Zanzibar 2020 Tathmini fupi mara Baada ya uteuzi wa Dkt Hussein Mwinyi huko NEC ya CCM

Zanzibar 2020 Tathmini fupi mara Baada ya uteuzi wa Dkt Hussein Mwinyi huko NEC ya CCM

Mimi iki kitu ndio huwa sielewi mgombea wa uraisi zanzibar anapitishwa na nec bara ..kwa nini nec zanzibar wasikae wakapitisha mtu wao huko ndio aje bara wasalimu
Huyo ni mgombea wa CCM, cuf na vyama vingine vinaweza vikampitisha mgombea wao kule kule zenji......
usiwaze...
 
Mimi nilijua Kuna Unguja na Pemba tu.

Kumbe kuna Unguja kusini,Unguja Kaskazini,Unguja Magharibi na Unguja kati.

Mmewabagua wapemba hadi mmeanza kujibagua wenyewe...

Kweli dhambi ya ubaguzi haijawahi kuacha wabaguzi salama.
Yaani kama wanavyobaguliwa wapinzani kule nchi kavu
 
Muungano wetu utakuwa Salama chini ya Dr Hussein Ally Mwinyi
 
Yamechujwa vipi? Walipigia kura wapi hayo majina matano? Kila mtu anajua hayo majina yamepatikana kwa SHINIKIZO kutoka bara. Zanzibar ndio inakufa hivyo, Wazanzibari chukueni hatua haraka.

Zanzibar ife mara 2?
 
Wafuatiliaji wetu walioko Zanzibar wametuletea tathmini hii fupi mara baada ya NEC ya CCM kumteua Dkt Hussein Mwinyi.

Kwanza baadhi ya wana CCM wamenuna wakilalamika kwamba wazanzibari hawana tena chaguo lao kwenye CCM, isipokuwa Upande wa Bara ndio unamuweka Mtu mwenye Maslahi yao.

Kuingizwa Dkt Khalid na Shamsi kwenye tatu bora kulilenga kuzigawa kura za Zanzibar hasa Unguja ambapo kura zimeelekea zaidi kwenye maeneo ya watu wanakotoka. Shamsi kaungwa mkono kwa kura 16 ikiaminiwa zaidi ni wajumbe wa NEC kutoka Kusini Unguja na Khalid kura 19 kutoka Kaskazini Unguja ambapo anatoka. Dkt Hussein kanufaika na kura za NEC bara na baadhi ya kura za mijini Magharibi ambazo zinanasibishwa na watu kutoka Tanzania Bara ambao ni wazanzibari wenye maslahi na Bara.

Kelele za kumkataa Mnyaa ambae inasemekana alikuwa chaguo la Watawala zilipindisha maamuzi mapenma ili kuepuka chuki ya wazi ambayo ingekigawa chama. Mwenyekiti na Timu yake walishtuka mapema. Taarifa zinabainisha ndio sababu ya kupelekwa Shamsi na Khalid ili kutuliza mpasuko wa kura za Unguja za mkoa wa Kaskazini na kusini.

Waliopanga mchezo walitegesha ilimradi maslahi ya Bara yamezingatiwa. Acha Mbarawa atote lakini Mwinyi apite na Bara ipete huo ndio msemo wa Mwisho ' Acha Mbarawa atote, Mwinyi apite na bara ipete"

KWA NINI MNYAA alilazimika kuachwa?
Nimeeleza kidogo. Huyu alihesabika mtu asiyewafaa wana CCM wahafidhina na wale maslahi. Ukweli ni kwamba Rais MAGUFULI anaogopwa na hata CCM wenzake. Zanzibar kuna utamaduni wa ulaji na kupendeleana sana . Ufisadi ndani ya serikali ni mkubwa na huwa wanalindana.

Prof Alihatarisha maslahi ya wana CCM waliozowea kudekezwa. Lakini upepo wa Upemba na kuwa mtu wa Mwenyekiti anaeogopwa ulilazimisha watu kushikamana wasikose yote. Walau Dkt Mwinyi angetosha na kweli ametosha baada ya kura za Kusini na Kaskazini Unguja kugawiwa.

Kwa kiasi kupitishwa kwa Dkt Mwinyi kuna usalama wa wastani kwa CCM kuliko angepitishwa Mnyaa. Mwenyekiti ameruka mtego kiasi.

