TCRA: Matapeli wa "Tuma kwa Namba Hii" tumewapunguza

TCRA: Matapeli wa "Tuma kwa Namba Hii" tumewapunguza

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Vitendo vilivyoripotiwa vya ulaghai kwenye mitandao ya simu vimepungua kwa asilimia 28 kati ya Juni na Septemba mwaka huu, kutokana na hatua kali za serikali na kampeni za kuongeza uelewa wa watumiaji.
1733216610531.png
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Dkt Jabiri Bakari, alifichua katika Ripoti ya hivi karibuni ya Takwimu za Utendaji wa Sekta kuwa majaribio ya ulaghai yalipungua kutoka 22,267 Juni 2024 hadi 16,069 mwishoni mwa Septemba, pia alisema ushirikiano mkubwa kati ya wadau muhimu, wakiwemo watoa huduma za simu pia ni jambo muhimu katika mafanikio hayo.

Katika azma mpya ya serikali ya kupambana zaidi na vitendo vya uhalifu, hivi karibuni wizara ya habari, mawasiliano na teknolojia ya habari na mambo ya ndani iliitisha mkutano wa ngazi ya juu wa wadau ili kushughulikia utapeli wa mitandao na usalama wa mitandao, washiriki wakiwaa wenye leseni za mitandao ya simu za mkononi na wadau wengine wa usalama mtandaoni.
 
Kwangu txt za utapeli zimepungua.
Ila ilitakiwa iwepo adhabu public tena mtu arushwe kuanzia channel 10,star tv,TBC milard ayo kote akijielezea kwamba yeye ni tapeli na msamaha wake uwe ni complete list ya watu aliowatapeli na kiasi na apewe muda kuzirudisha hela zote hizo akishindwa ni jela.
Nadhani Public display itawanyoosha.
 
Matapeli bado wengi sana na saivi wapo wanapiga kutoka TCRA kabisa eti piga namba hiyo ufuate maelekezo, bila hivo tunakufungia line yako. Mimi nikawaambia fungeni tuone
 
Back
Top Bottom