Tathmini: Shida ya maji hadi ziwa Victoria?

Tathmini: Shida ya maji hadi ziwa Victoria?

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Ni wazi kuwa kama nchi tunapita wakati mgumu sana uliohitaji busara zaidi kuliko maguvu.

Kuna shida ya maji Dar tuliyoaminishwa kuwa ni kupungua kwa maji mto Ruvu japo unaendelea kumwaga yake baharini.

Hivi kiwiano, maji kiasi gani yanavunwa Ruvu kulinganisha na yanayoishia baharini?

Kwamba leo tunaanza kulaumu hata ng'ombe kunywa maji ruvu na kilimo cha umwagiliaji?

Kwani huko kanda ya ziwa ambako shida ya maji nako imekamata kama Dar tu, nako ziwa Victoria limekauka?

Tusipoangalia tutamlaumu sana dobi na hata kutupia makombati juu, lakini kaniki litaendelea kuwa na rangi yake.

Faulo inazocheza serikali dhidi ya watu wake isijidanganye kuwa hazionekani. Ifahamike wapo watanzania wengi tu wasioridhika na faulo hizi waliomo ndani ya serikali yenyewe.

Kwamba watanzania hawajui madege mnayonunua kwa pesa zetu msizokuwa na mchango wowote, hatuzihitaji?

Kwamba watanzania hawajui faulo mnazofanya mahakamani?

Kwamba watanzania hawajui faulo mnazofanya bungeni?

Kwamba watanzania hawajui faulo mnazofanya polisi?

Kwamba watanzania hawajui faulo mnazofanya kwenye taasisi ipi? Kwani mnadhani wote ni wafuasi wenu?

Hamukuwahi kusikia viwalavyo vi nguoni mwenu?

-----------
Serikali ni kikundi cha watu kilichojitwalia madaraka kutoka kwa wananchi
 
Hivi kwa nini wasiende kupata ujuzi Nchi za kiarabu wakajifunze wao wametumia njia gani maana kule kuna ukame mno ila hakuna tatizo la maji mfano kama Dubai mpaka nje baadhi wanaweka Freji mpita njia ukisikia kiu unakunywa kuishi kwangu sijawahi kuona wana tatizo la umeme au maji.
 
Unapigwa mwingi kamanda. Tulia kwanza

Unadhani ofisi ya DPP mko wenyewe tu? Mnadhani polisi ni ninyi peke yenu?

Mnadhani ziwa Victoria limekauka? Au mnadhani Ruvu kumekauka au ng'ombe wamekunywa maji?

Vaeni kombati na hata bukta kabisa. Ila tulipo subirini kidogo hatuko mbali sana.
 
Hivi kwa nini wasiende kupata ujuzi Nchi za kiarabu wakajifunze wao wametumia njia gani maana kule kuna ukame mno ila hakuna tatizo la maji mfano kama Dubai mpaka nje baadhi wanaweka Freji mpita njia ukisikia kiu unakunywa kuishi kwangu sijawahi kuona siku wana tatizo la umeme au maji.

Uwezekano mkubwa ni kuwa hii ni sabotage.

Utawala umekuwa dhwalimu kupitiliza. Tutegemee mengi.
 
Hivi kwa nini wasiende kupata ujuzi Nchi za kiarabu wakajifunze wao wametumia njia gani maana kule kuna ukame mno ila hakuna tatizo la maji mfano kama Dubai mpaka nje baadhi wanaweka Freji mpita njia ukisikia kiu unakunywa kuishi kwangu sijawahi kuona siku wana tatizo la umeme au maji.
Haya matatizo ni sehemu ya kupigia pesa mkuu
 
Tatizo huduma za jamii kufanywa hisani ya watawala badala kuwa ni hitaji la lazima kwa wananchi
Sasa wananchi wenyewe ndio hao serikali ikiwajibika kwa kujenga barabara au kuunganisha umeme,maji wanapiga kabisa magoti eti tunashukuru mh.....kwa kutuletea....utafikiri ni hisani ... wakati ni kodi zao . kaazi kwelikweli
 
Sasa wananchi wenyewe ndio hao serikali ikiwajibika kwa kujenga barabara au kuunganisha umeme,maji wanapiga kabisa magoti eti tunashukuru mh.....kwa kutuletea....utafikiri ni hisani ... wakati ni kodi zao . kaazi kwelikweli
Ujinga ni mtaji mzuri wa CCM
 
Back
Top Bottom