"NGUVU YA MFUMO ULIOKWISHWA KUMUANDAA DKT MWINYI NA USALAMA WA CHAMA UMEPINDISHA MSIMAMO WA MWENYEKITI KWENYE DAKIKA 15 KIPINDI CHA KWANZA". Nguvu hiyo imemtoa Prof kwenye reli.

Siasa ni hesabu.

Almuradi CCM kindaki kindaki na wana ASP asili wamenuna. Ila kwa wahafidhina wasioitakia mema Zanzibar kidogo wameshusha pumzi kuliko angepita Mnyaa.

Watu wamenuna kiasi na picha nyengine ya kudharauliwa chaguo halisi la Zanzibar kwa wana CCM limedhihiri tena.

KUHUSU DKT MWINYI.

Huyu aliandaliwa mapema kuja kushika nafasi ya urais wa Zanzibar na tetesi zinasema hata urais wa JMT huko mbele.

Ana aminiwa kuwa ametengenezwa kuulinda Muungano kuliko CCM wengine ambao mara kadhaa huzusha zogo pale maslahi yao yanapohojiwa ndani ya CCM Zanzibar . Alitengenezwa sana huyu LAKINI Utawala uliopo haukumpa kipaumbele kwa kuepuka makambi yaliyoko Bara.

Utawala uliopo unamuona ni zao la wale wale waliozoea kubweteka na wasiosimamia maamuzi ya hapa kazi tu lakini mfumo ndio uliokwisha kumuandaa.

Bye bye Zanzibar. Usiniulize kwa nini.


Kwa hisani ya wanachimbo walioko Field Zanzibar



Kishada
Zanzibar ni mkoa tu wa Tanzania. Hizo nyingine ni mbwembwe za kisiasa.
 
Wafuatiliaji wetu walioko Zanzibar wametuletea tathmini hii fupi mara baada ya NEC ya CCM kumteua Dkt Hussein Mwinyi.

Kwanza baadhi ya wana CCM wamenuna wakilalamika kwamba wazanzibari hawana tena chaguo lao kwenye CCM, isipokuwa Upande wa Bara ndio unamuweka Mtu mwenye Maslahi yao.

Kuingizwa Dkt Khalid na Shamsi kwenye tatu bora kulilenga kuzigawa kura za Zanzibar hasa Unguja ambapo kura zimeelekea zaidi kwenye maeneo ya watu wanakotoka. Shamsi kaungwa mkono kwa kura 16 ikiaminiwa zaidi ni wajumbe wa NEC kutoka Kusini Unguja na Khalid kura 19 kutoka Kaskazini Unguja ambapo anatoka. Dkt Hussein kanufaika na kura za NEC bara na baadhi ya kura za mijini Magharibi ambazo zinanasibishwa na watu kutoka Tanzania Bara ambao ni wazanzibari wenye maslahi na Bara.

Kelele za kumkataa Mnyaa ambae inasemekana alikuwa chaguo la Watawala zilipindisha maamuzi mapenma ili kuepuka chuki ya wazi ambayo ingekigawa chama. Mwenyekiti na Timu yake walishtuka mapema. Taarifa zinabainisha ndio sababu ya kupelekwa Shamsi na Khalid ili kutuliza mpasuko wa kura za Unguja za mkoa wa Kaskazini na kusini.

Waliopanga mchezo walitegesha ilimradi maslahi ya Bara yamezingatiwa. Acha Mbarawa atote lakini Mwinyi apite na Bara ipete huo ndio msemo wa Mwisho ' Acha Mbarawa atote, Mwinyi apite na bara ipete"

KWA NINI MNYAA alilazimika kuachwa?
Nimeeleza kidogo. Huyu alihesabika mtu asiyewafaa wana CCM wahafidhina na wale maslahi. Ukweli ni kwamba Rais MAGUFULI anaogopwa na hata CCM wenzake. Zanzibar kuna utamaduni wa ulaji na kupendeleana sana . Ufisadi ndani ya serikali ni mkubwa na huwa wanalindana.

Prof Alihatarisha maslahi ya wana CCM waliozowea kudekezwa. Lakini upepo wa Upemba na kuwa mtu wa Mwenyekiti anaeogopwa ulilazimisha watu kushikamana wasikose yote. Walau Dkt Mwinyi angetosha na kweli ametosha baada ya kura za Kusini na Kaskazini Unguja kugawiwa.

Kwa kiasi kupitishwa kwa Dkt Mwinyi kuna usalama wa wastani kwa CCM kuliko angepitishwa Mnyaa. Mwenyekiti ameruka mtego kiasi.

