Tatizo ni mfumo wa mawasiliano au? Aliyeshtakiwa makosa 280 ateuliwa kuwa M/kiti Bodi ya VETA

Tatizo ni mfumo wa mawasiliano au? Aliyeshtakiwa makosa 280 ateuliwa kuwa M/kiti Bodi ya VETA

G Sam

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2013
Posts
11,795
Reaction score
36,704
Mashtaka yalisomwa January sita ila kesho yake DPP akaondoa kesi mahsksmani kimya kimya. Sijui alipewa maagizo?


====
Peter Maduki, ambaye alishtakiwa kwa makosa 280 yakiwamo ya kughushi, kuwasilisha nyaraka za uongo pamoja na utakatishaji fedha, ameteuliwa na Rais John Magufuli kuwa mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (Veta).

Mashtaka yao yalisomwa Januari 6 Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Kisutu, lakini ofisi ya Mwendesha Mashtaka wa Umma (DPP) ililiondoa shauri hilo siku iliyofuata baada ya kuonyesha nia ya kutoendelea na kesi hiyo.

Siku hiyo, Maduki na mhasibu wa Wizara ya Afya, Luis Lymo(54) ambaye hakuwapo mahakamani, walisomewa mashtaka na mawakili wa Serikali, Zakaria Ndaskoi na Genes Tesha mbele ya hakimu mkazi mwandamizi, Augustina Mmbando.

Wakati kesi hiyo iliyokuwa imeahirishwa ikisubiri kutajwa, Maduki, ambaye ni mtendaji mkuu wa taasisi ya Christian Social Services Commission, juzi aliteuliwa na Rais Magufuli kuendelea kuwa mwenyekiti wa bodi hiyo ya Veta.

Baada ya taarifa ya uteuzi huo huku kukiwa na kesi hiyo, Mwananchi ilifuatilia kujua undani wake na kuelezwa kuwa ofisi ya DPP ilionyesha nia ya kutoendelea na kesi hiyo.

Wakili wa Serikali, Genes Tesha alilieleza Mwananchi kuwa kesi hiyo iliondolewa mahakamani siku moja baada ya kufunguliwa.

“Shtaka hilo kweli limeondolewa ingawa mimi niko likizo. Taarifa nilizozipata liliondolewa siku iliyofuata baada ya kufunguliwa. DPP alionyesha nia ya kutoendelea na kesi hiyo,” alisema Wakili Tesha.

Mwananchi ilipofuatilia mahakamani hapo ilielezwa na mmoja wa makarani kuwa shauri hilo lilishaondolewa.

“Nakumbuka hiyo kesi ilishaondolewa lakini sikumbuki ni lini jaribu kufuatilia kwa waendesha mashtaka wa serikali,” alisema karani huyo.

Katika kesi hiyo, washtakiwa hao walikuwa wanakabiliwa na mashtaka 150 ya kughushi, mashtaka 128 ya kuwasilisha nyaraka za uongo, moja la wizi na moja la kutakatisha fedha.

Wakili Ndaskoi alidai siku hiyo mahakamani kuwa washtakiwa walitenda makosa hayo kati ya mwaka 2017 na 2019 jijini Dar es Salaam.

Alidai washtakiwa hao kwa nafasi zao wakiwa na nia ovu walighushi hundi mbalimbali zenye thamani ya mamilioni ya fedha na kusaini kwa jina la Upendo Mwingira bila ridhaa yake huku wakijaribu kuonyesha kuwa Luis Lymo alikuwa akilipwa na taasisi ya Christian Social Services Commission fedha hizo kama kamisheni wakati si kweli. Pia walidaiwa kuwasilisha nyaraka za uongo benki ya Standard Chartered.

Pia, washtakiwa hao kwa nyakati tofauti wanadaiwa kuandaa taarifa ya uongo ya benki wakionyesha akaunti iliyopo tawi la NIC Life House la Standard Charterd NIC Life House kuwa ilikuwa na zaidi ya Sh1.7 bilioni.

