Sasa wasafi wasubiri kufutiwa leseni.πππ
Kwani Kina Lokole na Baba Levo ndio Walioomba hiyo kazi ama UTAWALA uliamua?!!!
Isije ikawa vetting ya kupata faida zaidi imefanyika zaidi kuwa recruit halafu wewe unakalia HISIA..ππ
Cutie bana ππSasa wasafi wasubiri kufutiwa leseni.
Sema watangazaji ndo reflection ya watazamaji/wasikilizaji.Hakika...
Je Wasomi Waandishi wa habari wanaweza kudeliver vyema kitakachopendwa na Walaji Wa habari?!!!
Kwani Walaji wanaopenda UDAKU ili uwapate Ni Lazima uwe MDAKU....
Sure...Sema watangazaji ndo reflection ya watazamaji/wasikilizaji.
Basi walau wawe update na sheria na wajue nini inatakiwa iende hewani na ipi haitakiwi.Nawaza Hapa.....
Hivi mtu anataka kuwe na MWANATAALUMA wa habari,kwenye kipindi Kama MASHAMSHAM Cha WASAFI FM?!!!
Huyo mwanataaluma atadeliver vyema ubora kwa wateja wao kama hao kina Dida,Babu Iddy na Ankali Mambi?!!!
Nikiwa Kama Msomi nilikuwa Sina mzuka kabisa wa kusikiliza vipindi Aina hiyo,ila ninavyozidi kukua kifikra huwa nikiwa OFF DUTY huwa ninawasikiliza vyema tu ili kuwafahamu maisha ya wenzetu wa uswazi lakini pia kutoa STRESS ZA MIHANGAIKOπππ
Aache fujo alete makaratasiUko sahihi jamaa yuko vizuri kichwani ana IQ kubwa , nimemjua kitambo mtaani kijitonyama miaka ya 80s,angesoma zaidi sijui ingekuaje
Swadakt!!Basi walau wawe update na sheria na wajue nini inatakiwa iende hewani na ipi haitakiwi.
Ha ha ha Kwako Makaratasi Yana Umuhimu Sana kuliko INTELLECT eee?!!!Aache fujo alete makaratasi
Huyu jamaa Ni jembe!Sina Mafungamano na Masudi Ally Kipanya na nikiwa Kama kijana Msomi siijui elimu yake ila toka ninakua mpaka Sasa nimekuwa nikimfuatilia KP na kumaizi kuwa ni mtu Mwenye akili,patriotic and visionary zaidi ya Sisi wengi tulio na Doctorates na Masters....
Nisamehe kwa kusema labda unamsigina haiba yake kwa Ad Hominem.
....Mtu HASWAAAA!!Huyu jamaa Ni jembe!
Ilitolewa Miaka mitano kuanzia 2016 mpaka 2021 sasa Kama mtu anataka kuwa mtangazaji na hajasomea awaachie waliosomea.Kutabaki mtu kweli kwenye vyombo vyetu vya habari Tanzania?
Mtu mwenye uzoefu miaka 5 wa kufanya kazi chini ya mtu mwenye taaluma au chombo cha habari tajika pia wangeruhusiwa lakini siyo chini ya Cyprian Musiba wa Tanzanite TV.
Hii TCRA wakikazia kina Dida, Fumbuka n.k kweli watabaki mjengoni?
Au wafanye kipindi cha mpito wasiokuwa na vyeti wasome Kozi maalum ya wiki moja kuwawezesha wasio na vyeti isimamiwe na Media Council of Tanzania (MCT) au The School of Journalism and Mass Communication UDSM , SAUT n.k
Baada ya muda wa mpito tuseme miaka 5 toka sasa sheria hiyo ya TCRA itumike bila kupepesa macho.
Hivi kunatofauti kati ya "journalist" na "Presenter"..?MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA(TCRA) YATOA ONYO KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU KUAJIRI WATANGAZAJI WASIO NA TAALUMA.
Mamlaka ya Mawasiliano nchini imetoa onyo kwa vyombo vya habari hususani redio na televisheni kwa kile inachodai kuwa vyombo hivyo vimekua na tabia ya kuajiri watangazaji wasio na taaluma hiyo.
Katika tarifa iliyotolewa na mamlaka hiyo leo Septemba 14 imewataka wamiliki wa vyombo hivyo kuzingatia matakwa ya sheria na masharti ya leseni ya utangazaji kwa kuhakikisha kuwa wanaotangaza katika vyombo vyao wana vigezo vya kitaaluma kama waandishi wa habari.
Mamlaka hiyo imefafanua kuwa kwa mujibu wa sheria ya vyombo vya habari ya mwaka 2016 kifungu cha 19(1) kinaeleza kuwa kufanya kazi kama mwandishi wa habari pasipo kuthibitishwa kwa mujibu wa sheria ni kuvunja sheria na kwa mujibu wa kanuni ya 17(2) ya vyombo vya habari ya mwaka 2017 ili mtu athibitishwe kuwa mwandishi pamoja na mambo mengine anatakiwa kuwa na shahada au stashahada ya uandishi wa habari au inayohusiana na masuala ya vyombo vya habari kutoka chuo kinachotambulika kinachotoa elimu ya masuala hayo au shahada au stashahada ya masuala ya Vyombo vya Habari.
Kuwa na watangazaji wasio na elimu juu ya masuala ya habari na utangazaji kunapelekea kutendeka kwa makosa mengi ya kutozingatia miiko ya uandishi na utangazaji wa habari, hivyo kuwa kinyume na matakwa ya kifungu cha 7(2)(a)(iii) cha sheria ya vyombo vya habari ya mwaka 2016 kinachotaka vyombo vya habari kuzingatia misingi na miiko ya uandishi wa vyombo vya habari.
Aidha, Mamlaka imevikumbusha na kuvionya vyombo vya habari kuwa hatua zaidi zitachukuliwa, ikiwa ni pamoja na kutoza faini, au kufuta leseni ya chombo chochote kitakachokiuka masharti ya leseni, kanuni na Sheria.
Ikumbukwe kuwa mamlaka hiyo ilitoa taarifa kuwa mpaka kufikia mwaka 2021 Vyombo vyote vya Habari vinatakiwa kuwa na waandishi na watangazaji waliokidhi vigezo vya kitaaluma.
Yule Dr Isaack Mzee wa Njia Panda vipi? KASOMEA UANDUSHI AU UDOKTA?Hakuna tatizo hapo na vyombo vya habari vilishajipanga.
Mfano:
1. Clouds katika powerbreakfast mtangazaji ni Barbara ambaye naamini ni mwana taaluma. Halafu hawa wengine wanahudhuria kama waalikwa au wachangiaji. Ndio maana utaona yeye ndiyo hucontrol matukio ndani ya kipindi.
2. Wasafi vivyo hivyo wana Salma Dakota, Maulid, Sekioni ambao ni wana taaluma na wanacontrol vipindi husika. Wengine wanakuwa wachangiaji tu.
Duh afadhali maana hii taaluma iliingiliwa sana, subiri nirushe karata zangu sasa
Upuuzi ndo unaanziaga hapa[emoji121][emoji121]Kuwa teller hakuitaji kusomea banking