Tatizo namba moja la Yanga ni Clement Sanga

Tatizo namba moja la Yanga ni Clement Sanga

Way forward ni kubadili mfumo wa uendeshaji.... Hizo nyingine ni blah blah. Mfumo wa unachama kushika timu ni pasua kichwa.
Ahaa! Ndala Sports, mmeaanza kuweweseka? Tarehe 29 kichapo chenu kipo palepale! Na Ubingwa mtausikia kunako mwaka huu. Mleteni sasa Mzee Akilimali, khee! kheeee! kheeeeeeeeeeee!
 
Pia Madrid inamfumo wa wanachama na Arsenal ina mfumo wa hisa. Tatizo la club zetu ni viongozi halafu mifumo ndo inafuatia
Mfumo mbovu ndio Huleta viongozi wabovu. Usitegemee kupata viongozi katika mfumo mbovu ulioanzishwa na wanachama wanaoitegemea timu badala ya kinyume CHAKE.

Mfano wa arsenal sijauelewa, ila kama unamaanisha kwamba japo wao wanafuata mfumo wa hisa lakini ni wabovu hapo utakuwa umekosea. Wameshafika UEFA CHAMPIONS LEAGUE FINAL, wamefika nusu fainali mara kadhaa, sasa hivi wapo EUROPA NUSU FAINALI. Wamedumu kwenye ushindani na timu imara, bora na zenye mifumo mizuri kwa miaka Mingi tu.

Real Madrid ipo chini ya wanachama lakini structure yao unaifahamu. Kuna Wanachama, body of directors, rais. Uongozi wao upo very well organized (wanamfumo mzuri). Lakini kikubwa kuliko vyote, ni timu yao inaendeshwa kibiashara sio kama Yanga.
 
Mfumo mbovu ndio Huleta viongozi wabovu. Usitegemee kupata viongozi katika mfumo mbovu ulioanzishwa na wanachama wanaoitegemea timu badala ya kinyume CHAKE.

Mfano wa arsenal sijauelewa, ila kama unamaanisha kwamba japo wao wanafuata mfumo wa hisa lakini ni wabovu hapo utakuwa umekosea. Wameshafika UEFA CHAMPIONS LEAGUE FINAL, wamefika nusu fainali mara kadhaa, sasa hivi wapo EUROPA NUSU FAINALI. Wamedumu kwenye ushindani na timu imara, bora na zenye mifumo mizuri kwa miaka Mingi tu.

Real Madrid ipo chini ya wanachama lakini structure yao unaifahamu. Kuna Wanachama, body of directors, rais. Uongozi wao upo very well organized (wanamfumo mzuri). Lakini kikubwa kuliko vyote, ni timu yao inaendeshwa kibiashara sio kama Yanga.
Naunga mkono hoja, mabadiliko ni lazima
 
Ahaa! Ndala Sports, mmeaanza kuweweseka? Tarehe 29 kichapo chenu kipo palepale! Na Ubingwa mtausikia kunako mwaka huu. Mleteni sasa Mzee Akilimali, khee! kheeee! kheeeeeeeeeeee!
Mzee akilimali hajawahi kuwa mchezaji pale ni mwanachama kama wengine. Kutufunga hakuwafanyi muwe timu kubwa na yenye a fan base kubwa nchini. Tahadhari msing'oe viti maana huwa mnaingia mkiwa na matarajio makubwa.
 
Eti sasa Lwandamina anatongozwa aende ethiopia
 
Habari wanamichezo!
Tangu kujiuzulu kwa Manji timu sauti ya mamlaka ya kiungozi imepotea!Huo ndo ukweli hata ukibisha. Tatizo la Mzee Sanga nikupenda madaraka ambayo pia hajui atayapataje,yupo yupo tu ,kifupi hajielewi.
Kajaribu kuwajaza watendaji wa upande wake ,lakini nao ni tatizo yaani mizigo .Yanga chini ya Clement Sanga imekuwa yanga ya malalamiko, na kibaya zaidi tumeaminishwa kuwa timu haina pesa ,mpaka wengine tumechangia. Timu ina udhamini:
Vodacom
Maji ya Afya
Yanga tv kupitia azam TV
Sportpesa.
Gate collection n.k.
Cha ajabu mishahara inacheleweshwa ,wachezaji hawaambiwi sababu, kama kuna upungufu ni wa kiasi gani wanachama hatujui. Ni ngojera kila uchao.
Mzee huyu ameshindwa hata kuitisha mkutano wa wanachama ili nafas hiyo izibwe,sasa katuwekea Katibu ambae anaetamani kuwa Kocha,very selfish, sasa amemleta msemaji ambae ameshindwa kuisemea brand ya timu yetu. Umaarufu wa timu unashuka ,si bora Jerry Muro pamoja na mapungufu kadhaa ila alisaidia kuimarisha brand ya club yetu.
Ndugu Dismas ten ,hata huko alikotokea hakuwa jina lenye ushawishi,sijui ni ndugu wa Mzee Sanga.
Nasikia eti Mzee wa saba anaitaka timu ,sawa. Asifikirie yanga nikama taifa stars ,watu watamfanyia vurugu kama Nchunga.
Naskia umeitwa mkutano mwezi Mei, lengo ni kubadili Muundo wa wendeshaji, sambamba na hilo . Uongozi chini ya Sanga utupishe tujaribu akili mpya , hata huyo atakaenunua hisa namuonea huruma,Atapata hasara isiyo mithilika. Tunataka akili mpya .Na siendi uwanjani tena. Mpaka hata majinamizi yapishe.