"NGUVU YA MFUMO ULIOKWISHWA KUMUANDAA DKT MWINYI NA USALAMA WA CHAMA UMEPINDISHA MSIMAMO WA MWENYEKITI KWENYE DAKIKA 15 KIPINDI CHA KWANZA". Nguvu hiyo imemtoa Prof kwenye reli.

Siasa ni hesabu.

Almuradi CCM kindaki kindaki na wana ASP asili wamenuna. Ila kwa wahafidhina wasioitakia mema Zanzibar kidogo wameshusha pumzi kuliko angepita Mnyaa.

Watu wamenuna kiasi na picha nyengine ya kudharauliwa chaguo halisi la Zanzibar kwa wana CCM limedhihiri tena.

KUHUSU DKT MWINYI.

Huyu aliandaliwa mapema kuja kushika nafasi ya urais wa Zanzibar na tetesi zinasema hata urais wa JMT huko mbele.

Ana aminiwa kuwa ametengenezwa kuulinda Muungano kuliko CCM wengine ambao mara kadhaa huzusha zogo pale maslahi yao yanapohojiwa ndani ya CCM Zanzibar . Alitengenezwa sana huyu LAKINI Utawala uliopo haukumpa kipaumbele kwa kuepuka makambi yaliyoko Bara.

Utawala uliopo unamuona ni zao la wale wale waliozoea kubweteka na wasiosimamia maamuzi ya hapa kazi tu lakini mfumo ndio uliokwisha kumuandaa.

Bye bye Zanzibar. Usiniulize kwa nini.


Kwa hisani ya wanachimbo walioko Field Zanzibar



Kishada
Mada kama hizi huwa zinanipa shida sana.

Hubidi nibadili mawani mara tatu ili nisome na kuzielewa, lakini wapi, nabaki na kichwa kinazunguka tu mwisho wa kuzisoma.
 
Jiwe ametambua kwamba anawahitaji wale wazee waliomtangalio kwenye hiko kiti kuliko alivyozani hapo awali, tena hasa kipindi hiki cha uchaguzi, kaona hasara kuna hasara kubwa ya kubaki peke yake, ambayo inaweza kumcost hata kupoteza urais, sasa tayari kashamtega mzee mwinyi, tuone kwa kikwete, je ridhawani atapitishwa kule Bagamoyo? Kwa mkapa atafanyaje? Ngoja tuendelee kutafuna korosho toka mtwara, wakati game linaendelea.
 
Acheni nongwa
Wagombea walikua 31,wamechujwa na kubaki watano
Wagombea ni wazanzibari,wachujaji ni wazanzibari
Dodoma.yameletwa majina ya wazanzibari watano,ni lazima apite mmoja
Acheni nongwa
Mambo ya aibu,mnaifanya Zanzibar koloni la Tanganyika/Tanzania?Mikanganyiko imezidi,unashindwa kuelewa aina hii ya Muungano wetu ni kwa ajili ya nani hasa?Kero zingeisha once and forever endapo kungekuwa na serikali tatu au moja.Hizi mbili,???
 
Mambo ya aibu,mnaifanya Zanzibar koloni la Tanganyika/Tanzania?Mikanganyiko imezidi,unashindwa kuelewa aina hii ya Muungano wetu ni kwa ajili ya nani hasa?Kero zingeisha once and forever endapo kungekuwa na serikali tatu au moja.Hizi mbili,???
Jomba kero zimebakia ngapi unazozijuaa kwani katika hizi serikali mbil
 
Mimi iki kitu ndio huwa sielewi mgombea wa uraisi zanzibar anapitishwa na nec bara ..kwa nini nec zanzibar wasikae wakapitisha mtu wao huko ndio aje bara wasalimu

Ni hilo tu ambalo hulielewi? Mfumo mzima wa muungano haueleweki kabisa. Baraza la wawakilishi na bajeti zao, polisi, uhamiaji, fedha, uraia na mamlaka ya rais ni miongoni mwa issue ambazo hazieleweki kabisa. Halafu kuna hili suali la zanzibar ni nchi au mkoa. Yaani ni rahisi kujibu suali la baina kuku na yai nani kaja mwanzo, kuliko hili la zanzibar ni nchi au mkoa.
 
Wafuatiliaji wetu walioko Zanzibar wametuletea tathmini hii fupi mara baada ya NEC ya CCM kumteua Dkt Hussein Mwinyi.

