Ten Hag ana mechi mbili tu Man United

Ten Hag ana mechi mbili tu Man United

jjackline

Senior Member
Joined
Jul 25, 2024
Posts
111
Reaction score
274

Mchezaji wa zamani wa Newcastle United na timu ya taifa ya England, Alan Shearer amesema kocha wa Manchester United, Erik ten Hag ana michezo miwili pekee ya kuokoa kibarua chake.

Man United ambayo kwa sasa inashika nafasi ya 14, katika mechi tatu za mwanzo za EPL imeshinda moja na kupoteza mbili.

Kutokana na kuanza vibaya, wachambuzi na mashabiki wengi wamekuwa wakimshambulia Ten Hag wakiamini yeye ndio tatizo kwani timu imetumia zaidi ya Pauni 200 milioni kwa ajili ya kufanya maboresho mbalimbali ikiwa pamoja na kuwasajili Joshua Zirkzee, Leny Yoro, Manuel Ugarte na Matthijs De Ligt.

Ripoti zinadai Ten Hag yupo kwenye presha kubwa ya kufutwa kazi ingawa baadhi ya viongozi wa juu wa timu hiyo bado wanataka aendelee na wana imani naye.
Kwa upande wake Shearer anaamini kocha huyo ana michezo miwili tu inayofuata kuamua juu ya hatma yake ikiwa atabakia au laa.
Snapinsta.app_458188810_1027770959045088_3258208450911941679_n_1080.jpg
 
Kwa wale ambao hawaelewi kitu naomba leo nijaribu kutoa ufafanuzi kuhusu sakata lililopo kati ya kocha mkuu Ten Hag na club hiyo ya Man utd: Hivi karibuni kumekuwa mfululizo wa matokeo mabovu ya kikosi hicho ila za ndani kabisa ni kwamba badala ya kufanya kazi kwa bidii ujikwamue kwenye umasikini uko bize unasoma comment yangu, kwani itakusaidia nini? Nenda kafanye kazi acha kushinda mitandaoni
 
Shida ni kupata mtu wakuirudisha man u kwenye zama zile ndio shida
Usisahau tena hag kawalaza na kombe msimu uliopita man u sio Azam au yanga wao wanaamini huenda kesho ikawa Bora
 

Mchezaji wa zamani wa Newcastle United na timu ya taifa ya England, Alan Shearer amesema kocha wa Manchester United, Erik ten Hag ana michezo miwili pekee ya kuokoa kibarua chake.

Man United ambayo kwa sasa inashika nafasi ya 14, katika mechi tatu za mwanzo za EPL imeshinda moja na kupoteza mbili.

Kutokana na kuanza vibaya, wachambuzi na mashabiki wengi wamekuwa wakimshambulia Ten Hag wakiamini yeye ndio tatizo kwani timu imetumia zaidi ya Pauni 200 milioni kwa ajili ya kufanya maboresho mbalimbali ikiwa pamoja na kuwasajili Joshua Zirkzee, Leny Yoro, Manuel Ugarte na Matthijs De Ligt.

Ripoti zinadai Ten Hag yupo kwenye presha kubwa ya kufutwa kazi ingawa baadhi ya viongozi wa juu wa timu hiyo bado wanataka aendelee na wana imani naye.
Kwa upande wake Shearer anaamini kocha huyo ana michezo miwili tu inayofuata kuamua juu ya hatma yake ikiwa atabakia au laa.
Hahahaha 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 hahaaaaaaaaaaaa..
 
Nimepoteza imani na huyu jamaa kwenye mechi na brighton, jamaa amekalili kwamba kuna wachezaji wake ni lazima wacheze, alimtoa magwaya na amad ili tu de ligt na antony wacheze lakini ukiangalia hao waliotoka walikua wanacheza vizuri tu. Amekalili mc tomnay anafunga magoli muhimu bila kupiga hesabu timu inachezaje matokeo yakr kamtoa bruno ambae ndie anaunganisha timu kamuingiza mctomnay ambae ana zali tu la kufunga, mwishoe tukapigwa
 
Man United nao wamezidi ubabaishaji. Ten Hag sio kocha wa kuifundisha timu kaliba ya Man United. Hivyo hayo matokeo ni halali kabisa na wakimbakiza hadi mwisho wa ligi wataishia kushika nafasi ya 10 msimu huu.
 
Back
Top Bottom