Tatizo la dini ni waumini wake kujikita kwenye mambo mepesi na kuacha mazito yanayogusa binadamu wenzao

Tatizo la dini ni waumini wake kujikita kwenye mambo mepesi na kuacha mazito yanayogusa binadamu wenzao

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Ukifuatilia waumini wa dini kubwa mbili za Ukristo na Uislamu utagundua huwa wanajikita au wanajielekeza katika mambo mepesi zaidi huku wakiwa hawatilii mkazo yale mazito ambayo yangeboresha maisha ya watu wanaowazunguka.

Mfano katika dini ya Ukristo kuna kitu kinaitwa Golden rule/ sheria ya dhaba inayosema "Watendee wengine vile ambavyo ungependa wewe kutendwa". Utakuta Wakristo wachache sana wanazingatia hii, ila wengi wao wamejikita kwenda kanisani, kutoa sadaka, wanasali kabla ya kula, kuvaa rozari na mambo mengine madogo madogo kama hayo.

Kwa upande wa uislamu nao kuna mambo mazuri yanayosisitiza utoaji haki kwa watu wote, kutoonea, kutodhulumu n.k lakini wengi wao wamejikita katika masuala mepesi ya kuswali mara nyingi kwa siku, kuvaa ushungi, kanzu, kutokula kitimoto n.k

Kama watu wa dini wangeyapa uzito mkubwa zaidi mambo yanayogusa binadamu wenzao wanaowazunguka hakika dunia ingekuwa sehemu iliyo bora zaidi na yenye furaha zaidi.
 
Uislamu na ukristo ni kwaajili ya watu ambao ni wagonjwa wa akili na wameshindwa maisha ndio maana kila siku hawaishi kutukanana,kudhalilishana na hata kutishiana.

Ndio maana sisi tusio waamini,waumini na wafuasi wa dini hizi tunaishi kwa amani na upendo mkubwa miongoni mwetu na miongoni mwa wanajamii wengine including hata hao waislamu na wakristo.

Back to your topic naunga mkono hoja nilishawahi kumuambia mtu mmoja kushika sana dini hakukufanyi uwe una roho nzuri au uwe mtenda haki n.k kwasababu uislamu na ukristo unashughulika sana na matendo yako kuliko roho yako na roho za wengine. Hii inafanya mtu awe muislamu sana au mkristo sana na sio mchamungu sana that is the reason mtu anashinda msikitini au kanisani halafu mchawi yeye,roho mbaya ya kwake yeye,dhuluma ya kwake yeye n.k
 
Back
Top Bottom