Tatizo la upele Kidevuni: Chanzo na matibabu yake

Omumura

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2009
Posts
476
Reaction score
18


BAADHI YA MASWALI YALIYOULIZWA KUHUSUNSHIDA HII
Jamani wana JF naombeni msaada wa ushauri wenu kwani kwa muda mrefu sasa ninasumbuliwa na tatizo la kutoka mapele ya ndevu mara baada ya kunyoa, nimejaribu aftershave nyingi tu lakini naona bado hazijanikubali.

Kwa sasa hivi nilikuwa natumia aftershave iitwayo Bump Patrol!
---
---
---

UFAFANUZI WA JUMLA WA TATIZO HILI
Kwa wastani binadamu anatumia miezi (5) mitano ya maisha yake kunyoa na ndani ya miezi hiyo mitano kwa mwanaume atashave mara elfu 20,000 katika muda wa maisha yake yote. Baadhi ya watu huchukia kabisa ikifika kipindi cha kushave kutokana na changamoto wanazozipata wakati na baada ya kushave. Kushave kuna changamoto nyingi, haijalishi ni unashave ndevu (mwanaume), sehemu za kwapa au sehemu nyeti.

Changamoto hizo zinaweza kuwa

1. Kupata vipele baada ya kunyoa hasa kwenye maeneo yanayozunguka kidevu, kwapani na weusi.

2. Ngozi kuwasha, kutokana na ukavu unaosababishwa na spirit au bidhaa yenye alcohol inayopakwa kweny ngozi.

3. Kupata weusi baada ya michubuko na vipele baada ya kunyoa kupona vinaacha weusi sehemu husika.


Changamoto hizi zinachangiwa zaidi na bidhaa na vifaa tunavyotumia kunyolea. Sio wote wanapata vipele na weusi, ila kwa wale wenye vipele na weusi kwenye maeneo wanayoshave, hiyo inachangiwa na vitu vifuatavyo:

1.kushave bila kulainisha ngozi

2.Kupaka spirit au aftershave yenye alcohol baada ya kushave

3.kutokupaka kitu chochote baada ya kushave

4.kutumia blade ama kiwembe kisicho na makali.

Ufanye nini ili usipate vipele na uondoe weusi?

1. Lainisha ngozi kabla ya kunyoa

Ni muhimu kulainisha ngozi yako kabla ya kunyoa kwa, layer ya juu ya ngozi ina chembe hai zilizokufa, ukilainisha ngozi kabla ya kunyoa itasaidia kuondoa na chembe hai zilizokufa wakati wa kunyoa, pia itasaidia wembe kuteleza vizuri kwenye ngozi bila kusababisha michubuko.

2. Tumia aftershave baada ya kunyoa.

unatakiwa kutumia aftershave ili kupoza ngozi, kuipa unyevu nyevu na kufanya nyororo. Spirit na aftershave zenye alcohol zinafanya ngozi kuwa kavu, itasababisha miwasho na ukijikuna ndo inapelekea kutoka vipele.

3. Nyoa kufatisha muelekeo wa nywele zilivyoota.
Hii itasaidia ngozi isiume zaidi wakati wa kunyoa. Pia hakikisha kiwembe au blade unayotumia kunyolea ni kikali, kikiwa butu Utarudi mara nyingi na kuumiza zaidi ngozi.

4. Usitumie deodorant yenye chumvi ya aluminum na alcohol.
Chumvi ya aluminum na alcohol inachangia kufanya ngozi iwe kavu na kuwasha baada ya kunyoa ambayo itapelekea kupata weusi wa kwapa.

Credit: Aloe life style
MAONI NA MAJIBU YALIYOTOLEWA NA BAADHI YA WADAU:
---
---
---
---
---
---
---
 
ni tatizo letu sote ila lina tatulika mkuu kabisa mkuu uwa na2mia poda fulani ina dawa napewaga na mnigeria ipo safi cku izi ata c2mii cana kama vp nipm 2saidiane mkuu
 
Mmmh jamani huu ndo ugonjwa wangu mkuu, NIMEMALIZA dawa zote, kilichonisaidia kidogo nilinunua mashine kama ya saluni nimeitumia, ikaibwa mota, nikanunua nyingine elfu sabini, juzi mtoto kaiangusha imeharibika, nimenunua bump patrol, mmh maendeleo madogo! sasa nanyoa daily kisha ndo napaka hio bump control! pls nisaidieni pia
 
Bump Patrol za sasa hivi nahisi zinachakachuliwa. Mwanzoni wakati zinaingia zilikuwa effective sana lakini haya matoleo ya sasa ni kama spirit tu ya kawaida!
 
Poleni sana wanyoa ndevu wenzangu. Mimi nilikuwa natatozo hilo lakini niliamua achana na viwembe vya kunyolea including gillete wanavyo sema ni nzuri, kwa sasa natumia mashine ya kunyolea, kwa sasa tatizo hilo limekwisha kabisa. nikitumia mashine sipati kipele hata kimoja.
 
wazee hili ni janga la kitaifa . embu tusaidiane kuambiana tutumie kitu gani ili tuondokane na huu usumbufu wa vipele vya ndevu.
 
tupo wengi mkuu
mwenye kujua atujulishe ila mimi huwa situmii gillete..natumia shaving mashine...nikikusa gilette tu nimekwisha
Nilikuwa mtumiaji mkuu wa aftershave nikidhani zinaondoa vipele, wife alinishauri niache hata kwa miezi miwili nione. Vipele vikaisha.

