Tatizo la mwili kuwa wa baridi

Ganda Mweri

JF-Expert Member
Joined
Mar 8, 2018
Posts
303
Reaction score
887
Habari zenu wanajukwaa.

Mimi ni kijana wa kiume mwenye umri wa miaka 27, Kuna hii hali ambayo ninayo nahisi si ya kawaida nahitaji ushauri wenu.

Toka nipo shule ya msingi wenzangu walikua wakiniambia kuwa mimi ni wabaridi sana kuanzia mikononi na mwili kiujumla na kipindi cha mvua hawakutaka kabisa niwasogelee.

Hata nikishikana mkono na mtu lazima ataniuliza, we mbona wa baridi? Au mwingine ananiuliza ulikua umeshika maji?. Hata mpenzi wangu ambaye nipo naye huwa ananiambia sana kuhusu hii hali ya ubaridi niliyo nayo.

Je hii hali inasababishwa na nini? Na nifanye kitu gani kuondokana na hii hali? . Ahsanteni.
 


Siyo kweli labda haujajitambua tu, kwani mwili ukiwa wa baridi maana yake unaanza kufa, mtu anayeanza kufa mwili huwa baridi kidogo kidogo na mwishowe mwili mzima.

Hivyo siyo kweli kwamba una mwili baridi kwani hakuna binadamu aliye hai ambaye ana mwili baridi!
 
Mimi mwenyewe naona Niko kawaida, watu ninaokutana nao ndio huwa wananiambia.
 

Nenda hosipitali haraka
 
Pole sana... control ya mwili wa binadamu huanzia kwenye ubongo wake, ubongo wenye afya... una matatizo...

Na inaonekana utakua mwembamba sana kuliko kawaida...


Cc: mahondaw
 
Hili tatizo ni kweli lipo,mimi mwenyewe linanitokea mst of the time ninakua na mikono barid na mda mwingine inakua inatoka jasho,na mda mwingine wakati wa barid inakua vice versa mikono inakua warm .Nilijaribu kugoogle hili tatizo nimeona lipo na tiba pia ipo sema ni mpka ughaibuni huko..
 
Aisee. Kumbe tupo wengi.
 
Pole sana... control ya mwili wa binadamu huanzia kwenye ubongo wake, ubongo wenye afya... una matatizo...

Na inaonekana utakua mwembamba sana kuliko kawaida...


Cc: mahondaw
Ahsante. Ila Mimi sio mwembamba nipo kawaida.
 
Hiyo hali hata mimi ninayo,ila sijawahi kuichukulia kama tatizo,nipo poa kabisa
 
Pole sana mkuu sio dalili nzuri hizo...vipi hauoti babu zako wanakuita uwafate
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…