Tatizo la taa ya 'oil' kuwaka na kuzima

Mshasha wane

JF-Expert Member
Joined
Oct 16, 2014
Posts
234
Reaction score
633
Wakuu habari mimi ni mfuatiliaji mzuri sana wa hii forum ya magari japo siyo mchangiaji. Nna gari yangu Toyota Allex jana kuanzia juzi taa ya oil nyekundu kwenye dashboard imekuwa inawaka na kuzima.

Kuna muda nikiwasha gari taa zote za dashboard zinawaka ila yenyewe haiwaki inakuja kuwaka baadae nikiwa naendesha na inaweza kuwaka kwa kucheza cheza (ina blink).

Nimeenda kwa fundi wa kwanza akaniambia issue za shaft na akasema engine lazima ifumuliwe ninunue shaft nyingine. Wa pili akaniambia issue itakuwa oil pump. Naombeni msaada kwa wataalamu wa hivi vyombo maana mimi hii ndo gari yangu ya kwanza kutumia.

MREJESHO:
 
Kama oil umepima na iko level sawa inaweza kuwa oil sensor mbovu au loose connection.
Yes oil nimepima. Nilijaribu kufuatilia pia humu JF kuna uzi wa 2017 mtu alikuwa na shida kama yangu baadhi wakachangia kwa kusema oil pressure inaweza kuwa na shida pia
 
Taa ya oil kuwaka huweza kusababishwa na mambo mengi kama sample kua na ushafu mwingi hivo kupelekea uchafu kuziba kwenye chujio la oil na kufanya oil isiwe pumped ya kutosha, pia oil pump kupitisha uchafu ulio kwenye sample na mengine mengi Ukienda kufanya service fungua na sample wasafishe chujio, pia ukipima oil angalia viscosity yake sio lazima KM zifike ndio ubadilishe oil, oil inaweza kuchoka kabla ya KM zake kufika kutokana na mizunguko mingi ya gari.

Aina ya oil pia ulioweka inaeza kuchangia, kuna baadhi ya oil zinauzwa bei nafuu sana Kariakoo huaa gari taratibu (cheap is expensive) jaribu kusafisha na oil pump.
 
The worst thing ni kuendesha gari ikiwa imewasha hiyo taa.

Haikawii kukununulisha engine mpya.

But kwa lugha rahisi ni kwamba Oil pressure kwenye engine yako haipo sawa.

Inaweza kuwa iko juu sana au iko chini sana au Au oil pressure switch ina shida.

Ukipima expect code ranging from P0520 to p0524

Kama upo Dar nicheck 0621 221 606
 
Wakuu habari mimi ni mfuatiliaji mzuri sana wa hii forum ya magari japo siyo mchangiaji. Nna gari yangu Toyota Allex jana kuanzia juzi taa ya oil nyekundu kwenye dashboard imekuwa inawaka na kuzima...
Yaan hawa mafundi huwa wanakera sana, ukitaka kuona vituko vyako basi zunguka kwa mafundi tofauti kila mtu atapiga ramli zake. Na usipokuwa makini watakutia hasara ya maana, mimi gari yangu ya kwanza walininunulisha mpka gearbox alaf mwisho wa siku tatizo likawa control box.

Cha msingi peleka kwa mafundi wa kueleweka wafanye diagnosis kwa mashine ili ujue exactly shida iko wapi!
 
Unaweza ukapima ukaona Oil kwenye dipstick ipo chini kabisa ila hiyo taa isiwake.
If the oil light flickers on and off while the vehicle is stopped or at an idle, there may be a problem with the oil sensor or the pressure is too low. ... Check the oil level and add motor oil to the vehicle, if needed, and continue to monitor the light. If the oil was indeed low, the light should turn off.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…