Tatizo la magoti

Tatizo la magoti

sweetdada

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2011
Posts
517
Reaction score
169
Wapendwa wana JF habari zenu wote,

Hii kam awiki ya pili magoti yanauma nikikaa yanavuuta inabidi nisimame kama dakika 10 hivi ndo nikae tena.

Hii inatokana na nini?
Kuna mtu kaniambia nivae bangili ya kopa itasaidia lakini hakueleza kwa undani.

Je kuna anayefahamu kopa na kuumwa kwa magoti kuna relation gani?
Msaada please kabla sijajipeleka hospitali.mi ni muoga sana wa hospitali.
 
Pole sana!
Usiogope hospitali ndugu!

anza kwa vipimo hospitali ili tatizo lijulikane. ni vigumu kukupa ushauri bila kujua kiini cha tatizo. ila kwa kupoza maumivu.

tumia maji baridi kuweka sehemu zinazouma, na pia epuka kukaa mikao ambayo inasababisha miguu yako kujikunja kwa muda mrefu.

Kunywa maji mengi na matunda kwa wingi bila kusahau mboga mchanganyiko (salad-kachumbari)
 
Asante sana Mwanamageuko nitafwata maelekezo
maumivu yakizidi itabidi niende tu hospital
 
Baridi yabisi inaweza kuwa au weigth kubwa kunywa dawa za calcium zinasaidia kuimarisha mifupa
 
Kuvaa bangili za kopa hakutasaidia kitu. Ushauri unaotolewa kuhusu kwenda hospitali, kula chakula bora, kupunguza uzito nk ndio wa kufuata.
 
Asanteni @Gaga &pmwasyoke

nitatafuta hizo dawa za calcium mana sina weight kubwa mi ni slim kabisa
nashukuru kwa ushauri wapendwa
 
kunywa dawa za calcium zinasaidia

nitatafuta hizo dawa za calcium nashukuru kwa ushauri wapendwa

I wouldn't do that.
It could be deposition disease. Collection of foreign materials in your joint. Adding Calcium may worsen whatever is deposited in the joint.
You said you are slim, and your age? some diseases are age related you know.
Have you been injured in your knee, or merely started itself?
The first thing I would have done is to see a doc, but since you have hospitallo-phobia, I cant help.
Try babu's cup, it does wonders i hear.
 
nenda hospitali hapo utapata kiini cha tatizo na tiba. Ila kama unakulaga sana nyama nyekundu hasa ya mbuzi husababisha maumivu ya magoti, pia na hata ya ng'ombe ingawa nyama ya mbuzi ni zaidi. Punguza au acha kabisa kula nyama ya mbuzi haf muone daktarikwa matibabu.
 
Mama yangu alikuwa na matatizo kama hayo, nikaagizwa dawa ambayo baada ya kuitumia matatizo yameondoka kabisa mwaka wa kumi sasa Pia nimekuwa nikiwashauri wengine na imeponyesha. Ikiwa unogopa hospitali, omba Mungu hii ukipenda:

1. Nunua shubiri ya kidonge (kwa wanaouza dawa za kienyeji. [Shubiri ni utomvu wa aina moja ya Alao Vera). Iloweke kwenye maji kidogo mpaka iyeyuke kabisa. Rangi yake inaweza kuwa nyuesi au brown.

2. Nunua mafuta ya zaituni (Olive oil, vile vile yanauzwa kwenye maduka ya dawa za kienyeji na baadhi ya maduka mengine).

3. Changanya shuburi iliyoyeyuka na mafuta, weka kwenye moto na koroga mara kwa mara. Chemsha kama dakika 5-10 mpaka ichemke. Iwache ipowe na hamishia kwenye chupa au chombo chochote cha kufunga, kwa tahadhari tu isije kumwagika.
ANGALIA: Usijaribu kutaka kujipunguzia kazi kwa kuchanganya shubiri na mafuta bila ya kuiyeyusha, itaganda kama gundi.

4. Kila siku, asubuhi unapoamka na usiku uanpotaka kulala, jipakae mchanganyiko huu kwenye sehemu inayouma. (Wiki moja hadi mbili).
 
@sigma..thnx for the advise..i've not been injured, it just started on its own..yes am slim and my age ranges btn 30-33, and hospitals are the last thing i think about..whenever i go to the hosp i feel dizzy and faint so al end up being treated for what took me there and the fainting thingy.

@MAMMAMIA..nashukuru sana nadhani nitaanza na hii ya tiba ila pa kupata hiyo shubiri ndo sijui..nitaulizia lakini ..natumai after two weeks nitakuwa nimepata nafuu.asante mpendwa
 
@sigma..thnx for the advise..i've not been injured, it just started on its own..yes am slim and my age ranges btn 30-33, and hospitals are the last thing i think about..whenever i go to the hosp i feel dizzy and faint so al end up being treated for what took me there and the fainting thingy.

@MAMMAMIA..nashukuru sana nadhani nitaanza na hii ya tiba ila pa kupata hiyo shubiri ndo sijui..nitaulizia lakini ..natumai after two weeks nitakuwa nimepata nafuu.asante mpendwa
Ikiwa unao mmea wa Alaoe Vera, kamua utomvi wake na changanya hayo mafuta.
 
Asante sana Mwanamageuko nitafwata maelekezo
maumivu yakizidi itabidi niende tu hospital
..nenda hospitali kabla maumivu hayajazidi Sweetdada, ukichelewa utalea ugonjwa na itakuchukua muda mrefu kupata tiba.
Tafadhali sana pata vipimo na ukilijua tatizo kama unaogopa dawa za hospitali tunaweza kuelekezana home remedy na tatizo litaisha natumai.
 
Kunywa alovela freedom ilinitibu mimi inafanya kazi 100 % nilikuwa na matatizo km yako nikapona ukitaka ntakuelekeza kwa kuipata
 
Si biashara ni kweli na utapata popote ulipo mi nipo mbeya safarini ukitaka upone niambie
 
sweetdada, inaelekea una matatizo ya arthritis -- rheumatoid arthritis, oesteoarthritis, au gouts. Ningekushauri kwanza uende hospitali ukaonane na mtaalamu (hapa nawekea msisitizo, mtaalamu) wa mifupa ili ujue km kweli una tatizo hilo au ni lingine tofauti. Km ni hayo niliyoyaorodhesha, usikimbilie kununua dawa; watakuandikia pain killers, ambazo ukitumia muda mrefu, zinaweza kukusababishia vidonda vya tumbo.

Lkn, kwa sasa, anza kutumia asali safi/halisi iliyochanganywa na mdalasini wa unga, kijiko 1 cha kulia; kutwa mara 2 au 3.

Utaijuaje asali halisi? Chovya njiti ya kiberiti (upande wa baruti) ktk asali. Iwache/Ishikilie kwa dk km 5, kisha iwashe; ikiwaka, asali uliyojaribia ni halisi, otherwise :A S-cry:
 
Back
Top Bottom