Tatizo la kina cha msingi wa nyumba

Tatizo la kina cha msingi wa nyumba

vipi kama ukitumia meshwire kwenye kufunga mkanda wa msingi badala ya nondo kwenye ardhi ya udongo wa mfinyanzi?
je msingi utakuwa imara kama mtu aliyetumia nondo?
Waya mesho ziende sanjali na nondo lakini ni kama unamwaga jamvi plain Eneo kubwa ila sio kwa msingi.

Funga plinth beam ya nondo za mm 10 juu na 12 chini afu zufunge kwa nondo za mm 8 kwa spacing ya 30cm au chini ya hiyo.

Kina cha zege uwe 25cm au isipungue 20cm ,ukizingatia mchanganyo kwa ratio ya grade 25 au 20 na umwage maji ya kutosha kwa siku 7 asubuh na jioni utakuwa umeimarisha msingi na hakuna tatizo lolote tena
 
Waya mesho ziende sanjali na nondo lakini ni kama unamwaga jamvi plain Eneo kubwa ila sio kwa msingi.

Funga plinth beam ya nondo za mm 12 juu na 10 chini afu zufunge kwa nondo za mm 8 kwa spacing ya 30cm au chini ya hiyo.

Kina cha zege uwe 20cm au isipungue 15cm ,ukizingatia mchanganyo kwa ratio ya grade 25 au 20 na umwage maji ya kutosha kwa siku 7 asubuh na jioni utakuwa umeimarisha msingi na hakuna tatizo lolote tena
Unamaanisha nini unaposema juu uweke 12mm na chini uweke 10mm kwenye plinth beam?

Sio kwamba nondo za chini ndio zinatakiwa ziwe kubwa kuliko za juu?
 
Waya mesho ziende sanjali na nondo lakini ni kama unamwaga jamvi plain Eneo kubwa ila sio kwa msingi.

Funga plinth beam ya nondo za mm 12 juu na 10 chini afu zufunge kwa nondo za mm 8 kwa spacing ya 30cm au chini ya hiyo.

Kina cha zege uwe 20cm au isipungue 15cm ,ukizingatia mchanganyo kwa ratio ya grade 25 au 20 na umwage maji ya kutosha kwa siku 7 asubuh na jioni utakuwa umeimarisha msingi na hakuna tatizo lolote tena
Asante sana mkuu
 
Kuna mtu kaja pm anauliza,huwa sijibu mambo ya pm tuulizane hapa hapa kwa faida ya wengi na pia kwa kukosoana

Ila ishu yake ilikuwa je nilazima amwage zege yaani reinforced concrete kwenye Eneo lote yaani juu ya msingi wa jengo ukiacha kuzunguka msingi tuu?

Jibu ni ndio kama uko vizuri mfukoni kimsingi ndio standard ya msingi wa jengo inataka.Ila kama pesa za mawazo just mwaga around foundations kwa upana wa tofari na kina kisichopungua cm 20

Zingatia nafasi ya kitaalamu kwa nondo za mm 8 yaani stirrups ni muhimu sana hiyo kuzuia cracks zitakazotoka anzia chini kupanda juu.
 
Ka diploma ndio nini mkuu,aisee bora utafute diploma holder anauzoefu wa changamoto za site kuliko graduate wa makaratasi

Nyumba za kawaida sio ghorofa haxihitaji injinia yeyote hapo
Kwani Graduate hawezi kuwa na uzoefu wa site??
 
basi brother tambua huwa hakuna mbadala wa msingi wa nyumba, msingi ndio nyumba yenyewe, kwa hiyo namna pekee ni wewe kukubali hasara ila usikubali kupata hasara zaidi kwa kutafuta mbadala wa kuacha kuchimba upya msingi wa nyumba yako.

Ushauri uliopewa wa kuzungusha tofali nyingine nje hautokusaidia maana hauna uhakika hata kitako kilichopo sasa kwenye hizo tofali sita kitaweza kuhimili jengo, asee nyumba ni kitu kingine mkuu! tofali unazoshauriwa uzizungushe hazitabeba uzito wa nyumba bali zitazuia tu erosion , chimba msingi kwenda chini upate layer ngumu ndipo ujenge msingi wako wa nyumba. Ni kheri uchelewe ufike kuliko kuharakisha alafu usifike unakokwenda.


