aina ya kuleta maana mbili tu.. yaani ya kuonesha you are well off and ile ya konesha ni maskini.. na hata wakikodi hizo sehemu hamna hata ile effort ya set designer (kama kweli wapo) kuweza shughulikia props… kuna a movie nishawahi angalia wakati niko safarini na bahati mbaya nimesahau – jamaa yuko ofisini kuna kabati la vyombo jipya (I bliv it was for sale..)

Am looking on that you will be back statement of your.. the post shows it is almost a week old, been absent for quiet some time and I believe it is time you are bound to come and finish what started…

Kuhusu that offer…. Wow…..
 
Whose age? Semzaba's or mine?
Semzaba is 60, I am 32.


3D.. You have made me regret my question….lol… or should I say curiosity and also kujisuta saana kuhusu the Private discussion we held… now I guess I know where it is coming from… If you don’t mind please say something on budget in the Film industry in Tanzania… or set designing…
 
  • Thanks
Reactions: 3D.
Asha D, sasa nimerudi rasmi kuchangia.

Kutokana na upeo wangu mdogo nadhani tuna matatizo kwenye tasnia yetu ambayo
yanaathiri sekta ya filamuna hadi sasa hakuna juhudi zozote zinazochukuliwa kuyatatua.
Matatizo hayo ni kutokuwepo malengo, mipango mibovu na uchoyo usiokuwa wa lazima
kwa filmmakers wenyewe.

Pia ukosefu wa elimu na kutokuwepo utafiti kwa waandishi wa miongozo pia vinasababisha
kuwa na uzalishaji mbovu wa sinema nchini kwetu. Huu ukosefu wa elimu umesababishwa
na mfumo mbovu wa nchi yetu kutokuwepo chombo maalum cha kuhakikisha mafunzo ya
msingi (nitty-gritty) ya namna ya kutengeneza kazi kwa watayalishaji wa filamu katika kiwango
kinachokubalika yanatolewa, na kwa sababu ya ubinafsi filamu zetu zimekuwa ni kitu kisichozingatia
au kuhitaji taaluma yoyote.

Pamoja na upeo wangu mdogo lakini sidhani kama uharamia katika filamu (film piracy) linaweza
kuwa tatizo kubwa sana hapa nchini bali uwepo wa mikakati mibovu katika masoko ndiyo tatizo kubwa
linaloikabili sekta yetu.

Kumekuwepo vurugumechi katika soko la filamu nchini inayochangiwa na watu walioko sokoni kujaribu
tu kupata faida iliyo kubwa zaidi bila kuangalia upande wa pili unafaidikaje. Kwa maana hiyo, wanachochewa
zaidi na uchoyo na ubinafsi, na siyo kuwajali wengine.


WISDOM SEEDS

Like your name from my observation it seems ulitupa akili na utafakari wako hapo.. nimependa mtazamo wako na the fact umeona kabisa kua tuko pamoja ni si kwa ajili ya ni mda/kiasi gani upo jamvini bali kwa sababu ya mawazo mbali mbali ambayo twaweza badilishana – tukajifunza/kongeza ama kurekebika ikitegemea ni kitu gani hasa..

Katika post yako nakubaliana na unalosema… lakini ni muhimu saana sisi kama Watanzania tutambue na tu face ukweli kua walo revolutionise movie industry mpaka imekua hapa ilipo ni hao hao amateurs (sio proffessinals wala si wasomi.. BIG UP to them).. Hivyo kufanya related activities ziendeshwe hivyo hivyo ki amateur – hio pia imewafanya wawe na a very strong defensive mechanism ya kutotaka kuwasikiliza ama kuwahusisha wasomi in areas such as graphics, directing, Setting na other important aspects of making a really good movie.