Mara nyingi ninanyoa saloon kwa magic na napata scrubbing na sipaki after shave kabisa na ninaponyoa kwa gillete ni lazime iwe na makali, isiwe butu maana ikiwa butu lazima vipele vinatoka, na kabla ya kunyoa ninanawa maji ya moto au vuguvugu kidogo na kupaka sabuni ya kuogea. nikimaliza sipaki aftershave kabisa.

Sina kipele hata kimoja, I have a very good baby face.
 
Isisahaulike option ya kutokutumia wembe au mashine kabisa. Sio lazima uwe Osama - unaweza kupunguza kwa mkasi.
 
ukinawa kwa maji moto baada ya kunyoa inasaidia sana, wembe noma tumieni mashine tu
 
Mkuu unatumia wembe? kama unatumia wembe acha tumia mashine kama wanazotumia vinyozi. baada hapo pakaza B&C SKIN TIGHT ni kiboko hii kesho yake tu ukiamka utaona tofauti.endelea siku mbili tatu vitapotea kabisa acha kutumia siku ukikata ndevu tena pakaza kidogo hivyo hivyo na utaona tofauti yake.
 
Tatizo langu mimi ni kwamba nikiacha ndevu ndo vipele vinakuja na ndevu zinaanza kuniwasha, zingekuwa haziwashi ningekuwa napunguza tu kwa mkasi. So tatizo nini hapa?
 
Dawa ya kuondokana na Vipele vya ndevu ni ndogo sana.

Endapo unatumia wembe iwe gelete au aina yoyoyote ya wembe ikiwa ni pamoja na magic shave acha mara moja.

Wembe hukwangua ndevu mpaka mwisho na hivyo kufanya ile ncha ya ndevu kuwa kali sana wakati inapoanza kuota tena. Hi hufanya ngozi kuvimba kwa sababu ule mzizi wa ndevu huichoma ngozi ili ndevu iweze kutoka na hivo kuifanya ngozi kuvimba na ndio hicho mnachokiona ni vipele. Hivyo vipele ni matokeo ya ndevu kusukuma ngozi ili iweze kujitokeza nje hivyo kuifanya ngozi kuvimba. matatizo haya huwakuta sana waafrika kwa sababu nywele za kaifrika ni ngumu na huwa na ncha kali kutokana na asili ya nywele zatu na hivo kusababisha kuichoma ngozi wa nguvu sana.

SULUHISHO
Ukitaka kuondokana na vipele hivi, unachotakiwa kufanya ni kuachana na kutumia wembe. Tumia mashine ya kunyolea ndevu kwani mashine kwa bahati nzuri huwa hauwezi kukwangua na kumaliza nywele zote kama ilivyo wembe.
 
Kuna hii inaitwa Calmurid cream, sina uhakika na availability yake hapo bongo lakini is effective na resuls is just in a day or two, lakini unatakiwa kuendelea kuitumia kama utaendelea kunyolea wembe!
 
Salaama ndugu zangu

Ni kweli kwamba vipele vya ndevu ni tatizo kubwa kwa watu wengi. Tatizo hilo linasababishwa na hair ingrowth zinapoanza kurefuka baada ya kunyolewa au skin inflammation associated with pus forming bacterial infection. Tatizo la hair ingrowth linawasumbua wale ambao ndevu zao ni curled yaani badala ya kurefuka away from the skin zenyewe zinachomoza kidogo kwenye ngozi then zinaota kuelekea ndani ya ngozi.

Kwahiyo ile sehemu ambayo nywele inaingia inavimba amabapo inaonekana kipele. Ukiwa makini siku 3 baada ya kunyoa jichunguze vizuri kwa kutumia kioo utaweza kuona nywele nyingi zipo ndani ya ngozi na kupata muwasho amabao unasababishwa na irritation ya hizo nywele kwenye ngozi. Watu wengine wanatumia kitu chenye ncha kali na kuzichomoa hizo nywele then vipele vinapungua.

Pia utaweza kuona vipele amavyo vimepata infection na kutoa usaha. Kwahiyo kujikinga na tatizo la hair ingrowth ni kwamba usiruhusu nywele kuota na kufanya U- turn na kurudi kwenye ngozi. Ukiwa mtumiaji wa mashine ya kunyolea na haupendi kuwa na ndevu inakubidi unyoe kila siku lakini wengi wao wanasumbuliwa na ngozi kuvimba na kupata bacterial infection ambapo utapata maumivu ya ngozi! Otherwise tumia mashine ambayo itazibakiza bila kuzikata hadi level ya ngozi ambapo hautopata tatizo la hair ingrowth na vipele havitakusumbua.

Pia unaweza tumia shaving creams au powder mfano magic ambayo nami naitumia bila kupata madhala ya kutokwa na mapele. Unapotumia powder au cream hakikisha hauruhusu ndevu kuota. Huo ni ushauri wangu kwa leo
 
Nilikuwa mhanga pia, ila kwa sasa natumia gillette disposable na shaving cream ya gillette, also nivea shaving cream can do. Situmii after shave! Softiii!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…