Tazama: Said Fella ni mshamba Not In a Way - huyu ni mshamba Per sé

Tazama: Said Fella ni mshamba Not In a Way - huyu ni mshamba Per sé

Fella mchizi wangu... tena sana tu... long time kitambo hata Bongo Flavor haijaanza!! Lakini kibongo bongo, uki-mess na Fella; umeumia... bora u-mess na Ruge! Nakumbuka enzi za Wanaume Family, maskani madogo walikuwa wanamuogopa kama ukoma... wakianza kumng'ong'a basi ni lazima wafanye hivyo kimachale machale kwa imani kwamba Fella alikuwa anawaandea kwa bibi! Siku nimemuona Fella nyoko ni pale alipozinguana na mmoja wa washikaji wa Wanaume Family... kwa ku-show love, watu tukam-support yule mchizi akaenda studio, akagonga kopi kibao... nakumbuka tulihangaika sana kusambaza ile album radio stations...hata hivyo, haikupata airtime kabisa! Wambeya wakatupenyezea habari kwamba Fella kapita kufukia nyayo kila tulipopita... mchizi ambae tulimpa support ni very talented lakini amebaki historia!!

Hata hivyo, Fella sio mshamba kihivyo, sema inawezekana akinyuka pamba hazimtoi! Long time alikuwa na tabia ya kuvaa vijinzi vya kubana... ingekuwa siku hizi tungeita model... pata picha na ule mwili wake ingawaje enzi hizo hakuwa vile!!!

Kweli kabisa Juma nature kibra akapotea hadi leo amebaki kivuli cha nature tu
 
mkuu bado nipo huku,lol naona unabadili sana majina,mmu nimepunguza siku hizi nakaa huko kwenye siasa na celebrity.

Kumbe ni wewe... Watu mmebadilika mhhh hata chige y ulibadilisha jina na ngozi yako? Ni wakati na Mimi nibadilishe jina japo ngozi sitaibadili
 
Last edited by a moderator:
Kumbe ni wewe... Watu mmebadilika mhhh hata chige y ulibadilisha jina na ngozi yako? Ni wakati na Mimi nibadilishe jina japo ngozi sitaibadili

lol kumbe hukunigundua siku nyingi,huyo chige bado sijamsoma
 
Last edited by a moderator:
Na ni kweli, its a total turn off kwa mimi, mi mwenyewe sipendi kujitwisha mipete akuu

Umeona eeh?Mimi napenda kijipete kiduuuchu kizuri zuri,sio jipete hilo!
Hadi kidole kinakufa ganzi!
 
kiukweli fella kwa muonekano ni mshamba sana ila jamaa ni bonge la mjanja la kupanga mawazo kuwa pesa....siyo leo jamaa janja wayback kabla halijatoka dizonga na kuja bongo na kuanza kupiga mpunga kwenye music kwa kuanzia na juma nature!

Mke wake huwa namkubali sana.

MkewaMkubwaSaidFelakulia.jpg
Mke wa Said Fella aliyevaa pedo nyekundu.
 
Ni nani anayevaaga hizi nguo zenye rangi ya kijani akawa mjanja!
Mkubwa-Fella-II1.jpg
 
Well, kikubwa kinachowaangusha wasanii ni mtaji na ubora wa kazi zao. Shughuli yoyote inahitaji uwekezaji, kama mtu ni msanii kweli ana kipaji, akaweka na userious unaotakiwa akatoa kazi ya kiwango cha juu sidhani kama soko litamsumbua. Kikubwa ni kazi iwe na ubora, na hii inahitaji fedha.
 
bwah bwah bwah.... mwenyewe nilishajiandaa kwamba huyu akinifanisha na boyfriend wake wa shulei tu, nasema YES, ndo mimi huyo huyo!!!

hahahaaaaaaaa nimecheka kwa sauti kubwa kweli yaani weweeeee
 
Mwacheni mkubwa Fela senzii kabisa! Hajui kuvaa ila anakuzidi mavumbaa
 
Kweli kabisa Juma nature kibra akapotea hadi leo amebaki kivuli cha nature tu
Dah... we acha tu. Kibla kimya kabisa... liebaki jina tu na hata leo akipandishwa jukwaani ni kwa ajili tu ya kazi alizofanya zaidi ya miaka mitano iliyopita!
 
Kumbe ni wewe... Watu mmebadilika mhhh hata chige y ulibadilisha jina na ngozi yako? Ni wakati na Mimi nibadilishe jina japo ngozi sitaibadili
Sijabadili jina Mrembo by Nature, moja ni la kabla ya kwenda jando na lingine nililopewa baada ya kurudi jando... kwanza rangi na sauti ndo kabisaaaaaa; kama zamani tu!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom