Tathmini: Kesho bora ya Tanzania inategemea uwepo wa Katiba Mpya

Mkuu hebu weka mbinu zinazopaswa kufanyika ili kupata katiba mpya. Nadhani nikiona mbinu zako naweza kupata mwanga zaidi.
 

Hapa ndipo tunapopotezwa maboya. Tunahitaji uongozi, uratibu na msukumo wa force iliyo na dhamira, uthubutu na iliyo organized.

Chadema, ma Imamu wa Shura na wa namna hiyo tuwapende au tusiwapende, hawa ndiyo watakaotuvusha.

Mzizi mkubwa wa fitina uko hapa:



Maimamu wa Shura walifanya haya:



Katiba mpya mbona ipo sana hapa!
 
Mkuu hebu weka mbinu zinazopaswa kufanyika ili kupata katiba mpya. Nadhani nikiona mbinu zako naweza kupata mwanga zaidi.

Mkuu japo yote yameelezwa vyema kwenye mada, ninaya summarize tena hapa kwa ufupi kwa ajili yako:

1. Lazima kuwa na uongozi wenye uthubutu kwenye jambo hili. Kuwepo kwa Force yenye nia, dhamira na organization inayoeleweka hakuepukiki. (Chadema, Maimamu wa Shura, na wa namna hiyo wana fit sana hapa)
2. Lazima kuwatambua maadui na washirika vyema. Kujipanga kuvumiliana within limits ni muhimu. Vita hivi vinahitaji watu wanaoweza kuhesabika.
3. Madhara kwa wahanga yanapaswa kufahamika na mipango thabiti ya kuya accommodate ikawepo.
4. Options zote zinapaswa kuwapo mezani. Kupatikana kwa katiba mpya hakuwezi kuja kwa hisani ya wanaonufaika na katiba iliyopo.
5. Elimu itabidi iendelee kutolewa wakati wote wa mpambano. Ni wazi kuwa sote kabisa tu wahanga wa katiba hii japo kwa viwango tofauti tu na wengine kwa kutokujua tu.
6. Pamoja na kuwa Mizani ya ushindi inaegamea zaidi kwetu, tusiache kujifunza na kutumia uzoefu wa wengine na hasa waliofanikiwa katika haraka kama hizi.

Ifahamike jitihada hizi zikishawashwa rasmi upepo utabadilika. Tutegemee top brass toka CCM wakiwamo Mama na wenziwe kujitokeza kutaka kuongoza mchakato huu. Ndipo tume zitakapofuata ambazo nazo tutataka ziwe huru.

Haya ni kama nionavyo miye. Katika hatua hii maboresho kutokea kokote yanakaribishwa. Kwa pamoja tutakwenda mbali zaidi.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 

Naunga mkono hoja, ila najaribu kuangalia changamoto za utekelezaji wa mapendekezo yako. Tukifanikiwa juu ya nusu ya mapendekezo yako, jambo zuri litatokea.
 
hivi kwani katiba mpya itawaletea hela? fanyeni kazi achani kelele za kitoto iliyopo inatosha
 
Naunga mkono hoja, ila najaribu kuangalia changamoto za utekelezaji wa mapendekezo yako. Tukifanikiwa juu ya nusu ya mapendekezo yako, jambo zuri litatokea.

Hata hivyo mkuu tambua wala hayako mambo mengi. Kutoka kwenye mada yaliyoko kwenye red yana husika:



Ninakazia: "It is not easy, but not impossible."
 
Hata hivyo mkuu tambua wala hayako mambo mengi. Kutoka kwenye mada yaliyoko kwenye red yana husika:

View attachment 1825423

Ninakazia: "It is not easy, but not impossible."

Najua inawezekana, lakini ukiachia cdm na viongozi kadhaa wa kidini, hakuna wengine walio Active kwenye kudai katiba mpya. Wengine wote wanasubiri mchakato ukubalike na wafaidika wa katiba hii mbovu, kisha waanze kujifanya wanatoa ushauri wa katiba nzuri.
 

Mkuu wawepo au wasiwepo wengine "Active kwenye kudai katiba mpya" hii haitakiwi kuwa issue tena.

Wapo ma opportunists wengi kama si wote wanataka kula matunda tu. Hawako tayari kupambana. Kama ilivyo, matokeo ya kwanza ya mapambano yatazaa tume ya kushughulikia katiba itakayo husisha makundi zaidi.

Ma optimists wote wako mkao wa kula. Wanasubiri ipatikane hiyo tume ya kufanyia kazi katiba mpya. Wao hawako tayari kuipigania kupatikana bali wanataka tu kuwapo kwenye tume. Hao huwezi kuwakwepa kabisa.

Namna ya kuyaepuka machungu yao ni kuhakikisha kuwa ule usemi wa kila mchuma janga hula na wakwao umesambaratishwa. Maimamu wa Shura waliliweza hilo.

Si mbaya pia kufahamu mwendazake awamu ya 5 alijipanga na kuwa brainwash vilivyo wenye uelewa mdogo:


Kwa gharama zozote, mwendazake alihakikisha anajipanga na kuwa manipulate wote hao kuwa upande wake.

