Duh hiyo kitu ilinitesa sana nikiwa mdogo. Nilikuwa namiss shule wiki nzima kifuta kimebana. Chai ya tangawizi au tangawizi henyewe ilinisaidia sana pamoja na vidonge vya aminophiline. Nilikuwa natembea navyo mfukoni yaani vumbi kidogo tu hichooo. Lkn nilipofika form 2 nikaanza cheza mpira tulikuwa na timu yetu daraja la nne na baadaye daraja la tatu. Yale mazoezi ya ligi yaliweza kutanua kifua kikawa mara chache mno. Mpaka sasa kikija kinakuja kwa mbali sana bado huwa nanunua aminophiline ingawa nikisikia zimepigwa marufuku lkn mie zilinisaidia sana.