Tatizo la tumbo kujaa gesi

Tatizo la tumbo kujaa gesi

Lafacha

Senior Member
Joined
Feb 3, 2017
Posts
195
Reaction score
275
Habari wana JamiiForums.

Nimekuja mbele yenu kuzungumza na wale wenye tatizo la tumbo kuunguruma, Mimi ni moja wenu na tatizo hili limenisumbua kwa muda sasa lakini hivi karibuni nimepata nafuu kwa kiasi kikubwa.

Mwanzo kabisa sikumbuki tatizo la tumbo kuunguruma lilinianzaje, sijui chanzo wala sababu isipokuwa baada ya muda kupita nikaja kufahamu baadhi ya vyakula nikila basi tumbo litaanza kuunguruma mwanzo mwisho mithili ya genereta iliyoishiwa mafuta.
1. Chai iliyochanganywa na tangawizi,
2. Chakula chenye viungo vingi,
3. Vitafunwa vya ngano,
4. Maziwa mgando kama ni machachu,
5. Maharage,
6. Kuchelewesha kula.


Basi, siku nikijichanganya nikala hiyo misosi apo juu, tumbo litasumbua balaa hata haja sipati vizuri (choo Napata cha mafungu mafungu kama mbuzi ).

Nilishawahi kuambiwa kuwa dalili ninazozipata ni dalili za kuwa na vidonda vya tumbo. Basi kama ni kweli ninachokitumia sasa iv kinaweza kuwa moja ya tiba nzuri ya vidonda vya tumbo.
1. Nimeacha kula misosi inayonisababishia tumbo kuunguruma,
2. Nimeacha kunywa vinywaji vyenye gesi,
3. Nimeacha kuchelewa kula , ratiba yangu ya jana inafanana na leo [ muda ni ule ule].

HITIMISHO: sijajua kama hiki ninachotumia kinaweza kikasaidia wengine wenye tatizo kama langu, ila napenda nawe ukajaribu kama itakusaidia utakuja HAPA KUTUPA MREJESHO, pia sijajua inaweza kuwa msaada kwa wenye stage zote za vidonda vya tumbo au kwa baadhi tu.

Jambo kubwa ninalolifanya mimi ni kuhakikisha kila siku kabla ya kula kitu chochote lazima ninywe class mbili za maji ya uvugu uvugu [umoto moto kama wa chai sema upoe kidogo tu sio sana].

Na muda wote ninao sikia kiu basi maji yangu ni ya uvugu vugu. Nina wiki moja tu toka nimeanza kutumia maji ya uvugu vugu na matokeo ni mazuri kwani siku nzima tumbo linaeza unguruma mara moja au mbili basi.

MAJI HAYA YAMEKUWA MSAADA MKUBWA KWANGU NAKUOMBEA KWA ALLAH NAWE YAKUSAIDIE .
 
🌳 VIDONDA VYA TUMBO NA TIBA YAKE🌳
⚡Mfumo wa mmeng'enyo wa chakula ni mfumo unaohusika na umeng'enyaji wa chakula mpaka kuwa katika hali inayoweza kusharabiwa na mwili.
⚡Sehemu kuu zinazohusika katika umeng'enyaji huo ni kinywa, umio 'Esophagus', mfuko wa tumbo 'Stomach', ini, mfuko wa nyongo, utumbo mwembamba 'Duedenum & Ileum', kongosho, utumbo mpana na puru 'Rectum'.
⚡Mfumo wa mmeng'enyo wa chakula hasa kuta za umio, tumbo na utumbo mwembamba hupata mmomonyoko ambao husababishwa na asidi inayotumika kumeng'enya chakula inaposhambulia kuta hizo. Kitaalamu hali hii hutambulika kama 'Peptic ulcers'.

stomach_ulcers
Vidonda vya mfumo wa umeng'anyaji chakula vikiwa kwenye tumbo tunaita vidonda vya tumbo 'Gastric ulcer', vikiwa katika duodenum tunaita 'Duodenal ulcer' na vikiwa katika esophagus tunaita 'Esophageal ulcer'
wa.me/255656303019

☘SABABU ZA VIDONDA VYA TUMBO☘
👉Bakteria aina ya Helicobacter pylori 'H.pylori' & Non-Steroidal Anti Inflammatory Drugs 'NSAIDs' ndio visababishi vikuu.
👉Bakteria H.pylori wanahusika sana kwa angalau nne ya tano ya vidonda vya tumbo 'Gastric ulcers' & 95% ya 'Duodenal ulcers' ambapo NSAIDs husababisha 20% ya 'Gastric ulcers' na 5% ya 'Duodenal ulcers'
👉Bakteria H.pylori husababisha kupitia vyakula na maji. Pia hupatikana kwenye mate ya binadamu hivyo inaweza kusambazwa mdomo kwa mdomo wakati mkila denda/kunyonyana midomo.
👉Bakteria H.pylori huishi kwenye kuta za utumbo na hutengeneza vimeng'enya 'Enzyme' iitwayo 'Urease' inayopunguza athari za asidi kwenye utumbo.
👉Utumbo hutaka kufidia kiasi cha asidi kinachopotea kwa kutengeneza zaidi na husababisha kukwangua kuta za utumbo.
👉Non-Steroidal Anti Inflammantory Drugs 'NSAIDs' ni dawa za kutuliza maumivu ya kichwa, maumivu ya hedhi, kushusha homa na kuondoa maumivu madogo madogo mfano Aspirin, Ibuprofen,Diclofenac & Meloxicam. Dawa hizi hupunguza uwezo wa kuta za tumbo na kufanya uwe rahisi kushambuliwa na asidi za tumboni hivyo kusababisha vidonda.
👉Chembe za urithi 'Genetics': Idadi kubwa ya watu wenye vidonda vya tumbo wana ndugu wa karibu wenye vidonda pia, hii huwafanya wataalamu kufikiria kuwa chembe za urithi zinahusika pia.
👉Uvutaji sigara/tumbaku: Wavutaji wa sigara wako katika hatari ya kupata vidonda vya tumbo ikilinganishwa na wasiovuta.
👉Matumizi ya pombe/vilevi: Walevi wako katika hatari zaidi ya kupata vidonda vya tumbo ikilinganishwa na wasiotumia vileo/pombe.
👉Msongo wa mawazo 'Mental stress': Msongo wa mawazo hausababishi vidonda moja kwa moja ila hufanya hali kuwa mbaya zaidi kwa wagonjwa.

