TCRA ishirikiane na Shirika la Mawasiliano la Kenya kuwasaka matapeli hawa wa mitandaoni

TCRA ishirikiane na Shirika la Mawasiliano la Kenya kuwasaka matapeli hawa wa mitandaoni

mmaroroi

JF-Expert Member
Joined
May 8, 2008
Posts
4,635
Reaction score
2,271
Ni wito kwa TCRA ishirikiane na Shirika la Mawasiliano la Kenya kuwasaka matapeli hawa wa mitandaoni. Huu utapeli wa mtandaoni umevuka mpaka kutoka kuwa wa Kitaifa sasa ni utapeli kimataifa. Namba za simu zifuatavyo ni baadhi ya zinazotumiwa na matapeli, +254794812691 (Alex Kairi), +254102269805 (Rusi Sigel) na +254102143329. Katika utapeli wao wanatumia jina UNICEF Foundation Funds. Tahathari kwa wote juu ya utapeli huu. Mods tafadhalini huu uzi usichanganywe na zingine ili ibaki wito kwa TCRA ishirikiane na Shirika la Mawasiliano la Kenya kuwasaka matapeli wa mtandaoni. Nawasilisha.
 
Vipi umeshasikia kuhusu zile pesa za Unicef? Ukiingia mkenge umeliwa sababu ya Tamaa zako
Ni kweli inawezekana wanafanikiwa, ndio maana tunapaza sauti wasakwe wasiendelee kuwatapeli watu. Kutokana na umaskini kutamalaki ni rahisi watu kunasa kwenye mitego ya matapeli hao kwa kuwatamanisha watu na utajiri wa haraka.
 
Zimenikuta mara nyingi mno mpk ninawatukana pia nimegundua kuwa wana hacked account za watu na kufanya michezo iyo😡
Ni kweli, wanadukua namba za simu za watu na kutumia kuwahadaa watu kwa utapeli huo. Tuorodheshe humu namba zote wanazotumia ili mamlaka husika ziwafuatilie.
 
Ni kweli inawezekana wanafanikiwa, ndio maana tunapaza sauti wasakwe wasiendelee kuwatapeli watu. Kutokana na umaskini kutamalaki ni rahisi watu kunasa kwenye mitego ya matapeli hao kwa kuwatamanisha watu na utajiri wa haraka.
Sasa unaambiwa ioli upate ile milioni mbili toka UNICEF basi uchangie kiasi flani cha pesa. Why wasikate hicho kiasi hukohuko? 😀
Unatuma 150k wanapotea nayo
 
Zimenikuta mara nyingi mno mpk ninawatukana pia nimegundua kuwa wana hacked account za watu na kufanya michezo iyo😡
Yaani mtu akifuata link yao inampeleka kwenye namba ya WhatsApp ya Kenya huko. Pale ndio anakuwa hacked. Saaa hivi wanahack mpaka WhatsApp maana walikuwa kule Facebook tu.
Tukiacha kupenda vya bure hawawezi kutupata Sema shida yaani umaskini ni jambo baya sana
 
Sasa unaambiwa ioli upate ile milioni mbili toka UNICEF basi uchangie kiasi flani cha pesa. Why wasikate hicho kiasi hukohuko? 😀
Unatuma 150k wanapotea nayo
Hakika ni suala la kutumia lojiki hiyo kugundua utapeli wao ila si wote wenye upeo huo wa ufahamu na huangukia kwenye mitego yao. Ndio tuwasaidie kwa kupasa sauti ili wahusika wasakwe popote na wasiendelee kuwatapeli watu.
 
Yaani mtu akifuata link yao inampeleka kwenye namba ya WhatsApp ya Kenya huko. Pale ndio anakuwa hacked. Saaa hivi wanahack mpaka WhatsApp maana walikuwa kule Facebook tu.
Tukiacha kupenda vya bure hawawezi kutupata Sema shida yaani umaskini ni jambo baya sana
Umesema kweli tupu. Tuorodheshe humu namba zote wanazotumia matapeli hao
 
Back
Top Bottom