Teknolojia isiathiri utu wetu, Polisi Tanzania msifanye kazi kwa mhemko. Trafiki 2 warudi Ofisini haraka

Yaani wewe ni zer,o brain. Kwahiyo kuna posho ya kuchomwa jua iliyohalalishwa na serikali sio?

Kwani hiyo kazi ya jeshi unafuatwa nyumbani kwenu kulazimishwa kuwa askari ama unaiomba na kuitafuta kwa kila njia?

Rushwa ni rushwa iwe kubwa au ndogo zote hazitakiwi.

Kazi ya ku deal na mikataba unayoiita kama DP world nakadhalika sio kazi ya polisi kuchunguza kuna idara zinazohusika na mambo ya uchunguzi wa rushwa ungewatupia lawama hao.

Jeshi la polisi kazi yao ni kukamata mtu aliyeamriwa akamamtwe kwa kosa fulani.
 
Na wananchi tutahamasishana kuvhukua video za ushahidi wa wala rushwa wote tunaokutana nao iwe barabarani ama maofisini.

Haiwezekani askari asimamishe gari badala aende kufanya ukaguzi yeye anasimama mbali ili kondakta amfuate ampelekee elfu mbili ya rushwa halafu gari tayari inakuwa nzima inaendelea na safari. Rubish.
 
H
ivi vipesa vya kiwi na maji mimi huwa hata simaindi sana Kwakweli.
Huyo jamaa aliyerekodi huenda amekataliwa au ameachwa !

Nenda karekodi mikataba mikubwa mikubwa ya madini na Gesi na mengineyo !
Hivi vijihela vya maji na kiwi we are not interested at all !
Watu wanahenya juani sio mchezo !
Muwe na huruma nanyi mtahurumiwa na Mungu !
Watanzania ni Asili yetu kusaidiana !
Mabig Fish yanachekelea tu na mabilioni yao nobody can touch them !
Wale wa vijihela hela ndio wanahenyeshwa ! Acheni hizo Bandugu we are not interested in this issue at all !
 
Mwizi anakuwa mwizi pale anapokatwa not before that, rushwa no matter how petty ni rushwa tu.
Hypocrisy ni pale polisi wanapojifanya kama hili ni kitu kisicho common, it's an open secret kwamba what we saw in that clip ndiyo order of the day na baadhi ya hayo makusanyo huenda kwa 'bosi' anayewapanga sehemu(strategically) za kukusanyia hizo bribes.
Inauma kwamba masuala makubwa(uhalifu mkubwa unaofanywa na dola) polisi huwa hawazingumzii kabisa na tatizo ni upumbavu wa raia wa Kitanzania kwani huyachukulia kisiasa badala ya kuyachukulia kibinadamu. Mtu katekwa live anapelekwa kuuawa and nobody knows kwamba kabla ya kuuawa atakuwa amepitia physical or mental torture za kiwango kipi lakini utaona 'mbwa watu' wakijifanya spin masters 'huo utakuwa ni ugonvi wao within their own party' ili tu kulinda serikali/chama tawala/vyombo vya ulinzi na usalama.
Wote tunajua kwamba uhalifu ambao serikali haihusiki lazima polisi waweke pressure kubwa, press conferences uchwara lazima zitakuwepo ila sasa brainwashed motherfvckers ambavyo kwa upuuzi wa ushabiki wa kisiasa hujaribu shamelessly kuilinda serikali kwenye kuhusika na uhalifu.
Just imagine juzi hapa Mtanzania anatekwa, a popular Tanzanian for that matter na utekaji unakuwa na public attention kuanzia Kenya mpaka Tanzania na mpaka kwenye baadhi ya vyombo vya habari vya kimataifa lakini hata embassy(consulate) ya Bongo pale Nairobi hautoi tamko lolote kwa kuwa wanajua ni uhalifu unaofanywa na serikali yao.
Watanzania wenyewe ndiyo wanaolea ujinga wote huu, you reap what you sow.
 