Hivyo unakuta baadhi ya matatizo wanapata ni kutokana na kutohusisha the right people in certain and special film related fields such as promotion, Advertisements, management and the like… Wisdom am sorry kua sikubaliani nawewe kuhusu mambo ya kua Piracy is not a problem… Aisee nitolee mfana wa music hapa… hawa watu (Bongo flavor for instance) the way music yao inapendwa na kusikilizwa na a lot of people kama woote wangekua wananunua hizo singles collections/albums; kweli wangekua mbali saana… nime observe, where ever I go walokua na collections za Bongo zooote ni kwa njia yaku burn… hamna kitu kinadororesha maendeleo ya msanii hapa bongo kama Piracy… Na katika hio hio paragraph uloelezea nakuunga mkono (uwepo wa mikakati mibovu&#8230😉
 
WISDOM SEEDS

Like your name from my observation it seems ulitupa akili na utafakari wako hapo.. nimependa mtazamo wako na the fact umeona kabisa kua tuko pamoja ni si kwa ajili ya ni mda/kiasi gani upo jamvini bali kwa sababu ya mawazo mbali mbali ambayo twaweza badilishana – tukajifunza/kongeza ama kurekebika ikitegemea ni kitu gani hasa..

Katika post yako nakubaliana na unalosema… lakini ni muhimu saana sisi kama Watanzania tutambue na tu face ukweli kua walo revolutionise movie industry mpaka imekua hapa ilipo ni hao hao amateurs (sio proffessinals wala si wasomi.. BIG UP to them).. Hivyo kufanya related activities ziendeshwe hivyo hivyo ki amateur – hio pia imewafanya wawe na a very strong defensive mechanism ya kutotaka kuwasikiliza ama kuwahusisha wasomi in areas such as graphics, directing, Setting na other important aspects of making a really good movie.

Hivyo unakuta baadhi ya matatizo wanapata ni kutokana na kutohusisha the right people in certain and special film related fields such as promotion, Advertisements, management and the like… Wisdom am sorry kua sikubaliani nawewe kuhusu mambo ya kua Piracy is not a problem… Aisee nitolee mfana wa music hapa… hawa watu (Bongo flavor for instance) the way music yao inapendwa na kusikilizwa na a lot of people kama woote wangekua wananunua hizo singles collections/albums; kweli wangekua mbali saana… nime observe, where ever I go walokua na collections za Bongo zooote ni kwa njia yaku burn… hamna kitu kinadororesha maendeleo ya msanii hapa bongo kama Piracy… Na katika hio hio paragraph uloelezea nakuunga mkono (uwepo wa mikakati mibovu&#8230😉

Ashadii, si kama napinga maelezo yako lakini elewa kuwa; niliposema kuwa uharamia si tatizo kubwa
nilimaananisha kuwa kama miundombinu ya soko la kazi za sanaa itasawazishwa na wasanii wakapata
haki stahiki kulingana na kazi zao, hata kama piracy itakuwepo hawatadhurika kama ilivyo sasa ambapo
hawauzi na piracy ipo.

Angali Hollywood, hawatishwi na piracy ya Wachina kwa kuwa wana uhakika wa kurudisha gharama zao
zote na kutengeneza faida maradufu.
isitoshe kwenye tafiti zilizofanywa (kama ile iliyokuwa presented na
Bishop J. Hiluka; The Perspective of Film and Television Industry in Tanzania) zinaonesha kuwa
Tanzania ni nchi yenye kiwango nafuu sana Afrika katika uharamia huu wa kazi za sanaa, huku nchi tano
zinazoongoza katika Afrika kwa kiwango kikubwa cha uharamia wa kazi za sanaa zikiwa ni Nigeria,
Cameroon, Togo, Kenya, na Benin, na nchi zenye unafuu sana katika uharamia huu ni Afrika Kusini
(kwa sababu imerekebisha sana sheria zake ikilinganishwa na nchi nyingine za Afrika), Namibia,
Ghana, Tanzania na Zimbabwe.


Ni muhimu pia ukayaelewa mazingira ambayo uharamia wa kazi za sanaa umejikita na sababu za
kuongezeka uharamia huu. ambapo kwa mujibu wa tafiti hizo ni pamoja na ukosefu wa ajira na mfumo
mbovu wa serikali katika kuwasaidia na kuwawezesha vijana ndiyo umepelekea wengi wao kuuza bidhaa
haramu kama njia ya kutengeneza fedha. Kuongezeka kwa uharamia huu kumechangiwa pia na viongozi
wala rushwa ambao mara nyingi wamekuwa wakishirikiana na maharamia, kitu kinachopelekea kutotungwa
sheria kali dhidi ya uharamia huo.