Mzee wa saba???!! Ni nani huyu?? dah
 
Huyu ana nunua mechi.

The end justifies the means...hehehehehhehehe....Inawezekana kweli ananunua lakini tatizo la Yanga ni kushindwa kupanga mikakati ya ushindi...Mechi inachezwa kesho, eti watu ndiyo wanaanza kuhangaika...huu ni upuuzi... mpira hauchezwi mdomoni...Mpira unachezwa kwa mipango...na watu wa mipango ndani ya Yanga wapo tena wengi, na wala hawataki sifa, wala kuongea ongea kwenye media...ila watu hao, hawashirikishwi kwenye mipango, wamewekwa kando, na wameamua kubaki kando, hawataki kelele...kiongozi baadala ya kusema YANGA imesajili, anabwabwaja hovyo kwenye media na kusema 'MIMI nimesajili'...yaani anataka sifa...hovyo kabisa...very selfish...Yanga ina pesa na pesa hizo ziko kwa wanayanga...lakini pia ushindi siyo lazima pesa, ingawa pesa ni muhimu pia...ushindi ni mipango mizuri na kuwashirikisha watu makini...Timu ya Yanga ni nzuri ila naona lipo tatizo la mipango mibovu...Yaani viongozi wanalalamika zaidi kuliko kutenda...Uongozi ni mipango mizuri, kujituma, uaminifu, mapenzi kwa timu, PR, kujitoa mhanga, kuwa na majibu mazuri kwa wachezaji lakini wakati huo huo kuwa mkali kwa watovu wa nidhamu...
 
Lakini tutawakamata Simba tu huko juu. Huwa wanatangulia hadi pointi nane lakini tunawashika! Hata mwaka huu tutawapita tuu kama kawaida
 
1954 huo ndo ukweli timu za mjini zinaendeshwa kimjini kimjini,Katibu Mkuu mlalamikaji hatufai, badala ya kuitisha vikao anakuja kwenye media kusema yanga ipo hali mbaya ,sjui kasomea wapi yule. Kusema vile kunashusha morali na brand ya timu. Hawa watu yaani ;Sanga,Mkwasa, Dismas Ten,na Nsajigwa ,wanachokisubiri watakiona.
 
Timu kesho inacheza ikiwa na Kocha wa muda
 
Clement Sanga hakuwa tatizo hadi Yanga imefuzu hatua ya makundi kombe la CAF.
Sasa akina Mzee Akilinyingi wataibuka kutaka mkutano kuchagua viongozi wapya.
 
Clement Sanga hakuwa tatizo hadi Yanga imefuzu hatua ya makundi kombe la CAF.
Sasa akina Mzee Akilinyingi wataibuka kutaka mkutano kuchagua viongozi wapya.
Utakuwa hujielewi wew, au nyie ndo mnanufaika. Makundi hiyo hatua Sanga ndo kawesha kwa namna gan?Halafu Mzee Akilimali sio sehem ya post hii kama unamwashwa mtafute kivyako.
 
Utakuwa hujielewi wew, au nyie ndo mnanufaika. Makundi hiyo hatua Sanga ndo kawesha kwa namna gan?Halafu Mzee Akilimali sio sehem ya post hii kama unamwashwa mtafute kivyako.
Akilinyingi mumeo? Mtafute
 
Mungu tuepushe na fedheha ya leo, huu ujinga ambao uongozi unachotufanyia ipo siku tu.
 
Mfumo mbovu ndio Huleta viongozi wabovu. Usitegemee kupata viongozi katika mfumo mbovu ulioanzishwa na wanachama wanaoitegemea timu badala ya kinyume CHAKE.

Mfano wa arsenal sijauelewa, ila kama unamaanisha kwamba japo wao wanafuata mfumo wa hisa lakini ni wabovu hapo utakuwa umekosea. Wameshafika UEFA CHAMPIONS LEAGUE FINAL, wamefika nusu fainali mara kadhaa, sasa hivi wapo EUROPA NUSU FAINALI. Wamedumu kwenye ushindani na timu imara, bora na zenye mifumo mizuri kwa miaka Mingi tu.

Real Madrid ipo chini ya wanachama lakini structure yao unaifahamu. Kuna Wanachama, body of directors, rais. Uongozi wao upo very well organized (wanamfumo mzuri). Lakini kikubwa kuliko vyote, ni timu yao inaendeshwa kibiashara sio kama Yanga.
Now what do you say, maana sasa kombe tumeshakosa
 
Back
Top Bottom