Kwanza baadhi ya wana CCM wamenuna wakilalamika kwamba wazanzibari hawana tena chaguo lao kwenye CCM, isipokuwa Upande wa Bara ndio unamuweka Mtu mwenye Maslahi yao.

Kuingizwa Dkt Khalid na Shamsi kwenye tatu bora kulilenga kuzigawa kura za Zanzibar hasa Unguja ambapo kura zimeelekea zaidi kwenye maeneo ya watu wanakotoka. Shamsi kaungwa mkono kwa kura 16 ikiaminiwa zaidi ni wajumbe wa NEC kutoka Kusini Unguja na Khalid kura 19 kutoka Kaskazini Unguja ambapo anatoka. Dkt Hussein kanufaika na kura za NEC bara na baadhi ya kura za mijini Magharibi ambazo zinanasibishwa na watu kutoka Tanzania Bara ambao ni wazanzibari wenye maslahi na Bara.

Kelele za kumkataa Mnyaa ambae inasemekana alikuwa chaguo la Watawala zilipindisha maamuzi mapenma ili kuepuka chuki ya wazi ambayo ingekigawa chama. Mwenyekiti na Timu yake walishtuka mapema. Taarifa zinabainisha ndio sababu ya kupelekwa Shamsi na Khalid ili kutuliza mpasuko wa kura za Unguja za mkoa wa Kaskazini na kusini.

Waliopanga mchezo walitegesha ilimradi maslahi ya Bara yamezingatiwa. Acha Mbarawa atote lakini Mwinyi apite na Bara ipete huo ndio msemo wa Mwisho ' Acha Mbarawa atote, Mwinyi apite na bara ipete"

KWA NINI MNYAA alilazimika kuachwa?
Nimeeleza kidogo. Huyu alihesabika mtu asiyewafaa wana CCM wahafidhina na wale maslahi. Ukweli ni kwamba Rais MAGUFULI anaogopwa na hata CCM wenzake. Zanzibar kuna utamaduni wa ulaji na kupendeleana sana . Ufisadi ndani ya serikali ni mkubwa na huwa wanalindana.

Prof Alihatarisha maslahi ya wana CCM waliozowea kudekezwa. Lakini upepo wa Upemba na kuwa mtu wa Mwenyekiti anaeogopwa ulilazimisha watu kushikamana wasikose yote. Walau Dkt Mwinyi angetosha na kweli ametosha baada ya kura za Kusini na Kaskazini Unguja kugawiwa.

Kwa kiasi kupitishwa kwa Dkt Mwinyi kuna usalama wa wastani kwa CCM kuliko angepitishwa Mnyaa. Mwenyekiti ameruka mtego kiasi.

"NGUVU YA MFUMO ULIOKWISHWA KUMUANDAA DKT MWINYI NA USALAMA WA CHAMA UMEPINDISHA MSIMAMO WA MWENYEKITI KWENYE DAKIKA 15 KIPINDI CHA KWANZA". Nguvu hiyo imemtoa Prof kwenye reli.

Siasa ni hesabu.

Almuradi CCM kindaki kindaki na wana ASP asili wamenuna. Ila kwa wahafidhina wasioitakia mema Zanzibar kidogo wameshusha pumzi kuliko angepita Mnyaa.

Watu wamenuna kiasi na picha nyengine ya kudharauliwa chaguo halisi la Zanzibar kwa wana CCM limedhihiri tena.

KUHUSU DKT MWINYI.

Huyu aliandaliwa mapema kuja kushika nafasi ya urais wa Zanzibar na tetesi zinasema hata urais wa JMT huko mbele.

Ana aminiwa kuwa ametengenezwa kuulinda Muungano kuliko CCM wengine ambao mara kadhaa huzusha zogo pale maslahi yao yanapohojiwa ndani ya CCM Zanzibar . Alitengenezwa sana huyu LAKINI Utawala uliopo haukumpa kipaumbele kwa kuepuka makambi yaliyoko Bara.

Utawala uliopo unamuona ni zao la wale wale waliozoea kubweteka na wasiosimamia maamuzi ya hapa kazi tu lakini mfumo ndio uliokwisha kumuandaa.

Bye bye Zanzibar. Usiniulize kwa nini.


Kwa hisani ya wanachimbo walioko Field Zanzibar



Kishada
Tunaelekea serikali moja tu .
 
Back
Top Bottom