Mwisho, watu hawana elimu wala ufahamu kuhusu thamani na umuhimu wa kununua kazi halisi na hawajui
chochote kuhusu sheria dhidi ya uharamia katika nchi yao.
 
Ili soko la filamu lifikie kiwango kizuri, kuna vigezo muhimu viwili ambavyo vinaweza
kutuongoza katika dhana nzima ya mafanikio katika usambazaji filamu:
(1) Maudhui/Mahitaji ya Watazamaji (Content/Audience Connection) na
(2) Jukwaa la Uwasilishaji (Media Delivery Platforms)


Content/Audience Connection:
Kwa miaka kadhaa, sekta ya filamu Tanzania imeshuhudia utofauti mkubwa kati
ya maudhui katika hadithi zetu na kile watazamaji wanachokihitaji, na matokeo yake
yameendelea kuyumbisha mikakati ya soko na sera za usambazaji. Maudhui lazima
yahusishwe moja kwa moja na mahitaji ya watazamaji ili kuwe na nafasi ya mafanikio
kwenye soko.


Maudhui yanayofaa katika kizazi cha leo ni yale yanayokwenda sambamba na watazamaji
ndani ya akili zao na kuihusisha jamii moja kwa moja. Mafanikio yanayotokana na maudhui
yanategemea sana mmenyuko wa watazamaji, na kujenga maudhui yaliyo kwenye mstari
na mwelekeo wa watazamaji na matarajio yao imekuwa vigumu, na sasa inahitajika kwa
watayarishaji/ waandishi wa miongozo ya filamu kujihusisha moja kwa moja na mtazamo
wa watazamaji katika mazingira waliyomo. Kwa matokeo haya, utafiti ni suala la kupewa
umuhimu mkubwa kabla ya kuandaa kazi husika.

Kitu ambacho mtayarishaji/ mwandishi anapaswa kujua kuhusu watazamaji wake ni
muhimu sana kwa mafanikio katika biashara ya usambazaji. Kujenga maudhui bila uelewa
mkubwa na ufafanuzi kwa walengwa, ni kama kufunga safari ya kwenda mahali bila
kufikiria jinsi ya kufika huko. Kama maudhui yako hayakushikamana na aina ya maisha
au matarajio ya watazamaji wako, jua umewapoteza.

Kundi la kwanza la watazamaji wa filamu ni la akina mama wa nyumbani, wafanyakazi
wa ndani, na vijana wasio na ajira. Kundi la pili ni la watazamaji linalotokana na matokeo
ya moja kwa moja ya kituo cha Africa Magic kuonesha filamu kwenye familia za watu
wa tabaka la kati na la juu wenye uelewa mpana kwa maana ya kwenda shule.


Na bila shaka kuna kundi la tatu linalotokana na watazamaji Watanzania walio nje ya nchi
na Waafrika (hasa wanaojua au kukipenda Kiswahili) katika bara la Afrika na maeneo waliko.
Ni muhimu kuelewa kwamba kila moja ya makundi haya ya watazamaji yana muundo na
mawazo ambayo ni tofauti sana na kundi jingine.


Utafiti unaonesha watazamaji wa filamu za Kitanzania wamegawanyika kama ifuatavyo:
Asilimia 67 ya watazamaji wa filamu hizi wanaishi ndani ya Tanzania, asilimia 25 wanatoka
katika nchi nyingine za Afrika Mashariki, na asilimia 8 wanatoka sehemu zilizobaki za dunia,
hasa ambako Kiswahili kinafundishwa au kupewa umuhimu.


