TCRA kazi ya kudhibiti muingiliano wa masafa imewashinda?

TCRA kazi ya kudhibiti muingiliano wa masafa imewashinda?

Jidu La Mabambasi

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2014
Posts
16,419
Reaction score
26,594
Kazi moja kubwa ya TCRA toka wakiwa kitengo cha kudhibiti masafa ya kurusha mawimbi ya redio wakiwa Posta na Simu(TP &TC), ilikuwa kuangalia ni nani anarusha mawimbi yake katika masafa yepi.

Sasa hivi tuna TCRA ambao siyo siri wana mitambo mikubwa na makini zaidi lakini wasomi hapo na mainjinia ni wengi zaidi.

Majuzi nikiwa nasikiliza redio ya gari yangu nikafungulia masafa ya 92.5 MHz.

Nilikuwa nasikiliza zilipendwa, mara baada ya dakika fulani nasikia mawahidha ya kiislamu, mara mtangazo mengine.
Nikajaribu ku fine tune lakini tatizo likawa pale pale.

Siwalaumu wenye redio, nailaumu TCRA, inaelekea wanaanza kushindwa kazi ya kiuhandisi ya ku monitor matumizi ya masafa.
Aidha wametoa leseni za masafa karibu karibu sana yaani wameuza 92.3, 92.4 na 92.5 hivyo muingiliano au uzembe tu wa ku monitor matumizi ya masafa.

Kwa kweli inakera wakati ukisikiliza kipindi pendwa, halafu kinaingiliwa na masfa mengine.

Wajuvi wa sheria ya mawasiliano mtujuze na mpo mnaoifahamu hiyo sheria, tunaweza vipi kuishitaki TCRA kwa huduma mbovu wanayotoa kwa umma.

Kiukweli wao TCRA wanakuwa wakali katika ku monitor content ya matangazo na kupiga fine kubwa kubwa.
Wasikilizaji je tuchukue hatua zipi kulishitaki hili shirika kwa uzembe wa wazi?
 
Sijui upande wa sheria ila hili tatizo la frequency kuingiliana ni kero sana mfano FM ukiwa mara, Arusha redio za Tanzania huzishiki jioni utaishia kusikiliza kiganda na kijaruo tu.
 
Nadhani hiyo ni radio mpya ya nchi jirani ya Zanzibar ipo kwenye majaribio bado. Nenda TCRA Zanzibar au Sam Nujoma watatatua haraka sana hiyo changamoto.
 
Nadhani hiyo ni radio mpya ya nchi jirani ya Zanzibar ipo kwenye majaribio bado. Nenda TCRA Zanzibar au Sam Nujoma watatatua haraka sana hiyo changamoto.
Elewa tatizo.
Sina tatizo na redio yangu, tatizo lipo kwenye muingiliano wa masafa.
Wanaotoa masafa ni TCRA, na hapa wamevurunda.
Watatoje masafa yanayoingiliana?
 
Ni kweli kabisa.
Jioni hii nasikiliza nyimbo za kuabudu na kusifu channek 87.5Mhz ,kuna muingiliano na redio nyingine.
TCRA wapi weledi wenu?
 
Ni kweli kabisa.
Jioni hii nasikiliza nyimbo za kuabudu na kusifu channek 87.5Mhz ,kuna muingiliano na redio nyingine.
TCRA wapi weledi wenu?
Kuzuia kuingiliana masafa kwa redio ndio inatakiwa kuwa core duty-jukumu kubwa la TCRA.
Wanashindwa wapi haieleweki.
 
Nilichogundua redio nyingi za dini ya kiislam mikoani zimeminywa na huo ukaribu wa freq na redio nyengine.wenye kufuatilia fuatilieni.
 
Miaka ya nyuma nilikuwa nasikiliza KBC Nairobi akiwepo lenadi mambmbotela!

Mchana DW kutoka mjini koloni na jioni BBC London!


Kitaalam frequencies huathiriwa na majengo, good conductor, miinuko na ubora wa chombo chako.

Mwl wa physics
 
zaman tultengenezaga ka redio ka mtaan kwa kutumia zile memory q tukaweka antena na maik zetu ikawa inashka bila mpangilio tukawa tunashka mawimb karbu mtaa mzma tunatangaza maziwa ya mgando unapata kwa mama flan mkaa mzur uko kwa flan wanatulipa 500 tu cc tunaona raha cku ya cku tukashangaa goflu ya polis iko mtaan inatutafuta na k redio mtaa kikafia apo apo
 
zaman tultengenezaga ka redio ka mtaan kwa kutumia zile memory q tukaweka antena na maik zetu ikawa inashka bila mpangilio tukawa tunashka mawimb karbu mtaa mzma tunatangaza maziwa ya mgando unapata kwa mama flan mkaa mzur uko kwa flan wanatulipa 500 tu cc tunaona raha cku ya cku tukashangaa goflu ya polis iko mtaan inatutafuta na k redio mtaa kikafia apo apo
Yaan hapo ndipo unapoona akili za wabongo zilivyo mbovu yaani badala ya kuwasaidia ili mkuze kipaji zaidi lakini mtu anatumia nafasi hiyo kuifungia tena duuuh
 
Back
Top Bottom