Technology: Mifuko ya uzazi bandia inayotengeneza watoto, wanawake hawatabeba tena mimba. Wazazi kuchagua jinsia,rangi,akili urefu wa watoto?

Technology: Mifuko ya uzazi bandia inayotengeneza watoto, wanawake hawatabeba tena mimba. Wazazi kuchagua jinsia,rangi,akili urefu wa watoto?

Justdr

Member
Joined
Jun 1, 2021
Posts
52
Reaction score
104
Mwanateknolojia wa kibaolojia na mtayarishaji wa Filamu Hashem Al-Ghaili anatupeleka kwenye ziara isiyotulia lakini ya kuvutia ndani ya EctoLife - kituo cha kwanza cha uzazi wa mpango

EctoLife ni teknolojia itakayowapa wazazi wa siku za usoni njia mbadala inayodhaniwa kuwa salama zaidi ya uzazi wa asili, kuondoa matatizo ambayo mara nyingi huwa hatari yanayohusiana na uzazi.

Mfano kifurushi cha "Elite package" kitaruhusu watu kuchagua kiwango cha akili cha mtoto wao, urefu, nywele, rangi ya macho, nguvu za mwili na hata rangi ya ngozi.

'Kulingana na Shirika la Afya Ulimwenguni, karibu wanawake 300,000 wanakufa kutokana na matatizo ya ujauzito.

Tumbo la uzazi la EctoLife limeundwa ili kupunguza mateso ya binadamu na kupunguza uwezekano wa kujifungua kwa upasuaji,' anaandika Al-Ghaili.

Badala ya mama kusukuma kwa uchungu na mwili wake, wanandoa wanatakuwa wanabonyeza kitufe ambacho kitawapa mtoto wao aliyepachikwa. Mradi huo pia umeundwa kwa ajili ya wanawake ambao wameondolewa mfuko wa uzazi kufuatia maswala ya kiafya, kama saratani,nk.

Al-Ghaili anaamini kwamba vifaa vya mfuko wa uzazi bandia vinaweza kuwa tiyari kabisa katika miaka 10 au zaidi ikiwa vizuizi vya maadili vitaondolewa.

"Kila kipengele kimoja kilichotajwa katika dhana kimekamilika na ni asilimia 100 ya sayansi na tayari kimefikiwa na wanasayansi na wahandisi", alisema.

"Kitu pekee kilichosalia ni kuunda mfano kwa kuchanganya vipengele vyote kwenye kifaa kimoja", mtengenezaji wa filamu alinukuliwa akisema.

Anasema mara tu vikwazo vya kimaadili vinapolegezwa, watu wanaweza kuwa tayari kutumia teknolojia hiyo katika siku za usoni.


Je, Wataalam wanasema nini?

Wataalamu wanaamini kuwa teknolojia hiyo sio ya mbali sana na inaweza kuwa ukweli katika siku zijazo. Andrew Shennan, profesa wa Uzazi katika Chuo cha King's London, aliiambia HuffPost, "Kwa mtazamo wa kinadharia inawezekana. Ni suala la kutoa mazingira sahihi na oksijeni na teknolojia zipo ili kuweza kufanikisha hilo.
 
Salama zaid ya uzazi wa asili?????? sidhani....anyway kama ni kwel bas ile SIKU ambayo hatujui saa yake itakuwa karibu sana kuliko tunavyodhani..
N.B:Ni mtazamo wangu tu..
 
Haya mambo sio ya kuleta complications ni kuangalia ni nini kinahitajika katika ukuaji wa mtoto na kama kinaweza kuwa replicated....

Mambo ya kuchagua ngozi na urefu na sijui nini yanafanyika hata sasa (wewe unavyochagua partner ndio unachagua aina ya mtoto) ukichagua mbantu mwenzako haiwezekani ukapata mzungu au mchina....

Kuna watu wanaitwa surrogate mothers kama mwanamke hataki kubeba ujauzito kuna surrogate mothers ambao fertilized eggs zinakuwa implanted ili wabebe ujauzito kwa miezi tisa...

Ndebile akizaliwa ambapo zamani angekufa sasa hivi anaweza kuwekwa kwenye environment ambayo atakuwa mkubwa...

Mwisho wa siku living things wapo pale ku-propagate (kuzaana) ili species yao isiwe instinct (hio ndio nature); kwahio kama mchungwa unaweza ukazaa through grafting (nadhani chungwa litakushukuru kwa kulisaidia kuliko process ingeanza kwenye mbegu)....
 
Haya mambo sio ya kuleta complications ni kuangalia ni nini kinahitajika katika ukuaji wa mtoto na kama kinaweza kuwa replicated....

Mambo ya kuchagua ngozi na urefu na sijui nini yanafanyika hata sasa (wewe unavyochagua partner ndio unachagua aina ya mtoto) ukichagua mbantu mwenzako haiwezekani ukapata mzungu au mchina....

