Mabibi na mabwana hii ni tathmini fupi ya matukio yanayoendelea na ugonjwa huu hapa nchini. Kwa hakika ni wazi kuwa pana tafahadhari nyingi na za msingi sana ambazo sasa hivi wananchi wao kama juhudi binafsi tu, wanazichukua.
Ama kweli "Mwenye macho haambiwi tazama." Kama vifaranga wa kuku sasa hivi watanzania wanachakura vilivyo labda baada ya kutambua kumsubiria mama kuwafunza wanachelewa bure.
Ninaleta uzi huu baada ya kuwa nimeshiriki katika shughuli za mazishi kadhaa zikiwamo kuwasafirisha wapendwa kadhaa waliotangulia; kwa mazishi ndani na nje ya Dar.
Kwa hakika wananchi wanaonekana kuwa wamefuzu kwa mafunzo ya vitendo. Wananchi wamepigika na wametambua kuwa ni lazima kubadilika.
Kwa hakika aisifuye mvua, si bure! Baada ya mama kutowafunza, kwa hakika dunia imewafundisha bahati mbaya kwa hesabu za wafu!
Yafuatayo ni niliyoyaona:
1. Kuna mwamko mkubwa sana wa kuvaa barakoa kwa waombolezaji kwa Dar kuliko mno kulinganisha na huko mikoani.
Ni wazi kuwa kwa siku za karibuni kwenye mikusanyiko ya mazishi Dar waombolezaji waliovaa barakoa ni wengi zaidi kuliko wasiovaa.
Kimsingi si nadra kuona hata kufikia 95% ya waombolezaji wakiwa wamevaa barakoa kwenye msiba mmoja.
Jambo la kheri kabisa.
2. Heshima za mwisho Dar kwa marehemu wengi kwa siku za karibuni, zinatolewa sasa bila ya kufungua majeneza tena, kulinganisha na ilivyo kuwa siku za nyuma.
Hii ni mahsusi zaidi kwa wale wapendwa wengi wanaokuwa wametangulia, changamoto za kupumua zikiwa sehemu ya visababishi.
Jambo la kheri kabisa.
3. Katika moja ya misiba, kigogo mmoja wa serikali alikataa kutumia microphone iliyokuwa ikitumika kwenye matangazo mbali mbali hapo msibani.
Mnene huyo alichagua kutoa neno lake bila ya kujali kuwa kusikika kwake kulikuwa kwa taabu katika kadamnasi hiyo.
Jambo la kheri kabisa.
4. Uwepo wa watu msibani umekuwa unazingatia sana kupunguza mrundikano. Primitive social distancing inakuwa implemented na wananchi kama juhudi binafsi.
Jambo la kheri kabisa.
Jitihada zinazofanyika kuwaelimisha wananchi pamoja na vizingiti vilivyopo hazipotei bure.
Alisema Museveni, "maendeleo ya Uganda hayawezi kuwasubiria wakaramoja kujua umuhimu wa kuvaa suruali."
Kitisho cha ugonjwa huu ni dhahiri.
Watu wanapoendelea kufa, bila kujali nani anasema nini, mwenye macho haambiwi tazama. Wananchi waendelee kuchukua hatua.
Penye nia pana njia.
Ninawasilisha.
Ama kweli "Mwenye macho haambiwi tazama." Kama vifaranga wa kuku sasa hivi watanzania wanachakura vilivyo labda baada ya kutambua kumsubiria mama kuwafunza wanachelewa bure.
Ninaleta uzi huu baada ya kuwa nimeshiriki katika shughuli za mazishi kadhaa zikiwamo kuwasafirisha wapendwa kadhaa waliotangulia; kwa mazishi ndani na nje ya Dar.
Kwa hakika wananchi wanaonekana kuwa wamefuzu kwa mafunzo ya vitendo. Wananchi wamepigika na wametambua kuwa ni lazima kubadilika.
Kwa hakika aisifuye mvua, si bure! Baada ya mama kutowafunza, kwa hakika dunia imewafundisha bahati mbaya kwa hesabu za wafu!
Yafuatayo ni niliyoyaona:
1. Kuna mwamko mkubwa sana wa kuvaa barakoa kwa waombolezaji kwa Dar kuliko mno kulinganisha na huko mikoani.
Ni wazi kuwa kwa siku za karibuni kwenye mikusanyiko ya mazishi Dar waombolezaji waliovaa barakoa ni wengi zaidi kuliko wasiovaa.
Kimsingi si nadra kuona hata kufikia 95% ya waombolezaji wakiwa wamevaa barakoa kwenye msiba mmoja.
Jambo la kheri kabisa.
2. Heshima za mwisho Dar kwa marehemu wengi kwa siku za karibuni, zinatolewa sasa bila ya kufungua majeneza tena, kulinganisha na ilivyo kuwa siku za nyuma.
Hii ni mahsusi zaidi kwa wale wapendwa wengi wanaokuwa wametangulia, changamoto za kupumua zikiwa sehemu ya visababishi.
Jambo la kheri kabisa.
3. Katika moja ya misiba, kigogo mmoja wa serikali alikataa kutumia microphone iliyokuwa ikitumika kwenye matangazo mbali mbali hapo msibani.
Mnene huyo alichagua kutoa neno lake bila ya kujali kuwa kusikika kwake kulikuwa kwa taabu katika kadamnasi hiyo.
Jambo la kheri kabisa.
4. Uwepo wa watu msibani umekuwa unazingatia sana kupunguza mrundikano. Primitive social distancing inakuwa implemented na wananchi kama juhudi binafsi.
Jambo la kheri kabisa.
Jitihada zinazofanyika kuwaelimisha wananchi pamoja na vizingiti vilivyopo hazipotei bure.
Alisema Museveni, "maendeleo ya Uganda hayawezi kuwasubiria wakaramoja kujua umuhimu wa kuvaa suruali."
Kitisho cha ugonjwa huu ni dhahiri.
Watu wanapoendelea kufa, bila kujali nani anasema nini, mwenye macho haambiwi tazama. Wananchi waendelee kuchukua hatua.
Penye nia pana njia.
Ninawasilisha.