Pia ni asilimia 30 ya wakazi wanaoishi mijini ndiyo huangalia filamu za Kitanzania.
Takwimu hii inatofautishwa kulingana na umri: Asilimia 50 ya watazamaji hawa ni
wenye umri kati ya miaka 10-24, asilimia 30 ni wenye umri kati ya miaka 25-34,
asilimia 15 ni kati ya watu wenye umri wa miaka 35-49 na asilimia 5 tu ya watu
wenye umri zaidi ya miaka 50 ndiyo huangalia filamu hizi. Dar es Salaam ndiyo mji
unaoongoza kuwa na idadi kubwa ya watazamaji wa filamu ikichukua asilimia 31.
Hata hivyo, vijana wadogo ndiyo wenye mazoea ya kwenda kwenye mabanda ya video.


Katika utazamaji filamu hizi, kuna dhana ambayo huendana na mitazamo ya watazamaji
(matamanio, maadili, na mtazamo wa mtu binafsi kulingana na uzoefu wake katika
kuangalia kazi mbalimbali) na vitu hivi huathiri namna watazamaji wanavyohusiana na
dunia inayowazunguka, ikiwa ni pamoja na maudhui.


Media Delivery Platforms:
Maudhui ya jukwaa la uwasilishaji katika dunia ya kisasa ya filamu hayaishii tu
kwenye kazi ya usambazaji, yanakwenda ndani zaidi ya kile hasa soko la filamu lilivyo leo.
Jukwaa litakusaidia kuwasilisha mawazo yako kwa watu katika njia itakayojumuisha
mitazamo yao, na si kupambana nayo.


Ufanisi katika uwasilishaji unachangia utoaji haki ya kuchagua; kuyaleta maudhui kwa
watazamaji katika dunia yao wenyewe. Kulingana na uwezo mkubwa wa soko la Tanzania
kama litawezeshwa (ndani na nje ya bara la Afrika), jukwaa muafaka litamfanikisha kwa
urahisi mtengenezaji wa filamu kuendana na ushindani wa soko.

Mustakabali wa biashara ya usambazaji wa filamu na masoko Tanzania unatokana na
watazamaji vijana. Watoaji filamu wanatakiwa kuandaa kwa uangalifu takwimu (demography)
hii ya watazamaji na kukutana nao katika dunia yao. Dunia hiyo hustawi (flourishes) kwenye
kundi la kweli la teknolojia ya digitali.


Katika hatua hii itakuwa vizuri pia kuuchunguza mfumo wa usambazaji ili kupata ufumbuzi
wa kutangaza na kusambaza (promotion and distribution solutions) ambao umesaidia
kurekebisha tasnia katika nchi nyingine, na kuigwa katika sekta ya filamu Tanzania.
Filamu ni nembo (Film is a brand), kama zilivyo nembo/ bidhaa nyingine, kuzitangaza
na kuzisambaza ni vitu vyenye umuhimu sawa.


Mkakati ambao hatimaye utaweka tabaka la washindi na washindwa ni ubunifu katika kazi
na utafiti. Hii itaongeza mipaka katika utekelezaji wa kampeni ya kuzitangaza kazi.
 
Dah! Mkuu umetupa post hapa zoote zahitaji utulivu... napita...
Nitarudi by the way ....
 
Dah, ngoja nikajipange kwanza nitarudi
 
Kama tu wahusika wangekua wanafuatilia michango kama hii na kuifanyia kazi....


Well mi nataka sio nijaribu ila niwaonyeshe mfano kwa kuandaa movie moja ambayo nadhani itakua na kiwango cha kuweza kuitwa movie!!Partner nategemea kukupata kama mteja!
 
Kama tu wahusika wangekua wanafuatilia michango kama hii na kuifanyia kazi....


Well mi nataka sio nijaribu ila niwaonyeshe mfano kwa kuandaa movie moja ambayo nadhani itakua na
kiwango cha kuweza kuitwa movie!!Partner nategemea kukupata kama mteja!

Wow! Nasubiri kuona synopsis na script yako kabla hujaingia kwenye shooting. Tunahitaji watu
wenye kuthubutu kama wewe... Ukihitaji msaada wa kitaalam niambie nikutafutie mtaalam mzuri zaidi
katika mausla ya script
 
Nina swali hivi kabla script writers wa movie zetu bongo hawajaanza kuandika uwa wanafanya research?
 
Back
Top Bottom