Hilo ndiyo lile kundi jingine lisilojua uwepi wa mapungufu ya katiba bali lilioaminishwa kuwa wapinzani na kila mwenye nacho ndiyo chanzo cha matatizo yao 😂😂😂😂!

Hiiiiii bagosha!
 
Ndugu yangu tindo,nakubaliana nawe shingo upande.Natamani tutengeneze Platform itakayoratibu upatikanaji wa Katiba ya Wananchi bila kuhusisha vyama vya siasa simply kwa sababu CCM na serikali yake wakisikia kuwa wawe na uwanja sawa na CDM kwenye mjadala wa Katiba wanachanganyikiwa.Nakumbukia yaliyotokea 2014=kura za maruhani/marehemu na wagonjwa kwa njia ya e-mail.
May be Jukwaa la Katiba.
 

Platform unayoizungumza inaweza kuwa ndiyo hii ninayoiongelea kama tume. Hii kuzaliwa kwake bila kuwapo kwa utashi wa watawala haitawezekana.

Mamlaka inatakiwa kulazimika kuiruhusu platform (au tume) hiyo kuwepo. Vinginevyo hawataikubalia kufanya lolote. Kupata ridhaa ya mamlaka kwenye hilo haitakuwa rahisi na hapa ndipo haswa kwenye ugumu wenyewe tunaouongelea. Kwa hakika, hapo ndipo kwenye ule msingi mzima wa hatimaye kupata katiba mpya.
 
Yawezekana kweli SSH akaweza kuishangaza Dunia kuwa mwanamke wa kwanza Rais wa nchi kuipatia nchi yake KATIBA MPYA !! wacha tuone !!
 

Mkuu mbinu yoyote itakayoleta katiba mpya itumike, ww ukiwa na mbinu yoyote itekeleze bila kusubiri ruhusa ya yoyote, lakini kutaka hivyo vyama vya siasa visiwepo kwenye huo mchakato ni ngumu kidogo, labda kungekuwa na uhakika wa hiyo mbinu yako.
 
Yawezekana kweli SSH akaweza kuishangaza Dunia kuwa mwanamke wa kwanza Rais wa nchi kuipatia nchi yake KATIBA MPYA !! wacha tuone !!

Kumsubiria kwa utashi wake tu, Mama alete katiba mpya itakuwa dhahiri ni kusubiria dodo Kwenye mnazi:

 

Au mkuu hii platform unayopendekeza kwa mawazo yako inazaliwa vipi? Au tufanye je kuipata?
 
China hawajui demokrasia, lakini ndiyo imepiga maendeleo kiuchumi kuliko nchi zote duniani kwa miaka 30 iliyopita . Maendeleo yanaletwa na nidhamu ya kutumia fedha kwa matumizi sahihi yaliyopangwa na nidhamu ya haki ya juu kiutendaji. Siwezi kubeza umuhimu wa Katiba mpya , lakini peke yake sio kitu cha kuleta maendeleo
 

Mkuu usiishie China tu, hata North Korea, Iran, Saudia, nk kuliko na inayoitwa mikono ya chuma na kusemekana kuna maendeleo.

Waulize Ethiopia, Rwanda au hata Tanzania awamu ya Tano. Kwani makelele yote haya ya nini? Hatutaki tena nchi kuendeshwa kama shamba la mtu.

Panga pangua hakuna kilicho bora kuliko demokrasia. Ulizia Bangladesh, Kenya, SA au India pamoja na umasikini wao.

Serikali kama ni watu waache watu wenyewe wajitawale kwa ridhaa zao si kwa utashi wa mtu.
 
Unataka iwepo kura ya maoni kabla ya kupatikana Katiba Mpya? ukiiruhusu hiyo CCM watachakachua, coz wanazo weapon za kila aina kufanya hivyo.

Usiogope kelele za CCM kwenye hili, hata wao CCM wanajua Katiba Mpya inahitajika kila pembe ya nchi yetu, JK kufanya kile alichofanya hakupenda, ilimlazimu kufanya vile, naamini tukifanya kwa Samia pia itawezekana.

Hili lazima lifanyike bila kujali uwepo wa "snitch" kama viongozi wengine wa vyama vya upinzani, wacha Chadema ianzishe, then viongozi wa makundi mengine kama dini, taasisi za kiraia, na wengine wataunga mkono pale watakapoona matokeo chanya ya movement.

CCM wajanja, wanataka hili liachwe kwa vyama vya upinzani pekee mathalan Chadema ili iwe rahisi kwao kusema wananchi hawako tayari, na pale ambapo viongozi wa dini kwa mfano wakianzisha wataambiwa msichanganye dini na siasa, hii game wacha Chadema waiongoze wengine watafuata.
 
Tayari kinaumana. Tarehe 1 July ni rasmi:



Cha kujizatiti - Kamanda Muliro anaweza kumbuka kama Mambosasa na kama Muroto.

Mikakati inatakiwa kuwa imewekwa tayari. What if?

Hapa ndipo kwenye kuwapa salamu ya vipi tumedhamiria. Wasaa muhimu sana.

Au nasema uongo ndugu zangu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…