Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 301,577
- 754,412
Wana mageuzi waliogeuzwa: Road Map to 2025. Walionja shubiri ya chamtema kuni. Unaweza pia kutumia neno "mchanja kuni." Kipigo na mateso vilionekana kama njia ya kujilinda, lakini pia vilikuwa ni visasi na onyo. Je, kuna kitengo maalum cha kuumiza, kutesa, na kupoteza watu ambacho kina kibali kutoka kwa mamlaka?
Picha inayojaribu kutengenezwa ni pana na ina vipaji vya kila aina vilivyojaa usherati, ugangwe, na ubaradhuli pia. Vipaji vya "hewala bwana" havijaachwa nyuma, vimo tena kwa wingi!
Visasi? Hilo liko wazi kabisa. Je, unajua ni kwanini mmoja alipokea kipondo kikali kuliko wengine, zaidi ya umbwa mwizi? Ni kwa sababu ya ushindi mnono wa kanda yake. Hapa mchungaji amefurahi sana.
Yote juu ya yote, ni nani huyu mwenye taswira nyuma ya kinyago? (A face behind the mask) Huyu ndiye injinia mkuu. Ni fundi mzuri sana wa kutengeneza mashimo ambayo watu watumbukie. Ana roho mbaya, kama ibilisi anasubiri. Huyu ni yule kiongozi mtukufu wa majabali. Hakuna jabali lisilomjua huyu mtwa!
Wanaotajwa kwa sasa ni wengi na lawama nyingi zinamwelekea mama na mwana. Hawa si wazoefu wa hizi figisu. Hata hao watumwa wengine, mchongo mzima unatengenezwa na mkubwa wa majabali; wao ni watekelezaji tu.
Huyu ni hatari zaidi kwa sasa na wakati ujao kwa sababu:
Good evening, Tanganyika..
Picha inayojaribu kutengenezwa ni pana na ina vipaji vya kila aina vilivyojaa usherati, ugangwe, na ubaradhuli pia. Vipaji vya "hewala bwana" havijaachwa nyuma, vimo tena kwa wingi!
Visasi? Hilo liko wazi kabisa. Je, unajua ni kwanini mmoja alipokea kipondo kikali kuliko wengine, zaidi ya umbwa mwizi? Ni kwa sababu ya ushindi mnono wa kanda yake. Hapa mchungaji amefurahi sana.
Yote juu ya yote, ni nani huyu mwenye taswira nyuma ya kinyago? (A face behind the mask) Huyu ndiye injinia mkuu. Ni fundi mzuri sana wa kutengeneza mashimo ambayo watu watumbukie. Ana roho mbaya, kama ibilisi anasubiri. Huyu ni yule kiongozi mtukufu wa majabali. Hakuna jabali lisilomjua huyu mtwa!
Wanaotajwa kwa sasa ni wengi na lawama nyingi zinamwelekea mama na mwana. Hawa si wazoefu wa hizi figisu. Hata hao watumwa wengine, mchongo mzima unatengenezwa na mkubwa wa majabali; wao ni watekelezaji tu.
Huyu ni hatari zaidi kwa sasa na wakati ujao kwa sababu:
- Bado ana ndoto kubwa.
- Kafanikiwa kuvaa kinyago.
- Kajisimika kwenye mgodi wa kaya.
- Anatekeleza mipango yake yote akiwa nyuma ya kinyago.
- Ni katili asiyejali wala kuogopa chochote.
- Kafanikiwa kwa asilimia 100 kumweka kiganjani bosi wake na anamuendesha atakavyo kutoka pande zote.
- Kajijengea mtandao imara sehemu zote kuanzia sungusungu mpaka mgambo.
- Kupitia mgodi wa kaya, kafanikiwa kujimegea na kujichotea vya kutosha, hivyo anatengeneza ushawishi na uungwaji mkono bila shida yoyote!
Good evening, Tanganyika..