🌿DALILI ZA VIDONDA VYA TUMBO🌿
⚡ Maumivu ya tumbo na huwa makali zaidi pale asidi inapopita juu ya vidonda.
...Maumivu yanaweza anzia kwenye kitovu na kupanda juu hadi katikati ya kifua 'Epigastric pain'
...Maumivu yanaweza kuongezeka unapokuwa njaa. Pia yanaweza kuwa makali wakati wa usiku kwenye mida ya kulala, yanayoweza kupunguzwa kwa kula chakula kidogo.
⚡ Kushindwa kumeza vizuri chakula.
⚡ Chakula kukwama kama kinataka kurudi mdomoni.
⚡ Kujisikia vibaya baada ya kula.
⚡ Kupungua uzito.
⚡ Kukosa hamu ya kula.

🌴DALILI HATARI🌴
⚡Kutapika damu.
⚡ Kupata choo kikubwa cheusi au chenye damu nzito.
⚡ Kichefuchefu & kutapika.

JINSI VIDONDA HUGUNDULIWA:-

Maelezo ya mgonjwa juu ya dalili alizonazo humsaidia daktari kuhisi kinachomsumbua mteja wake ni vidonda vya tumbo.

Ili kuthibitisha vidonda vipimo vifuatavyo hufanyika :-

Kupima damu 'Blood test'

Kuangalia bakteria aina ya H.pylori na kama mgonjwa amekuwa akitumia antibayotiki au dawa za vidonda Proton Pump Inhibitors 'PPIs' mfano Omeprazole vipimo vyake vya damu vitaonyesha majibu hasi 'Negative'

Kupima pumzi 'Breath test'

Mgonjwa hupewa anywe maji yenye atomi za kaboni zinazoweza kuvunjika, hii hufanya bakteria H.pylori kuvunjika na baada ya lisaa mgonjwa hutoa pumzi kwenye chombo kilichofunikwa kama mgonjwa ameambukizwa sampuli ya pumzi itaonyesha vipande vya kaboni kwenye kabonidioksaidi.

Kupima antijeni kwenye kinyesi 'Stool antigen test'

Kipimo hiki huangalia kama kuna bakteria H.pylori kwenye kinyesi. Vilevule kipimo hiki hutumika kuangalia ufanisi wa matibabu yaliyotolewa dhidi ya bakteria.

X-ray ya sehemu ya juu ya tumbo 'Upper gastrointestinal x-ray'

Picha huonyesha umio 'Esophagus', mfuko wa tumbo 'Stomach' na Dudenum. Mgonjwa humeza maji yenye 'Barium' ambayo hufanya vidonda kuonekana kirahisi kwa x-ray.

Kamera ya tumbo 'Endoscopy'. Mrija mrefu wenye kamera huingia tumboni na daktari huona vidonda kwenye skrini ya kompyuta 'Monitor'.

⚡MATIBABU YA VIDONDA VYA TUMBO⚡
Kama vidonda vitakuwa vimesababishwa na bakteria H.pylori dawa za kuua na kuondoa bakteria hutumiwa.

Kama vidonda vya tumbo vitakuwa vimesababishwa na 'NSAIDs' na hana maambukizi ya bakteria H.pylori atapaswa kutumia dawa Proton Pump Inhibitors 'PPIs'

Proton Pump Inhibitors 'PPIs' hufanya kazi kwa kuvunja/kuzuia kazi ya protini ziitwazo 'Proton Pump' ambazo huhusika katika utengenezaji wa asidi tumboni.

Matumizi ya NSAIDs kwa ajili ya kuondoa homa na maumivu yatalithiwa na dawa kama Paracetamol.

Matibabu yaliyozungumziwa hapo juu yanaweza kuchukua muda kabla ya kuanza kufanya kazi hivyo daktari anaweza kuongeza matibabu mengine kama vizuia asidi 'Antiacids' & 'Alginates' kwa ajili ya nafuu ya haraka.

Usitumie dawa hizi ndani ya lisaa moja baada ya kunywa PPIs mfano Omeprazole au H2-Receptor Antagonists mfano Cimetidine.

⚡⚡Matibabu kwa njia za asili, zipo dawa mbali mbali unazoweza tumia zikiwa kwenye mfumo wa unga au kimiminika

Kwa ushauri na tiba kwa maradhi mbali mbali wasiliana nasi.
what's app /call
wa.me/255656303019
~CHIEF SANG'IDA
 
Back
Top Bottom