Pia walidaiwa kuwa kati ya Machi 30/2017 na Oktoba 2018 waliiba zaidi ya Sh1 bilioni mali ya taasisi ya Christian Social Services Commission.

Kwa upande wa shtaka la utakatishaji fedha, walidaiwa kutakatisha zaidi ya Sh1 bilioni wakati wakijua fedha hizo zilitokana na kosa la kughushi.
 
Baba wa taifa mwalimu Nyerere alisema mtu mwenye tuhuma " hafai" kuwa Kiongozi!

Lakini kama kesi iliondolewa na aliyeileta, then Mwenyekiti mpya wa Veta hana makosa!
 
Baba wa taifa mwalimu Nyerere alisema mtu mwenye tuhuma " hafai" kuwa Kiongozi!

Lakini kama kesi iliondolewa na aliyeileta, then Mwenyekiti mpya wa Veta hana makosa!
Kumbuke pia kilichofanyika kwa Mtendaji Mkuu wa TPDC. Alirudishwa na Rais Magufuli kumbe alitolewa pale TPDC kwa mizengwe tu ili watu wafanye yao! Hii ndiyo Tanzania!
 
Unakumbuka yule mzee wa kwny kamati ya makinikia aliposhutumiwa Magu akasema yule alikua kazini.
wengine sio wahalifu, unaweza kuvunja nao sheria mkapelekwa wote mahakamani lakini mwisho unabaki peke yako. kuna watu hiyo ni kazi yao.

dodge
 
Au imetumika dhana ya mtuhumiwa hana hatia mpaka atakapohukumiwa?
 
G Sam, unapoamua kuchungulia chumbani mwa BABA yako ,tarajia mengi , ngoja mimi nikacheze nilipozoea tyu,
 
Ndipo taifa letu lilipofika.Umoja na ustawi wa taifa letu shakani. Wacha viongozi CDM,wateseke na wapoteze muda. DC Hai katoa hukumu wamiliki mabus. Ila uzuri yanamwisho haya

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kumbuke pia kilichofanyika kwa Mtendaji Mkuu wa TPDC. Alirudishwa na Rais Magufuli kumbe alitolewa pale TPDC kwa mizengwe tu ili watu wafanye yao! Hii ndiyo Tanzania!
Amini nakuambia kuna tatizo kubwa katika uongozi wa rais wa awamu hii. Rais anatumia vibaya madaraka yake "ku-dismiss" tuhuma za watendaji wa serikali yake anaowapenda.

Kwanza ieleweke kuwa kuna watu "wapo kazini" kufuatilia nyendo za watendaji walioko serikalini. Watu hao wanafanya hivyo katika kutekeleza majukumu na wajibu wa kazi zao. Wanatumia intelijensia zao kukusanya taarifa kuhusiana na utendaji kazi wa watu wanaowafuatilia na wanapobaini "madudu", huwasilisha ripoti kwa vyombo vingine ili hatua zingine zichukuliwe dhidi yao kama vile mashtka.

Kiufupi ni kwamba, kuna mlolongo mrefu ambao unahusisha vyombo mbalimbali hadi tuhuma dhidi ya wahusika zinafikishwa mahakamani. Lakini lamuhimu ni kuelewa kwamba watuhumiwa wanapofikishwa mahakamani si kwamba ni "uonevu" dhidi yao bali ni kuwapa haki (fursa) ya kujitetea dhidi ya tuhuma wanazoshukiwa kwazo.

Ni mahakama peke yake ndio yenye mamlaka ya kuamua iwapo watuhumiwa wana makosa kweli au la. Lakini inapotokea mtuhumiwa ni "kipenzi" cha rais, mchakato wa kimahakama haufiki mwisho. Rais huingilia kati mchakato wa kimahakama na kufanya jambo fulani ambalo "humnyanyua" na kumpa kinga mshtakiwa "kipenzi" na hatimae maagizo ya "ku-abort" mashtaka dhidi yake hufuata.