Kuna watu wanaitwa surrogate mothers kama mwanamke hataki kubeba ujauzito kuna surrogate mothers ambao fertilized eggs zinakuwa implanted ili wabebe ujauzito kwa miezi tisa...

Ndebile akizaliwa ambapo zamani angekufa sasa hivi anaweza kuwekwa kwenye environment ambayo atakuwa mkubwa...

Mwisho wa siku living things wapo pale ku-propagate (kuzaana) ili species yao isiwe instinct (hio ndio nature); kwahio kama mchungwa unaweza ukazaa through grafting (nadhani chungwa litakushukuru kwa kulisaidia kuliko process ingeanza kwenye mbegu)....
Hapa umeeleza vizuri Sana mkuu.
 
Salama zaid ya uzazi wa asili?????? sidhani....anyway kama ni kwel bas ile SIKU ambayo hatujui saa yake itakuwa karibu sana kuliko tunavyodhani..
N.B:Ni mtazamo wangu tu..
Naunga mkono hoja."Siku za mwisho maarifa yataongezeka"
 
Duuu nami nabaki kushangaa kama wao wanavyonishangaa
 
Wanafunzi leo tutajifunza kuhusu watu

kuna wanaume na wanawake. Pia wanaume wa kigenetiki (laboratory man made human being) na natural human being.

Nawaza kwa maandishi.
Huyu unayemwona ni mwanamke chotara. Hana kibuli, hana kizazi na hatagi mayai, ameomgezewa joto na hana hedhi wala period wala siku za hatari. Ni kwaajili ya kiburudisho tu

Huyu ni mwanamke asilia. Anachangamoto za kula nauli, mbea, anapenda hela na kula chips. Huyu ni hatari ukikaa vibaya anakuchoma na gunia la mkaa.

Hujatulia unasikia FB mtu ameandika. Tunauza watu wa kisasa jinsia zote kwa bei nafuu

🤣🤣🤣🤣
Mwana wa adamu mpaka afike tutakuwa tumeona mengi ya doctor shika
 
Mwanateknolojia wa kibaolojia na mtayarishaji wa Filamu Hashem Al-Ghaili anatupeleka kwenye ziara isiyotulia lakini ya kuvutia ndani ya EctoLife - kituo cha kwanza cha uzazi wa mpango

EctoLife ni teknolojia itakayowapa wazazi wa siku za usoni njia mbadala inayodhaniwa kuwa salama zaidi ya uzazi wa asili, kuondoa matatizo ambayo mara nyingi huwa hatari yanayohusiana na uzazi.

Mfano kifurushi cha "Elite package" kitaruhusu watu kuchagua kiwango cha akili cha mtoto wao, urefu, nywele, rangi ya macho, nguvu za mwili na hata rangi ya ngozi.

'Kulingana na Shirika la Afya Ulimwenguni, karibu wanawake 300,000 wanakufa kutokana na matatizo ya ujauzito.

Tumbo la uzazi la EctoLife limeundwa ili kupunguza mateso ya binadamu na kupunguza uwezekano wa kujifungua kwa upasuaji,' anaandika Al-Ghaili.

Badala ya mama kusukuma kwa uchungu na mwili wake, wanandoa wanatakuwa wanabonyeza kitufe ambacho kitawapa mtoto wao aliyepachikwa. Mradi huo pia umeundwa kwa ajili ya wanawake ambao wameondolewa mfuko wa uzazi kufuatia maswala ya kiafya, kama saratani,nk.

Al-Ghaili anaamini kwamba vifaa vya mfuko wa uzazi bandia vinaweza kuwa tiyari kabisa katika miaka 10 au zaidi ikiwa vizuizi vya maadili vitaondolewa.

"Kila kipengele kimoja kilichotajwa katika dhana kimekamilika na ni asilimia 100 ya sayansi na tayari kimefikiwa na wanasayansi na wahandisi", alisema.

"Kitu pekee kilichosalia ni kuunda mfano kwa kuchanganya vipengele vyote kwenye kifaa kimoja", mtengenezaji wa filamu alinukuliwa akisema.

Anasema mara tu vikwazo vya kimaadili vinapolegezwa, watu wanaweza kuwa tayari kutumia teknolojia hiyo katika siku za usoni.


Je, Wataalam wanasema nini?

Wataalamu wanaamini kuwa teknolojia hiyo sio ya mbali sana na inaweza kuwa ukweli katika siku zijazo. Andrew Shennan, profesa wa Uzazi katika Chuo cha King's London, aliiambia HuffPost, "Kwa mtazamo wa kinadharia inawezekana. Ni suala la kutoa mazingira sahihi na oksijeni na teknolojia zipo ili kuweza kufanikisha hilo.
Hao watakuwa watoto au matoi?
 
Back
Top Bottom