Kila la kheri
Option hii ni hasara mkuu, kwanza, ujenzi wa kitanzania hakuna anayechimba hadi kuikuta layer ngumu labda majengo ya Serikali. Layer ngumu unaweza kuikuta mita moja chini! Ina maana huo msingi pekee hadi uchomoze nje ya ardhi kwa tofari nne si utakuwa na kozi 15! Too expensive! Mi naona options rahisi na bora ni kujaza kifusi kwenye uwanja wa nyumba yake kwa kuhakikisha kozi tatu zinazama chini ya ardhi. That is simple. Tunajenga nyumba za kudumu miaka 50 hadi 70 na sio za kudumu milele.

Option nyingine ni chagua pembe za kimkakati ambazo zinabeba uzito wa jengo. Kisha hizo pembe/kona vunja na chimba kwenda chini kadri upendavyo na uweke nguzo ya zege itakayoishia kwenye beam ya msingi. Hapo hutakaa upate tatizo kwenye msingi wako.
 
Habari za humu jamvini waheshimiwa.

Nawapongeza sana kwa uwepo wenu kwenye jukwaa hili muhimu.

Mada:
Mimi nilifanya tathmini ya gharama za kujenga msingi wa nyumba ya vyumba vitatu, sebule, sehemu ya chakula, jiko na choo.
Na tukaafikiana vizuri na fundi.

Nikapambana kununua materials zote ili kuanza ujenzi.
Siku ya kuanza ujenzi nikapatwa na safari ya dharura, nikamwachia mdogo wangu asimamie usalama wa vifaa na kuwalipa mafundi.

Kazi ikafanyika, baada ya wiki moja ikakamilika.

Changamoto niliyoibaini baada ya kurejea ni kwamba,
Mafundi wamejenga msingi ambao umeinuka sana juu, Ila haujaenda chini.

Kwenye msingi wa jumla ya kozi sita (6),
Chini imeenda tofali moja tu, halafu tano zote zimekuja juu.

Hata kama ardhi ni tambarare,
Je, hii haina madhara kwa nyumba waheshimiwa?

Na kama yapo, kuna namna m'badala ya kuiimarisha nyumba?

NB: Bado sijainua boma.
Kiongozi hapo hakuna msingi, suluhisho ni kubomoa kama bado hujabomoa, utakuja angusha nyumba uingie gharama mara mbili. hicho kilichofanyika hakina sifa ya kuitwa msingi. Sijui kama uliemtumia ni fundi kweli au janja janja.Fundi anae jielewa asingeruhusu hicho kilichofanyika kitokee.
 
Vipi uki mwaga mchanga + zege juu ktk arshi ya mfinyanzi ..msingi unakuwa imara zaidi bila shaka
Unamwaga zege 230mm thick then unapandisha tofali za 6 inch hizi huwa kwenye msingi zinalazwa 1.0 m high then unaweza funga ka mkanda kazege lenye nondo 200mm thick, unajaza kifusi hapo unakuwa umemalizana na msingi.

Hii aina ya msingi kitalamu inatwa strip foundation

Nyumba ni msingi, ukikosea hapo utakaa uichukie nyumba yako milele.
 
Option hii ni hasara mkuu, kwanza, ujenzi wa kitanzania hakuna anayechimba hadi kuikuta layer ngumu labda majengo ya Serikali. Layer ngumu unaweza kuikuta mita moja chini! Ina maana huo msingi pekee hadi uchomoze nje ya ardhi kwa tofari nne si utakuwa na kozi 15! Too expensive! Mi naona options rahisi na bora ni kujaza kifusi kwenye uwanja wa nyumba yake kwa kuhakikisha kozi tatu zinazama chini ya ardhi. That is simple. Tunajenga nyumba za kudumu miaka 50 hadi 70 na sio za kudumu milele.
Au sio unawapa ujumbe gani wale wanao nunua nyumba kali kwa bei chee [emoji16][emoji16][emoji16]
 
Back
Top Bottom