Tatizo ni Diamond mwenyewe, si Nyange wala mama Dangote

Sasa, una hakika gani kuwa Diamond alipenda kubaki kuwa mtoto wa Abdul? Pia unadhani shinikizo ni huyo Diamond au hali halisi? Huwezi kumhukumu kijana wa watu kwa makosa ya wazazi wao.
 
Wanaweza kwenye dna, na wakatoa Ela kwa mkono wa nyuma, kumkana baba, huyo hawamtaki toka alivyopata mafanikio mtoto, baba hasipate chochote, kwakuwa hakumtunza na aliwatelekeza akiwa form one.
Lakini ukweli watakuwa wameufahamu, hata wakimkana!

Hizi drama za mitandao ni publicity stunts tu hizi.. Sehemu ya kupata ukweli wanaifahamu ila wapo bize kula publicity, lakini ndo vizuri.

Sababu hata mie kama ningekuwa Meneja wa Msanii yeyote yule basi tungekuwa tunapiga Kazi sambamba na kufyatua ma-KICK mengi, tunawapa wananchi umbea, watu wapige UMBEA halafu tunapiga PESA.

Ukizidi kuongelewa ndivyo unavyozidi kuwa ON TOP OF THE GAME, na ukizidi kuwa Top ndivyo watu wanazidi kuwa na Hamu na wewe, strategically unakula Pesa. (Kazi kwa sana + Publicity Stunt kwa sana)

ENTERTAINMENT INDUSTRY haitaki mtu wa upole upole, uzubae zubae au kuwa very innocent, inataka AMSHA AMSHA! Makeke makeke!
 
Ni wakumbushe wanaume kusimama kwenye jukumu lenu, kwa kesi ya Daimond huyo mtoto ni wa mama maana kuzaliwa bila ndoa na ndo maana huyo anafanya huo uhuni bila wasiwasi, Ukitaka kuwa baba Basi jiandae kujenga ufalme wako utakao usimamamia kwa nguvu zako zote, oa mke awe wako na ukifanikiwa kupata watoto Walee kwenye ufalme wako wawe wako hata kama ukiachana na mama yao wewe ngangania kulinda kizazi chako na ikiwa uliwapotezea watoto Basi achana nao wawe watoto wa mama mpaka mwisho na wewe jenga ufalme wako utakao usimamia kwa kupambana kutoa mahitaji na kuujenga, Ila kwa kesi ya Daimond yeye ni mtoto wa mama tena mama ambaye hakuingia kwenye umalikia hayo ya mzee Abdul itakuwa ni mambo ya ukahaba tu kwa wote hata huyo Daimond hakujengwa kwenye ufalme Ila kajengwa na mama asiyekuwa malkia.
 
Diamond na umaarufu wake ni mpumbavu tu.
Mama yangu kwa anavyonifahamu hawezi kuthubutu kuniambia huo ujinga anajua kabisa undugu wangu nayeye utaisha siku hiyo hiyo
 
Nina shauku ya kujua ivi izi drama zinawezaje kumuongezea hela huyu jamaa
 
Nina shauku ya kujua ivi izi drama zinawezaje kumuongezea hela huyu jamaa
Na kama zinamwongezea hela kwa nini wasiwe wanammegea mgao wa kutosha huyo mzee Abdul kutoka kwenye zile pesa zilizovunwa kutokana na zile drama zilizomhusisha?
 
Nina shauku ya kujua ivi izi drama zinawezaje kumuongezea hela huyu jamaa
Msanii anapokuwa ni mchapakazi, anayejua kuji-brand, anayebadilika kimuziki kwenda na muda.

Halafu akiwa na Drama (publicity stunt) nyingi basi ndivyo anavyozidi kuongelewa sana na jamii, na ndivyo anavyozidi kuwa ON TOP OF THE GAME.

Na watu (jamii) ndivyo wanavyozidi kuwa na HAMU na SHAUKU ya kutaka kufahamu kila next moves zake (Nyimbo zake, Biashara zake, Mafanikio yake, Maisha yake etc.)

Hii ni nzuri kibiashara, maana DEMAND (uhitaji) ni kubwa tayari, na SUPPLY ipo. Hivyo msanii hapo yeye ni ku-Supply kazi zake tu (Nyimbo mpya, Shows, Merchandise, Endorsement deals, Biashara ya Matangazo etc.)

Hata Makampuni Makubwa mengi yanapenda kufanya biashara na wasanii wakubwa wenye USHAWISHI (influence) katika jamii.

Drama zikiambatana na Kazi Nzuri zinaweza kumsaidia msanii kuongeza USHAWISHI na MVUTO katika Jamii, na kutengeneza Mashabiki Wengi ambao wako radhi hata kukopa bando ili kuingia online na kufuatilia maisha na drama za msanii wao.

Hivyo msanii wa hadhi na calibre hiyo ni rahisi kwake kupata Endorsement Deals kutoka katika makampuni makubwa.

Kampuni zinataka msanii ambaye ni highly marketable and easily recognizable.

Kazi nzuri zinazoenda na wakati zikiambatana na drama basi zinaweza kumsaidia kumfanya msanii awe highly marketable and easily recognizable.

Msanii akifikia status (hadhi) hiyo basi ni rahisi kwake hata kuanzisha BIASHARA ZAKE NYINGINE NJE YA MUZIKI na Kuzitangaza kwa wepesi zaidi na kupata wateja wengi.

NB:
Lakini inabidi msanii awe na team ya watu sahihi wanaojua jinsi ya kutumia jina la msanii kuongeza mapato (pesa).

Sanaa haihitaji mtu mpole mpole, very innocent, sanaa inahitaji Amsha! Amsha!, mbwembwe na makeke mengi.. Wape watu kitu cha kukuongelea, kile kitu ambacho unaona hakiwezi kukushusha kimuziki bali kitakunyanyua.

Watu Wanataka UMBEA, wewe wape UMBEA!
Changa karata zako ili Umbea ukupe pesa kupitia BIASHARA za NYIMBO katika platforms mbalimbali, SHOWS, ENDORSEMENT DEALS, MATANGAZO, MERCHANDISE (bidhaa mbalimbali au biashara zozote zenye chapa ya msanii) etc...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…