Habari wanamichezo!
Tangu kujiuzulu kwa Manji kwenye timu ya Yanga, sauti ya mamlaka ya kiuongozi imepotea! Huo ndo ukweli hata ukibisha.
Tatizo la Mzee Sanga ni kupenda madaraka ambayo pia hajui atayapataje, yupo yupo tu kifupi hajielewi. Kajaribu kuwajaza watendaji wa upande wake lakini nao ni tatizo yaani mizigo.
Yanga chini ya Clement Sanga imekuwa Yanga ya malalamiko na kibaya zaidi tumeaminishwa kuwa timu haina pesa mpaka wengine tumechangia. Lakini timu ina udhamini kutoka
1. Vodacom
2. Maji ya Afya
3. Yanga TV kupitia Azam TV
4. Sportpesa.
5. Gate collection n.k.
Cha ajabu mishahara inacheleweshwa, wachezaji hawaambiwi sababu na kama kuna upungufu ni wa kiasi gani wanachama hatujui. Ni ngojera kila uchao.
Mzee huyu ameshindwa hata kuitisha mkutano wa wanachama ili nafasi hiyo izibwe, sasa katuwekea Katibu ambae anatamani kuwa Kocha, very selfish! Sasa amemleta msemaji ambae ameshindwa kuisemea brand ya timu yetu. Umaarufu wa timu unashuka, si bora Jerry Muro pamoja na mapungufu kadhaa ila alisaidia kuimarisha brand ya club yetu.
Ndugu Dismas Ten, hata huko alikotokea hakuwa jina lenye ushawishi, sijui ni ndugu wa Mzee Sanga?!
Nasikia eti Mzee wa saba anaitaka timu. Sawa lakini asifikirie Yanga ni kama Taifa Stars, watu watamfanyia vurugu kama Nchunga. Naskia umeitwa mkutano mwezi Mei, lengo ni kubadili Muundo wa uendeshaji. Nashauri sambamba na hilo uongozi chini ya Sanga utupishe tujaribu akili mpya. Hata huyo atakaenunua hisa namuonea huruma, atapata hasara isiyomithilika.
Tunataka akili mpya na siendi uwanjani tena mpaka haya majinamizi yapishe.
Tangu kujiuzulu kwa Manji kwenye timu ya Yanga, sauti ya mamlaka ya kiuongozi imepotea! Huo ndo ukweli hata ukibisha.
Tatizo la Mzee Sanga ni kupenda madaraka ambayo pia hajui atayapataje, yupo yupo tu kifupi hajielewi. Kajaribu kuwajaza watendaji wa upande wake lakini nao ni tatizo yaani mizigo.
Yanga chini ya Clement Sanga imekuwa Yanga ya malalamiko na kibaya zaidi tumeaminishwa kuwa timu haina pesa mpaka wengine tumechangia. Lakini timu ina udhamini kutoka
1. Vodacom
2. Maji ya Afya
3. Yanga TV kupitia Azam TV
4. Sportpesa.
5. Gate collection n.k.
Cha ajabu mishahara inacheleweshwa, wachezaji hawaambiwi sababu na kama kuna upungufu ni wa kiasi gani wanachama hatujui. Ni ngojera kila uchao.
Mzee huyu ameshindwa hata kuitisha mkutano wa wanachama ili nafasi hiyo izibwe, sasa katuwekea Katibu ambae anatamani kuwa Kocha, very selfish! Sasa amemleta msemaji ambae ameshindwa kuisemea brand ya timu yetu. Umaarufu wa timu unashuka, si bora Jerry Muro pamoja na mapungufu kadhaa ila alisaidia kuimarisha brand ya club yetu.
Ndugu Dismas Ten, hata huko alikotokea hakuwa jina lenye ushawishi, sijui ni ndugu wa Mzee Sanga?!
Nasikia eti Mzee wa saba anaitaka timu. Sawa lakini asifikirie Yanga ni kama Taifa Stars, watu watamfanyia vurugu kama Nchunga. Naskia umeitwa mkutano mwezi Mei, lengo ni kubadili Muundo wa uendeshaji. Nashauri sambamba na hilo uongozi chini ya Sanga utupishe tujaribu akili mpya. Hata huyo atakaenunua hisa namuonea huruma, atapata hasara isiyomithilika.
Tunataka akili mpya na siendi uwanjani tena mpaka haya majinamizi yapishe.