Duh 🙄 !
Kwakweli 😱
 
Kosa ni kosa lakini Kwakweli we are not interested na vijikosa kosa hivi vinavyohusu vijipesa pesa vya maji na kiwi Wajameni !
We are not interested in this issue at all !
Madini ya dhahabu na Gesi hapo poa !
 
Hata vibaka huwa wanahenya sana kabla ya kufanikisha mission zao lakini haohao polisi wapokea rushwa wakiwakata wanaeatesa mpaka wengine wanapoteza maisha.
Unajua hustles za kukesha usiku kivunja madirisha ya watu ili mtu aibe simu au mkoba ambapo akishikwa anachomwa moto? It's a very pretty crime lakini haiondoi ukweli kuwa ni uhalifu. Mwizi wa kuku au anayeiba nyanya tatu shambani kwa mtu akishikwa anachomwa moto lakini wezi wakubwa wa mikataba hewa and the likes wako na suti zao wanakula viyoyozi lakini haiondoi ukweli kwamba hata hao wezi njaa ni wezi tu.
Haijalishi unaiba kwa kuwa nyumbani hakuna unga watoto wamekesha na njaa, wizi wa kuku au rushwa ya buku vyote ni uhalifu tu(according to the law) na hatua stahiki zinapaswa kuchuliwa ila wezi wakubwa(hapa namaanisha watu wenye madaraka makubwa wanaohusika na mikataba na wale wanaopanga utekaji na uuaji wa wakosoaji wa serikali) nao inapaswa wachimbwe kwa kina wakamatwe watiwe hatiani.
 
Your browser is not able to display this video.
 
Your browser is not able to display this video.
 
Upo sahihi 💯 %. Tanganyika kila mtu anapora, chochote kilicho mbele yake. Wakubwa wanajibebea. Madini, Magogo, Mikataba, Wanyama, nk. Wadogo nao wanajihudumia. Niliwahi kumpa lift Traffic mmoja saa 10 jioni, akiwa amechanganyikiwa hajafikisha idadi ya magari aliyoamuriwa kuyakamata ili ampelekee Boss wake mgao. Tanganyika ni Taifa kama pori la kujiokotea matunda pori ya bure. Kuwalaumu hao Traffic sio sawa.
 
Traffic police anashinda juani vumbi lake jua lake mvua yake afu kwa mwezi unampa laki 6..uonevu mkubwa.

ndiyo maana mie huwapa walau hela ya maji nikijisikia - hawa jamaa wanasota sana.

hawa wawili waachieni haraka.
 
Kwanini unaiita Rushwaa?

Waanze na Big Fish kama they want to solve
Shurwa ni rushwa, unaanza na palipo na ushahidi. It's very true madhara ya 'rushwa kubwa' zinazofanywa na the so called big fish ni makubwa sana lakini pia hawa small fish when you sum up pia madhara ya ni makubwa kwani hizo elfu mbili zinazokusanywa on daily basis katika kila kona ya nchi ki total ya kiasi gani per week.
Tusihalalishe uhalifu kisa tu ni uhalifu mdogo, dogo flani hana mboga nyumbani anaiba kuku au mayai anachomwa moto lakini alikuwa aki-hustle mlo wa siku hiyo ila mwizi wa mikataba analindwa na mfumo. Ndiyo uhalisia on the ground.
 
Traffic police anashinda juani vumbi lake jua lake mvua yake afu kwa mwezi unampa laki 6..uonevu mkubwa.

ndiyo maana mie huwapa walau hela ya maji nikijisikia - hawa jamaa wanasota sana.

hawa wawili waachieni haraka.
Waacheni haraka sisi tunawasaidia wenyewe hawatulazimishi
 
Nakumbuka Rais wa awamu ya tano JPM aliibariki na kuita posho ya kusafisha viatu,lini baraka hiyo ilitenguliwa? Waachwe wajikimu kazi yao ni ngumu sana.
 
Walikua wanawachangia mchango wa harusi sio rushwa warudishwe uraiani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…