Tatizo la kuingiza Maji kwa madirisha ya Aluminium

ZINDAGI

JF-Expert Member
Joined
Dec 5, 2015
Posts
1,118
Reaction score
1,430
NIna tatizo linanisumbua la kuingiza maji ndani kupitia madirisha ya Aluminium
Mvua kidogo tuu ikinyesha maji mengi yanaingia ndani, tumejaribu kujaza silicon lakini haikusaidia, naomba mwenye kujua suluhisho la hili tatizo, au kama kunafundi unamjua naomba tuwasiliane
 
Silicone umeweka wapi? Maana hilo tatizo nahisi maji yanaingilia kwenye njia za vioo, na kwenye upenyo unaotenganisha kioo na kioo, hata mijusi ndio inapopitia, hapo huwezi kuziba na silicone

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Silicone umeweka wapi? Maana hilo tatizo nahisi maji yanaingilia kwenye njia za vioo, na kwenye upenyo unaotenganisha kioo na kioo, hata mijusi ndio inapopitia, hapo huwezi kuziba na silicone

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu hata mbu si wanapitia hapo? Yaani hizi aluminium sliding windows naona ni fashion ambayo kwa majiji ya joto hazifai. Nikipata suluhisho la mbu kuingia kupitia madirishani nitafurahi sana.
 
Kiongozi
Hao Mafundi Wako Wanatakiwa Wayakate Huo Upande Unakaa Sambamba Na Ukuta Ili Mvua Ikinyesha Yanatiririka Kwenye Ukuta Kwa Nje
Idadi Kubwa Sana Ya Watu Hupatwa Hiyo Shida
 
Mkuu hata mbu si wanapitia hapo? Yaani hizi aluminium sliding windows naona ni fashion ambayo kwa majiji ya joto hazifai. Nikipata suluhisho la mbu kuingia kupitia madirishani nitafurahi sana.
Mkuu huwa kuna rubber fulani ambayo ni seal huwekwa hapo katikati ya kioo na kioo tembelea kwa mafundi wa aluminum utapata.
 
Mkuu fafanua zaidi tuelimike

Sent using Jamii Forums mobile app
Kuna Mafundi Wanachukua Kisu Huo Upande Unaokaa Sambamba Na Ukuta Ukatwa Ingawa Hutaweza Kuona Kiurahisi Sasa Mvua Ikija Maji Yake Hutiririka Hapo Hadi Ukutani


Haya Madirishi Yana Hizo Shida Sana Nyakati Za Mvua Unajua Wakati Mwingine Haupo Nyumbani
 
Nionanyo mimi, hayomadirisha yako yamekosewa kuwekwa au kukatwa wakati wa kutengenezwa
Upo mkoa gani ili uweze kupatiwa Fundi wa kukusaidia kurekebisha?
 
Maji yanapita wapi in the first place?
Hio silicone umejaza wapi?

Kuna kitu inaitwa Sikaflex 11FC.. ni tube kama silicone. Hio ni sealant na adhesive ya uhakika.. try that instead of silicone

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kingine pia hizi dirisha kutobolewa kwa chini vitundu vidogo kama outlet ili maji yakiingia kwenye reli yatoke nje. Vitundu vidogo tu wanatoboa na drill

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haya madirisha ni mazuri machoni lakini yanaruhusu mbu kupita, ni namna gani tunaweza kuthidbiti mbu wasipite?
 
Nina tatizo kama lako. Nimeshapiga dawa kwenye hizo wavu lakini hamna kitu

Sent using Jamii Forums mobile app
Binafsi sioni hata ubora wake hasa kwenye kuzuia mbu, yanaonekana mazuri kwa kutizama lakini hayafai kwa maeneo yenye joto kama mikoa ya pwani. Haya madirisha yanafaa huko kwenye baridi, lakini pia sio suluhisho la mbu.
 
Kuna zile ambazo zina steps kwa chini ndiyo suluhisho zile nyingine ni majanga matupu mvua ikinyesha maji yanatuhama moja kwa moja
 
Zipi hizo unaweza weka picha?
Kuna zile ambazo zina steps kwa chini ndiyo suluhisho zile nyingine ni majanga matupu mvua ikinyesha maji yanatuhama moja kwa moja
 
Zipi hizo unaweza weka picha?
Nikifika home huko Bushi nitapiga picha halafu nitarusha hapa, kunakuwa na steps kwa chini pale hivyo maji yanatoa nje
 
Nikifika home huko Bushi nitapiga picha halafu nitarusha hapa, kunakuwa na steps kwa chini pale hivyo maji yanatoa nje
Nitashukuru mkuu, tutakuwa tumesole tatizo la maji bado mbu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…