Uchaguzi 2020 Temeke: Kadawi Lucas Limbu, aliyetia nia kugombea Ubunge wa CHADEMA 2020 ahamia CCM

Uchaguzi 2020 Temeke: Kadawi Lucas Limbu, aliyetia nia kugombea Ubunge wa CHADEMA 2020 ahamia CCM

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
2020-09-08 (2).png

Mwaka 2010 alikuwa Mgombea Ubunge Jimbo la Temeke kupitia CUF, kutokana na kutofutwa kwa demokrasia, na uchaguzi huu alikuwa mgombea Ubunge Jimbo la Temeke kupitia CHADEMA.

Kutokana na kuwa Demokrasia ndani ya Vyama vya Upinzani haipo, leo ameamua kujiunga CCM

Amejiunga katika mkutano wa Mgombea mwenza wa Urais, Samia Suluhu, Kigamboni Dar-es-Salaam

======

Dare es Salaam.

Aliyekuwa Mtia nia kutaka kugombea Ubunge Jimbo la Temeke kwa Tiketi ya Chama cha Maendeleo na Demokrasia (CHADEMA) Lucas Limbu amtangaza kukihama Chama hicho na kuhamia Chamaa cha Mapinduzi (CCM) kutoka na kile alichodai kuwa kukosekana kwa Demokrasia ya kweli ndani ya Chama hicho.

Limbu ametoa kauli hiyo leo Jumanne Septemba 8 katika mkutano wa uzinduzi wa Kampeni za Chama cha Mapinduzi Jimbo la Kigamboni mbele ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan aliyefika kuzindua rasmi Kampeni hizo.

Amedai kuwa Vyama vya upinzani vinajaribu kufanya kampeni huku wakijuwa kuwa lengo lao ni kutaka kuwa na idadi kubwa ya wabunge wakiwemo wale wa viti maalumu ili baadae waweze kupata ruzuku kutoka Serikalini kutokana na nafasi za viti vya ubunge walivyopata.

“Nimeamua kuondoka CHADEMA kutokana na kukosekana kwa Demokrasia ndani ya Chama, Makamu Mwenyekiti Bara ambaye pia ni mgombea wa Urais wa Chama hicho Tundu Lissu antangaza kutaka haki huku ndani ya Chama hakuna haki wala Demokrasia” amedai Limbu.
WhatsApp+Image+2020-09-08+at+5.51.38+PM.jpeg
Screenshot_20200908-153803_1599570604359.jpg
 
Makelele yanaonyesha Chadema inashinda , but in reality uchaguz huu ndo utakuwa biggest Chadema nockout , hakuna matumaini yyte ya ushindi Kwa Chadema , wamebak Tu kuvitishia vyombo vya usalama na NEC, mfa maji haachi kutapatapa , but miraculously Chadema escaped total sinking by appointing TL to lead the worst
 
Ameafanikiwa kufikia ndoto yake kisiasa. Hongera zake.
 
Anasogeza jina lake karibu na chama tawala! ili wakirudi madarakani apate uteuzi! Njaa mbaya sana
 
Usipoitaja chadema unawashwawashwa, mgombea wa chadema Temeke anaitwa SINA SAID MANZI na wala si huyu uliyemtaja hapa.
Mkuu wanapotumwa huoneshwa kwa vidole hivyo wao hujitia maneno kinywani ili kumpendezesha mkuu
 
Back
Top Bottom