Tazama baadhi ya mapungufu yaliyojitokeza katika majina ya ajira za Ualimu yaliyotolewa. Jina la 'ABADALLAH LEONARD SHONDE lajirudia mara 196

Trust None

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2018
Posts
1,260
Reaction score
4,419
Kusema ukweli hizi ajira ni MAGUMASHI, hazina uhalisia wowote. Jina moja linajirudia mara nyngi na kituo ni kilekile.

Kuna wengine wamemaliza fom4 mwaka 2019 eti na wao wameajiriwa.

Swali: Kwanini hawajaandika vyuo walivyosomea? Kwanini hawajaweka serial number?

MUNGU TUNUSURU

---
---
Ali Maulid Mtawatawa-1997

Beatrice Apolinary Lyimo -1999

Charles Nyagaya John -1995

Miaka 20+ iliyopita alikuwa wapi hadi mwaka huu ndio waajiriwe?
---
---
---



PIA SOMA:
= > TAMISEMI yatangaza ajira za walimu shule za msingi na sekondari. Walimu waliopata ajira watakiwa kuripoti kuanzia Desemba mosi, 2020

= > Serikali: Walimu wa Shule za Sekondari na Msingi walioajiriwa ni elfu nane pekee
 

Attachments

Mkuu,

Unamacho na uko makini sana; ni kweli hilo jina limejirudia tena kila ukurasa mstari wa kwanza jina hilo ndio linaanza.

Matatizo ya watumishi ya kukopi na kupaste kwenye spreadsheet bila kutumia fomula ya hesabu sahihi ndio matokeo yake hayo.

Kwa mantiki hiyo jina hilo linakosesha haki ya walimu wenye sifa 195 hivyo kutoa mwanya wa rushwa kuchomeka mtu kisha orodha inarekebishwa.

TAMISEMI and Ministry of education must take drastic action to restore the rights of the qualified teachers.
 
Mwl Abdallah leonard shonde aibuka kidedea Kwa Kuorodheshwa Mara 3233,katika ajira Mpya Ni mwalimu wa kwanza kupendekezwa zaidi na Tamisemi Tangu Tanzania ipate Uhuru mwaka 1961[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Nmeinanga tu japo ni makosa ya mtu wa ms-exl
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…