kauli yako ina mapungufu ya aina mbili; kwanza ina mtizamo mgando. Ubora wa wahitimu katika miaka zaidi ya arobaini ya uhai wa chuo hicho, umekuwa ukihitirafiana siyo tu kwa fani moja na fani nyingine, lakini pia kwa mwaka hadi mwaka. Pili, kimsingi inalinganisha vitu viwili vilivyo tofauti. Katika hali halisi, wahitimu wa vyuo vya dit na mzumbe tangu mwanzo ilikusudiwa wawe watendaji (technitians), wakati wale wa mlimani walitegemewa wawe waratibu (coordinators). Ni kutokana na sababu hiyo, ndiyo maana baada ya kuhitimu dit na mzumbe walikuwa wanapewa diploma na mlimani digree. Tofauti kati ya diploma na digree, ni kwamba mtu wa diploma anazama zaidi katika eneo dogo, wakati mtu wa digree anafundishwa kwa lengo la kuwa na uelewa kwa maeneo mengi, ili aweze kuratibu kazi za wengine. Watu wengi huwa wanapotosha ukweli kwamba mtu anaweza akawa mwana taaluma tu kwa kujifunza darasani. Hii si kweli, ndiyo maana si sahihi hata kidogo kumwita jk mchumi au pinda mwanasheria, kwasababu waheshimiwa hawa tangu wahitimu wamekuwa wakifanya mambo tofauti na fani zao.