Wewe unafikri jamii ni UKAWA, umeishiwa, TBC1 ni gwiji la habari Tanzania.
Kwanza jamii inakushangaa wewe kuendelea kuisikiliza au kutazama tbc
Kwani chadema mnashindwa kuanzisha TV yenu ruzuku inaenda wapi ikiwa hata ktk matawi haifiki? Acheni kulalamika fungueni ya kwenu hata taasisi za dini zinawashinda??
Wewe kisebengo nini?hiyo tbc ni mali ya ccm?
Mkuu kama wewe ni Mwanaukawa mambo ya katiba mpya hayakuhusu. Tuachie wazalendo tutaipitisha.Kwa TBC1 hiyo haitatokea.
Hata wakeshe wananihamasisha kupiga kura ya ndiyo
mimi ni HAPANA tu maana mapendekezo ya tume ya Warioba mengi yalipanguliwa
Upo sahihi! Hiyo TBC tuwaachie wenyewe. Huoni hata wakuu wa wilaya wanateuliwa kutoka TBC!
TBC ni kama maji kama usipoyaogea utayanywa.
Ndio maana mijadala yenu kuhusu matangazo ya TBC haikauki humu jamvini wakati mnajifanya hamuitazami.
Mkuu kama wewe ni Mwanaukawa mambo ya katiba mpya hayakuhusu. Tuachie wazalendo tutaipitisha.
Wana Ukawa ni watanzania na katiba inawahusu.
Wanaposema kupiga kura ya NDIYO au HAPANA ina maana Watanzania wana mitizamo tofauti juu ya katiba pendekezwa.
Kuipitisha sio Demokrasia ila kutoa elimu ya yale yaliyomo kwenye katiba pendekezwa, kuweka mazingira rafiki ya kuipigia kura na kuhesabia kura kwa uwazi na uaminifu ndiyo democrasia. jambo hili sio utamaduni wa nyie "WAZALENDO"
Hakuna sehemu nimesema WANAUKAWA sio watanzania.
Viongozi wa UKAWA ndio waliosema kuwa wao na wafuasi wao hawatashiriki zoezi la kupigia kura katiba mpya.