Rais hutumia njia mbali mbali "kumnyanyua" mtuhumia kutoka kwenye tuhuma kwa kumpa nafasi ya uteuzi, kumpandisha cheo au hata kwa kusema tu "kuna watu wanafanya fitina kwa mashtaka ya uongo dhidi ya mtuhumiwa ili ang'oke na wafanye yao". Hivi kuna mtu au chombo chochote chenye uwezo wa kuendelea na mchakato wa kuchukua hatua dhidi ya muhusika ambaye anapewa "promotion" kutoka kwa rais wa nchi?

Hili ni tatizo kubwa la kiungozi. Kama mtuhumiwa ni "msafi" kwanini rais anaingilia mchakato wa mahakama kwa "kumnyanyua" mtuhumiwa? Kwanini rais anageuka "chombo cha kutoa haki" badala ya mahakama kwa kuonesha mtuhumiwa "alionewa" nia mbaya? Lakini anaposema "kuna watu" walimsingizia muhusika kwa nia mbaya, hao "watu" ni akina nani na huwa anawachukulia hatua gani kwa kujaribu "mumpaka matope" mtu aliye "msafi"? Hivi anatumia mchakato gani kubaini ubatili wa mashtaka zaidi ya 100 ya mtuhumiwa ndani ya siku moja baada ya kufikishwa mahakamani ?
 
Daaah,

Rule of Court is intervented by authorities.

So sad
 
Au imetumika dhana ya mtuhumiwa hana hatia mpaka atakapohukumiwa?
Hapana. Si hivyo kwa Tanzania. Watuhumiwa wote wa uhujumu uchumi wana hatia kiasi rais aliwasamehe na kuelekeza/ kutoa ushauri wakiri wenyewe na kurudisha kiasi cha pesa wanachotuhumiwa!

Mshana Jr., hapa kuna jambo. Si bure Kabudi alisema aliokotwa jalalani! Waangalie wateule wake: Kangi Lugola, Kicheere, Diwani Athmani, n.k Jaribu kukumbuka vizuri wanakopitishwa kwanza: tuhuma au kejeli; kisha kuteuliwa. Wanatolewa jalalani. Ya Kabudi hayafahamiki sana. Labda aliishashushwa au kutuhumiwa kama wengine. Anajua vizuri zaidi na akashukuru na ndipo nasi tukasikia.

Kumbuka field na house niggers wa Malcom X. Akiwatoa huko jalalani wanakuwa house niggers. Kabudi akiitwa pumbavu ndipo anapiga tabasamu la nguvu! Mwenendo wote ni wa house nigger. Lugola, Kicheere vilevile. Hata huyo mpya ukisikia amewafukuza wanafunzi wote wa VETA, ukishangaa utakuwa sio kiti! tena. Utakuwa umemsahau Ndalichako (of all people) na wanafunzi wa UDSM?Kuna kamchezo ka wateule wake wote kuitikia TAWIRE!
 
G Sam,

Jr[emoji769]
IMG-20200122-WA0026~2.jpeg
 
..hili suala linashangaza sana.

..inakuwaje mtu anatuhumiwa na serikali kwa makosa mengi kiasi hiki, halafu " gia inabadilishwa angani" kwa mashtaka kufutwa, na mhusika anapata presidential appointment?

..nadhani suala hili halipaswi kuachwa likapita hivihivi.

..yanahitajika maelezo ya kina kuhusu nini haswa kilitokea.



Cc : Nguruvi3, Kiranga, johnthebaptist, tindo, Mzee Mwanakijiji, Pascal Mayalla, Manelezu, Kamundu
 
ukiona ivo jua huo utakatishaji wake uliwanufaisha ccm katika michakato ya uchaguzi ama kuendesha ofisi na shughuli zao za kila siku.
 
Mnafiki hamuwa hana kumbukumbu. Umesahau yakle ya Alfayo Kidata?
 
JokaKuu,

Kama humpingi wala kumkosoa rais, hata ukiwa na makosa iwapo atataka hata kama una makosa anakuchagua tu, na makosa yako yote yanayeyuka.
 
Back
Top Bottom