Tatizo ni bodi ya mikopo au vyuo?

Tatizo ni bodi ya mikopo au vyuo?

DOTTO MUNGO

Member
Joined
Mar 11, 2012
Posts
15
Reaction score
1
Inasikitisha kuona kuwa tunaanza semista ya pili wiki ya pili sasa (udom) bila kuwa na chochote katika akaunti zetu kwa wale tunaoitegemea serikali kupitia bodi ya mikopo ya elimu ya juu (HESLB). Wanachuo wengi wanageuka kuwa ombaomba kwa ndugu, jamaa na marafiki huku idadi kubwa ikihaha kupata walau mikopo kutoka sehemu yoyote ili kuendelea na masomo wakati wakisubiri bodi kuwajaza mikwanja kwenye akaunti zao. Tatizo ni nini jamani?
 
Tatizo nini? fuatilia na uchukue hatua woga wenu hautawasaidia
 
Tatizo ni bodi ya mikopo inayoendesha shughuri zake kama kikosi cha kufyatua mizinga. no utaratibu. kila mmoja pale bodi anajoina bosi,kila mmoja anatoa utaratibu wake. mimi wamezilamba hela zangu za research nawavutia muda nimfikishe executive director mahakamani. dai haki yako usiombe, sijasema muandamane, wa taarifa za kiintellejensia watawa-songea
 
UDOM UdOm Udom udom mtaendelea kudanganywa na hayo majengo mpaka mwisho wa dunia, nasikia mkiwa kwenye hayo majengo mnacheka-cheka tuu, daini boom lenu, someni kwa bidii wadogo zangu.
 
Pouwa bana, lakini ni ngumu kwa sasa kudai haki kwani hatuna uongozi wa kutetea madent bali ........@Ghani
 
mpaka uchaguzi Arumeru uishe ndo mtapewa hilo 'bomu' lenu
 
komaen achen uwoga,mbona sua huwa hawaandaman lakin pesa yao inaingia mapema
 
Back
Top Bottom