TCCIA-Hali ya biashara ni mbaya Dodoma

TCCIA-Hali ya biashara ni mbaya Dodoma

Feld Marshal Tantawi

JF-Expert Member
Joined
Dec 24, 2014
Posts
655
Reaction score
1,069
CHAMA cha Wafanyabiashara wenye Viwanda na Kilimo Tanzania (TCCIA) Mkoa wa Dodoma, kimesema japo serikali haijawafungia watu ndani, lakini hali ya biashara mkoani hapa imeendelea kuwa mbaya siku hadi siku.

Akizungumza wakati wa mahojiano na Habari- LEO, Mwenyekiti wa TCCIA mkoani hapa, Denis Nyabiri amesema katika utafiti mdogo alioufanya kwa wanachama wake mkoani hapa, amegundua kuwa hali ya biashara siyo nzuri.

Alisema kila mfanyabiashàra mjini na vijijini, analalamika biashara kuwa mbaya, japo tangu awali hali haikuwa nzuri lakini kwa sasa imezidi kuwa mbaya.

“Nataka ufanyike utafiti kuhusu hali ya biashara nchini kwa sababu hata kama serikali haijawazuia watu ndani lakini hali imekuwa mbaya sijui kwa sababu serikali imezuia mikusanyiko na safari zisizo za lazima?”vip maeneo mengine huko hali ipoje?
 
Yeye ni wa Dodoma (mkoa) halafu anasema ANATAKA UTAFITI UFANYIKE, tena NCHINI...!!!

Hizi statement za NATAKA, NAAMURU, NAAGIZA, tena kwa issues zinazohusu NCHI, zinatolewa na mtu mmoja tu aisee. Yeye anatakiwa KUSHAURI.

Huyo jamaa anafeli wapi aisee???

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom