Tatizo la waamuzi kwenye ligi kuu

changaule

JF-Expert Member
Joined
Jan 10, 2020
Posts
6,039
Reaction score
10,151
Jana watu wengi walishangazwa na maamuzi ya refarii kuipa Yanga penati iliyo nyepesi nakupelekea kuonekana Yanga imebebwa ili wasazishe. Jana washabiki wa Simba walipovuka sana tukio hilo lakini leo wamesahau ya wenzio na wao refarii kawapa fadhira ya kubebwa pia. Yaani kila nikijaribu kurudia rudia nione kosa iliyopelekea Simba kupewa penati nashindwa kuelewa kabisa maana mchezaji wa Ruvu kaupiga mpira.

Penati ya Yanga ilikuwa ni aibu sana lakini hii ya Simba ni aibu mara ya mia ya penati ya Jana ya Yanga. Naona halizungumziwi hii penati kwavile tu Simba hawakufunga. Ila haikuwa penati pale mbeleko ya chuma imetumika
 
Simba na Yanga zinaua soka la bongo
 
Mimi ndio maana siangaliagi mipira ya bongo pathetic
 
Mbali na penalty waliyopewa Simba, mchezaji Ruvu Shooting alitakiwa kupewa na kadi ya njano Kwa kucheza mchezo hatarishi wa kuinua ndaluga lake juu ya usawa wa goti.

Penalty ya Yanga mchezaji yule mwenye uzoefu alijidondosha tu na kum-fool muamuzi. Hakukuwa na excess force ya kumdondosha.
 
Yanga wanataka kulinganisha penati yao ya jana na ya leo ya Simba lakini ya jana ilikuwa siyo penati huku ya leo ilikuwa penati ya wazi
 
Hata Morrison alistahili direct red card.
 
Hata Morrison alistahili direct red card.
Usimsahau aliyemkanyaga Morrison kwani yeye alistahili kadi ya njano na aliyempiga ngumi Boko akaenda chini wakati yeye alikuwa anaamua tu ugomvi naye alistahili kadi nyekundu. Mwisho wa siku kama hatua zitachukuliwa ni hao hao Ruvu Shooting ndio watakao adhibiwa zaidi Kwa sababu chanzo cha vurugu ni wao wenyewe na mpira gwaride walicheza wao.
 
Nimeona viandishi uchwara vimebeba bango kuhusu morison ila wachezaji wa jkt ruvu waliofanya fujo wamewaacha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…