Sikubaliani na uchambuzi wako hasa kwenye viwango vya uwezekano wa Simba kuwa bingwa kufikia 60% wakati Azam umeipa 10%. Unamaanisha Yanga ni 30% Huu ni mzaha mkubwa!
Ukweli ni kwamba uwezekano wa Simba Yanga na Azam kuwa bingwa ni karibu sawasawa! Ukiacha sababu zilezile za msingi kama ubora wa vikosi na wachezaji, ubora wa mabenchi ya ufundi, matuzo safi, na mengineyo yanayofanana na hayo, timu hizi zina ubora uanokaribiana sana. Tofauti yoyote iliyopo au itakayoonekana inatokana zaidi na mambo matatu;
1. Hamu/Njaa ya Ubingwa (40%)
2. Matumizi ya viwanja vya ugenini(35)
3. Ukubwa wa kikosi(25%)
Ukiangalia timu hizi zote tatu, zina ingredients nyingi zinazofanana za kuwa bingwa. Hata hivyo, Azam na Simba zinaonekana kufanya vzr zaidi kwenye vipengele hivyo kuliko Yanga. Kwangu mimi, Simba inaweza kuwa na nafasi lkn kwa utofauti mdogo sana. Simba wana njaa/kiu sana ya ubingwa. Kuanzia mashabiki, wachezaji, viongozi, na wadau wanazungumza lugha moja tu ubingwa. Hili wanalisema waziwazi, tena na tena kila mara. Biblia inasema 'Ajionavyo mtu nafsini, ndivyo alivyo' na Simba tayari wameshajiona wana haki ya kuwa mabingwa, basi 'nguvu hii' itawafikisha mbali sana, kama sio ubingwa basi karibia na ubingwa.
KIPENGELE MCHANGO YANGA AZAM SIMBA
NJAA YA UBINGWA 40% 12% 13% 15%
MATUMIZI YA VIWANJA VYA UGENINI 35% 12.5% 15% 12.5%
UKUBWA WA KIKOSI 25% 13% 13% 14%
JUMLA 37.5% 41% 41.50%
Uwezekano wa nafasi mwisho wa msimu 3 2 1
Huioni hali hii ktk mitaa ya Jangwani kwa sababu tayari wana hangover ya mafanikio ya msimu uliopita. Lugha yao ya mwili inaonesha kujiamini zaidi kwa sababu wanasema ubingwa kwao ni kama kawa. Azam pia inaonekana wana mikakati ya kuda mrefu kupitia benchi lao jipya la kihispaniola, lakini hata wao ukimsikia msemaji wao Jaffary Iddy, muda mwingi ana kauli za 'tunataka kufanya vizuri'. Kitu kizuri kuhusu Azam, pamoja na kuwa na malengo ya muda mrefu, wameanza vizuri ligi, na Wahispaniola wamefit haraka ktk mpira wa kibongo kiasi cha kushinda ugenini mfululizo. Hii ni dalili nzuri kwa timu inaayotaka ubingwa. Tumoena Simba na Yanga zikipata sare ktk michezo yao ya ugenini kwa Ndanda na JKT Ruvu. (Simba wanadaiwa waikuwa ugenini).
Kitendo cha Azam kucheza mara kwa mara kwenye viwanja vya Mabatini na Manungu, kinaweza kuwa kichocheo cha kuzoea mazingira yote kiasi cha kujichukulia pointi huko Sokoine Mbeya. Yanga, hata ile ya mwaka jana ilikuwa ikistrugge sana kupata ushindi kwenye viwanja wanavyoviita chakavu,na tayari wamesikika wakilalamikia uwanja wa Nangwanda Sijaona.
Simba bado ni pameja kuona watafanyaje wakianza kutoka nje ya Dar, lkn nao huwa na visingizio hivihivi wanapocheza ugenini, mikoani.
Ukiangalia ukubwa kikosi, nashawishika kuipa tena Simba nafasi kubwa. Wana wachezaji wengi wenye ubora unaolingana. Ukiona mtu kama Jjuuko Murshid anasubiri benchi na bado timu inapata ushindi, ujue kuwa mwaka huu Simba wamefanyia kazi mapungufu yao yale ya kutokuwa na wachezaji mbadala. Huu ulikuwa ni ugonjwa mkubwa kwa msimu miwili mitatu huko nyuma ambapo Simba ilikuwa na wachezaji angalau 13 au 14 na wengine wakitajwa kukamilisha tu idadi, tofati na Yanga ambayo aliyeko uwanjani na benhi wote ni ubora mtupu.
Kwa sasa, Yanga wanaoonekana kuwa na pancha kwenye eneo la ulinzi ka kiungo wa ulinzi. Ni ngumu kufikiria kama Yanga inaweza kushinda mechi tatu ngumu mfululizo ambayo Thabani Kamusoko hatakuwepo uwanjani! Eeno la ulinzi nao ni tegemezi sana kwa Vincent Bosou. Kwa upande wa Azam, bado eneo lao la ulinzi halina wachezaji wake fit hususani kaka jambazi, Paschal Wawa. Wachezaji wapya waliosajiliwa bado hawajatuonyesha kitu cha tofauti sana, na badala yake tunaona eneo la ushambuliaji likimtegemea bado John Bocco.
All in all huu ni mtazamo tu na uzuri ni kwamba mchezo wa mpira hautabiriki, maana yake ukidhani hivi kumbe inakuwa hivi.Pia huwa kuna sababu ambazo huwa ziko nje ya upeo wetu mashabiki na wapenzi wa mpira ila kitu kimoja hubaki kuwa kweli kwamba aliyejiandaa vizuri na mwenye ari ya mafanikio hufika mbali katika mashindano. Ni sawa na methali ya Kiswahili isemayo Mgaagaa na Upwa hali wali mkavu.