libeva
JF-Expert Member
- Mar 25, 2015
- 4,465
- 3,615
Yaleyale niliwahi sema hapa kuwa shule za vijijini ngumu wapekekwe jinsia ya ME sasa shule ngumu wamepelekwa jinsia KE wanahaha kuchomoa kutokwenda, nipo sehemu mama anapiga simu mdogo ake kapangiwa Katavi amekataa kwenda anataka Dar, Moro na Pwani mama anasisitiza ongea na katibu amuhamishe, lengo la ajira kwamba kuwe angalau kuna usawa wa ikama mashuleni linatoweka mrembo hatafundisha shule za pembezoni kamwe akienda baada ya miezi kadhaa anarudi mjini ndio maana shule za mijini walimu wengi ni wanawake wanaume wachache sana na shule za pembezoni zitaendelea kukosa walimu miaka nenda rudi kwa kuwapeleka wa jinsia wa KE.